Hakim Mkazi mfawidhi wa Mahakama ya wilaya ya Chunya Mhe James Julius Mhanusi amesema Mahakama ya wilaya ya Chunya kwa mwaka huu wa mahakama imejipanga kuhakikisha inamaliza mashauri yote yatakayofunguliwa ndani ya mwaka, jambo litakalopelekea kumaliza mwaka wakiwa na mashauri sifuli.
Ametoa kauli hiyo mapema leo 02.02.2026 katika viwanja vya msufini vilivyopo kata ya Lupa tarafa ya kipembawe wakati wa maadhimisho ya kilele cha wiki ya Sheria Nchini ambapo Halmashauri ya wilaya ya Chunya imesherekea wiki hiyo katika viwanja hivyo
“Mwaka jana tumehama na mashauri machache sana kwa mahakama ya wilaya, Mahakama zetu za Mwanzo walihama na mashauri ziro, Mahsuari Ziro maana yake hawakuhama na shauri hata moja yaani mashauri yote yaliyofunguliwa kwenye mahakama za mwanzo Chunya yalimalizaka ndani ya mwaka husika, Hivyo na sisi Mahakama ya wilaya tumejipanga kumaliza mwaka huu tukiwa tumesikiliza mashauri yote tofauti na mwaka uliopita ambapo Mahakama ya wilaya ilihama na mashauri 73” Alisema Mhe Mhanusi
Aidha Mhe Mhanusi amesema katika kuadhimisha kilele cha wiki ya Sheria, wamewatembelea wagonjwa waliokuwepo katika kituo cha Afya cha Lupa na kuwakabidhi vitu mbalimbali ikiwa ni kuwajali na kushiriki nao katika nyakati zao za kuugulia jambo ambalo linalopaswa kuwa funzo na kwa wengine kukumbuka kuwajali wengine kutokana na kidogo ambacho Mungu amewajalia.
Naye Bi Kissa Ngoloke kutoka TAKUKURU wilaya ya Chunya amewataka wanaChunya kuwa wazalendo na wenye maadili katika maeneo yote akitaja mchango mkubwa wa Mambo hayo mawili katika kupambana na Rushwa huku akisisitiza kwamba Rushwa ndiye adui Mkubwa wa haki, hivyo ametaka wanaChunya kuendelea kupambana na Rushwa kwa nguvu.
Wakili wa kujitegemea Mhe Jacqueline Massawe akimuwakilishi Rais wa Chama cha wanasheria Tanganyika (TLS) amesema wanachunya waendelee kuwatumia na kuwaamini mawakili katika shughuli zao mbalimbali jambo litakaloendelea kulinda haki zao na kupelekea maendeleo makubwa ya mtu mmoja mmoja na hatimaye Taifa kwa ujumla
Sherehe za Kilele cha wiki ya Sheria Nchi zimeadhimishwa kwa shughuli mbalimbali ikiwepo kutoa Elimu ya sheria kwa wananchi, kufanya matendo ya huruma na mambo mengine mengi. Katika wilaya ya Chunya sherehe zimefanyika kata ya Lupa eneo la Msufini, huku kauli mbiu ya Maadhimisho hayo ikiwa ni “Mchango wa Mahakama katika maendeleo ya Taifa”

Mhe James Mhanusi Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya wilaya ya Chunya akizungumza wakati wa Kilele cha wiki ya Sheria Lupa

Baadhi ya Viongozi wakiwa kwenye picha ya Pamoja wakati wa Kilele cha wiki ya Sheria wilayani Chunya
Itigi Road
sanduku la posta: P.O box 73 Chunya
simu ya mezani: 025 2520121
simu ya mkononi: 025 2520121
Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz
Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.