• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

Imewekwa: April 29th, 2025

Afisa Mwandikishaji wa Jimbo la Lupa Wakili Athuman Bamba, amewataka walioteuliwa na Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi kufanyakazi ya Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la wapiga kura awamu ya pili kufanya kazi kwa weledi, umakini na ufanisi wa hali ya juu kwani Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi imewaamini na ina Imani watatekeleza kazi hiyo kwa maslahi ya Taifa la Tanzania

Ametoa kauli hiyo mapema leo 29/04/2025 wakati akifungua mafunzo ya waandishi wasaidizi na waemdesha vifaa vya Bayometriki wanaotarajiwa kuongoza zoezi la uboreshaji wa Daftari la kudumu la mpiga kura awamu ya pili linalotaraji kuanza tarehe 1/5/2025 na kuhitimishwa tarehe 7/05/2025

“Sasa hivi idadi yetu ni ndogo kuliko ilivyokuwa awali, hivyo ninyi mmeaminiwa sana na Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi kufanya kazi awamu hii ya Pili, Zingatieni mafunzo haya ili kazi yenu ikawe yenye ufanisi na weledi unaokususdiwa na Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi” Amesema Wakili Bamba

Dkt. Theodory Lukas ambaye ni moja kati ya wakufunzi wa Mafunzo hayo amewataka washiriki kutokupuuzia kila kinachofundishwa kwani Tume huru ya Taifa ya Uchaguzi wanajua umuhimu wa Ninyi kupewa mafunzo haya jambo lililopelekea kuitwa katika mafunzo hayo

Mwenyekiti wa Mafunzo Mw Isakwisa Kaminyoge kwa niaba ya wanasemina wote amewashukuru wakufunzi waliotumika kutoa mafunzo hayo lakini amewashukuru washiriki kutoa ushirikiano mkubwa wakati wa Mafunzo hayo  huku akisisitiza washiriki wote wa Semina kwenda kuyatendea kazi mafunzo hayo watakapokuwa wanatekeleza zoezi la uboreshaji wa Taarifa katika Daftari la Kudumu la mpiga kura awamu ya pili

Jimbo la Lupa linataraji kuwa na vituo ishirini na sita (26) ambapo kata kumi na sita (16) zitakuwa na kituo kimoja kwa kila kata kitakachotumika katika uboreshaji (Ofisi za Kata) wakati kata za Kambikatoto, Mafyeko na Mamba kwa Tarafa ya Kipembawe na Kata za Matundasi Chokaa na Sangambi kwa tarafa ya Kiwanja zitakuwa na vituo viwili kwa kila kata

Mafunzo hayo yametolewa leo katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya  (Sapanjo) yakiwahusisha maafisa waandikishaji wasaidizi ngazi ya Kata, waandishi wasaidiizi ngazi ya vituo pamoja na waendesha vifaa vya Bayometriki huku zoezi la Uboreshaji wa Daftari la Kudumu la Mpiga kura awamu ya pili likitaraji kuanza rasmi tarehe 01/05/2025 na kutamatika tarehe 07/05/2025

Afisa Tehama Kutoka Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ndugu Salim Hassan Mohamed akifafanua jambo wakati wa mafunzo kwa Maafisa waandikishaji wasaidizi ngazi ya kata, waandishi wasaidizi wa vituo na waendesha vifaa vya Bayometriki

Wahiriki wa Mafunzo wakila kiapo tayari kwa kazi ya Uboreshaji wa Daftari la kudumu la Mpiga kura awamu ya Pili Jimbo la Lupa

Washiriki wakiendelea na mafunzo kwa Vitendo tayari kwa kazi ya Uboreshaji wa Daftari la kudumu la mpiga kura linalotaraji kuanza tarehe 1/05/2025 na kutamatika tarehe 7/05/2025

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.