• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

Vivutio vya Utalii

FURSA ZA UWEKEZAJI KATIKA UTALII

Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ina vivutio vya asili vya utalii na yapo maeneo ya kutosha yenye vivutio kwa ajili ya shughuli za utalii.

1.0 Mlima Mwene.

Halmashauri imebarikiwa kuwa na  mlima mkubwa sana wa kihistoria ambao chifu wa  Bungu alitaka kuuhamisha kutoka Kipembawe kwenda Wilaya Songwe Kwimba ili autumie kuhutubia wananchi wake, watu wengi walikufa kwa ajili ya zoezi hilo la kuubeba mlima na kuuhamisha kwa kuangukiwa na mawe. Mlima huu upo katika Kata ya Mamba takribani km 80 kutoka makao makuu ya Wilaya. Inaonesha kwamba  katika mlima huu kuna nguvu ya asili zinazoambatana na machifu waliozikwa katika mlima huo, kumekuwa na maajabu mengi yakitokea katika mlima huo mfano kuku kuonekana akiwa na mguu mmoja n.k. unapoupanda utakutana na vivutio lukuki kama wanyamapori kama digi digi, Nyani, na aina mbalimbali za ndege kama Kanga, Kware na Njiwa wazuri. Mlima una sifa ya kuwa na kilele ambacho  hutumika kuangalia maeneo ya mbali

2.0 Bwawa la Viboko Nzingwa.

Halmashauri ya Wilaya ya Chunya  imejaliwa kuwa na Bwawa kubwa la wanyama aina ya Viboko, wanyama hawa imekuwa kivutio kikubwa cha watalii kutokana na muonekano wao, Inashauriwa kuwa eneo hili linatakiwa kuhifadhiwa kwani ni kivutio kikubwa cha utalii kutokana na aina hiyo ya wanyama kuwepo humo.

 

3.0 Pango la Kipembawe lililomeza watoto.

Wilaya ya Chunya ina pango la ajabu lililomeza watoto, pango hili linalopatikana katika kata Mafyeko Tarafa ya Kipembawe.  Pango la Kipembawe limetokana jina la Tarafa hiyo. Pango hilo lina mwonekano mzuri wa kiutalii na unapolichungulia unaweza kuona giza nene ndani yake. Pango hili lina maajabu mengi sana ambapo ukifika katika eneo hili utajulishwa mambo mengi sana kuhusu historia ya pango hili.

 4.0 Uwindaji wa kitalii.

 Wilaya ya Chunya ina vitalu vizuri vya uwindaji wa kitalii ambapo Shughuli za uwindaji wakitalii hufanyika kila mwaka kuanzia mwezi julai hadi disemba. Uwindaji wa kitalii imekuwa kivutio kikubwa sana cha wageni. Shughuli za uwindaji wa kitalii zinafanikiwa kutokana na idadi kubwa ya wanyama wanaopatikana katika maeneo ya uwindaji. Wanyama wanaowindwa zaidi ni samba, nyati, chui palahara na kongoni wanyama hawa wanapatikana kwa urahisi hivyo kuvutia idadi kubwa ya wageni.

 

 

 

 

5.0 Soko la Dhahabu. (Utalii wa Madini)

Wilaya ya Chunya imekuwa ni eneo moja wapo lililobarikiwa kuwa na madini ya Dhahabu. Shughuli za uchimbaji wa madini zinazofanyika wilaya ya Chunya imekuwa ni kivutio kikubwa cha utalii,  hadi sasa kuna soko kubwa la dhahabu  linalopatika wilayani hapa ambapo shughuli za uuzaji na ununuzi wa dhahabu hufanyika. 

Wilaya ya Chunya ina idadi kubwa ya mashine za uchakataji wa dhahabu kuna idadi kubwa ya makarasha yanayotumiwa na wachimbaji kwaajili ya uchakataji wa dhahabu. Wilaya bado inamaeneo makubwa ambayo yanahitaji uwekezaji kama vile mashine za kisasa kwaajili ya uchakataji wa dhahabu ,  n.k.

6.0 Ngoma za asili (Utalii wa utamaduni)

Wilaya ya Chunya imebarikiwa kuwa na ngoma maarufu za makabila makubwa yanayopatikana wilaya ya chunya ni pamoja na Waguruka na Wakimbu pamoja na makabila mengine yaliyohamia kama wangoni ngoma hizi zina mvuto sana kutokana na mazingira yake,   Ngoma ya wakimbu zinapatikana zaidi katika tarafa ya Kipembawe, ngoma nyingine maarufu zinapatikana Chunya Mjini,  ngoma hizi huchezwa na kabila la wangoni ambao kwa umoja wao hutumia vifaa kama filimbi zinazotokana na vibuyu ambavyohufungwa na naironi kwa lengo la kutoa sauti yenye mvuto, nyimbo nzuri huimbwa kulingana na matukio kama ni matukio ya sherehe za harusi basi nyimbo zenye mafunzo ya ndoa huimbwa na kama matukio ni ya huzuni hakika nyimbo za huzuni huimbwa zikiambatana na uwiano wa stepu unaofanana .

7.0 JENGO LA MAKUMBUSHO.

Wilaya ya Chunya imebarikiwa kuwa na jumba la makumbusho ambapo  vitu vya kale, kazi za sanaa, na taarifa mbali mbali kuhusu vivutio mbalimbali vya utalii zinapatikana. Aidha jumba la makumbusho lina mkusanyiko wa taarifa za kiutamaduni na mazingira asilia na wenyeji wa Chunya kabla na baada ya uhuru. Jumba la Makumbusho lina vitu asilia vilivyo tumika enzi za babu zetu wa kale mfano kuna nguo ya magome ya miti iliyovaliwa miaka ya 1800 iliyo ambatana na historia yake ambayo hadi sasa ina miaka takribani 200.


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.