• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

‘UZOEFU UWEKWE PEMBENI’

Imewekwa: January 19th, 2026

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mhe Kelvin Nshinshi amewataka Madiwani wazoefu na wapya kwa Pamoja kupokea mafunzo na maelekezo ya utekelezaji wa majukumu yao katika nyadhifa zao walizoaminiwa na wananchi huku akiwakumbusha kwamba uzoefu wa miaka uliopita uwekwe pembeni ili kupokea maelekezo mapya

Ametoa rai hiyo leo tarehe 19.1.2026 kwenye ukumbi wa mikutano Usungilo Mbeya wakati wa Mafunzo ya Madiwani ambayo yanatolewa na wataalam kutoka Chuo cha Serikali za Mitaa huku mafunzo hayo yakikusudiwa kuhusisha mada mbalimbali zikiwepo maadili ya madiwani, bajeti na amambo mengine mengi

“Madiwani wazoefu naomba sana, ule uzoefu uliokuwa nao uuache pale mlangoni, ukiingia hapa ukumbi sisi sote yaani madiwani wazoefu na sisi wapya sote tusikilize, tufuatilie na tuwe makini ili tupate ujuzi wa Pamoja utakaotusaidia kutekeleza majukumu yetu huku kwenye kata zetu tulikoaminiwa na wananchi wetu” Amesema Mhe Shinshi

Mratibu wa Mafunzo kutoka OWM-TAMISEMI Bi. Yustina Bubinza kwa niaba ya wakufunzi wote amewataka Madiwani wote kuwa tayari kupokea mafunzo hayo huku akiwataka kuwa huru kuuliza na kutoa maoni ili kuendelea kuboresha zoezi la ujifunzaji kama ilivyokusudiwa kwani kwa kufanya hivyo itasaidia kutukumbusha Zaidi wakati wa utekelezaji wa Majukumu

Mkuu wa Idara ya Utumishi na utawala wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Jumanne Chaula kwaniaba ya Mkurugenzi mtendaji amewapongeza Madiwani wote walioaminiwa na wananchi na Serikali kwa ujumla wake kuongoza kata hizo hivyo ameahidi ushirikiano mkubwa wakati wote wa utekelezaji wa majukumu yao yote kwa kipindi ambacho watakuwa wanaongoza kata zao

Naye Diwani wa Kata ya Mamba Mhe Ramadhan Shumbi ambaye ameteuliwa na wanasemina kuwa mwenyekiti wa Mafunzo amesema mafunzo hayo yatawasaidia Madiwani kutambua majukumu yao na kutekeleza ipasavyo lakini pia Mafunzo yataondoa mivutano isiyo ya lazima ya viongozi na wananchi wake au viongozi kwa viongozi wao kwa wao

Mafunzo kwa Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya yanafanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Usungilo uliopo jijini Mbeya yakitarajiwa kuongeza uelewa kwa madiwani wote wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya tayari kutekeleza majukumu waliyoaminiwa na wananchi wao

Bi Yustina Bubinza Mratibu wa Mafunzo kutoka OWM TAMISEMI akizungumza na Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya wakati wa ufunguzi wa Mafunzo ya kuongeza uwezo na utendaji 

Mkuu wa Idara ya Utumishi na utawala wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Jumanne Chaula akizungumza na wanasemina (Madiwani) wakati wa ufunguzi wa Mafunzo

Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya wakiwa wanafuatilia maelekezo na mafunzo kutoka kwa wakufunzi wao

Mhe Ramadhan Shumbi diwani wa kata ya Mamba na Mwenyekiti mteule wa Mafunzo akizungumza na wajumbe wa Semina mapema leo

Matangazo

  • KUPIGA KURA YA RAIS KITUO AMBACHO HAUKUJIANDIKISHA September 15, 2025
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ‘UZOEFU UWEKWE PEMBENI’

    January 19, 2026
  • AFISA ELIMU MKOA WA MBEYA ATOA NASAA KWA WALIMU CHUNYA.

    January 16, 2026
  • KAMATI ZA UJENZI ZATAMBULIWA CHUNYA: MWENYEKITI ATUMA OMBI POLISI

    January 15, 2026
  • MKAWE MABALOZI WA MFUMO WA SIS KWA WALIMU WENGINE.

    January 14, 2026
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.