• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

WADAU WA MICHEZO WAWAGUSA WANAFUNZI WENYE MAHITAJI CHUNYA.

Imewekwa: February 13th, 2026

Wadau wa michezo Wilayani Chunya wameungana na kuwasaidia wanafunzi wenye mahitaji maalumu na wanaoishi katika mazingira magumu kwa kuwapa vifaa mbalimbali ikiwa ni pamoja na madaftari , kalamu , mashati ya  shule , mchele, mafuta , sabuni na mahitaji mengine ambayo yatawasaidia wanafunzi hao kukidhi mahitaji yao.

Wadau hao wa michezo  kutoka Mbeya motor sport club, Ngindo campany limited, Mapesa company  limited na Nyondo company limited  wametoa vifaa vya hivyo pamoja na chakula leo tarehe 13/02/2026 katika Shule za msingi sita (6) zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Chunya.

Mkuu wa kitengo cha utamaduni Sanaa na michezo wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya Bi Coretha Kalanje pamoja na kuwashukuru wadau hao wamichezo kwa misada mbalimbali waliyoitoa kwa wanafunzi wenye mahitaji ,pia ametoa rai kwa wadau wengine kuendelea kujitokeza katika kuendeleza sekta ya michezo  ili kudumisha umoja, ushirikiano na  utamaduni kwa usatawi wa jamii katika nyanja za kiuchumi na  burudani

Afisa elim Maalum Wilaya ya Chunya Bi Hawa Mtonyole amesema kuwa jumla ya wanafunzi 252 wamenufaika na misaada ya wadau hao huku akiwaomba  wadau wengine kuendelee kujitokeza na  kuwasaidia wanafunzi wanaotoka kwenye mazingira magumu na wenye mahitaji maalum kwani bado watoto hao wanauhitaji mkubwa.

“Tunawashukuru sana wadau kwa kuwaona watoto hawa wenye mahitaji  kwa kuwapa madaftari na vifaa vingine kwani vitawasaidia katika masomo yao ikiwa ni pamoja na kuandika , pia tunawashukuru wadau kwa kutuletea chakula kwa watoto wenye mahitaji maalum hapa Shule ya msingi kibaoni kwani wanauhitaji mkubwa wa chakula lakini pia bado tuna wanafunzi  wengine wenye mahitaji maalum katika kituo cha lupa tingatinga na Makongolosi” Amesema Mwl Mtonyole

 Wakizungumza kwa nyakati tofauti tofauti wadauhao wa michezo  ndugu Steven Nyondo , ndugu  Alex Mpoma  , Wesday Nyondo, Joyce Ndolela  wamesema kuwa mbali na kuwa wameandaa mashindano ya mchezo wa magari (drift) lakini pia wao kwa umoja wao wameona  nivema kuwatembelea na kuwasaidia wanafunzi wenye mahitahi maalum na wanaoishi kwenye mazngira magum ili kuweza kuwasaidia mahitaji yao .

Mwalim Mkuu msaidizi wa Shule ya Msingi Mbugani Mwalim Jocia Ndalo amesema kuwa vifaa walivyopoewa wanafunzi wenye mahitaji maalum na wanaoishi mazingira magumu vitawasaidia kutatua changamoto zilizokuwa zikiwakabili ikiwa ni pamoja na kushindwa kuandika kwasababu yakukosa madaftari  pamoja na adha nyingine.

Wakizungumza kwa niaba ya wanafunzi wengine bi Sheila Amon  na Ndugu Ezekiel Elias wamewashukuru wadau wa michezo kwa misada mbalimbali waliyoitoa ikiwa ni pamoja na madaftari kalam, soksi  masharti ,chakula na vifaa vingine huku wakiahdi  kusoma kwa bidi ili waweze kutimiza ndoto zao.

Mchezo wa magari( drif ) ulioandaliwa na wadau wa michezo unaotarajia kufanyika tarehe 14/02/2026 ambapo leo tarehe 13/02/2026 wadau hao wamewatembelea wanafunzi wenye mahitaji maalum na wanaoishi mazingira magum na kuwapa vifaa mbalimbali vya Shule pamoja na chakula  katika shule sita (6) za msingi ikiwa ni pamoja na Shule ya msngi Chokaa, Kibaoni, Kiwanja, Mbugani Chunya Mjini na Chunya kati .

Mwenyekiti wa Mbeya Motor sport club Ndugu Steven Nyondo akikabidhi madaftari na kalam bi Sheila Amoni  mmoja ya wanufaika wa msaada huo kkatika Shule ya msingi Chokaa.

Baadhi ya misaada iliyokabidhiwa kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum Shule ya msingi kibaoni ikiwa ni pamoja na Sabuni, Mchele , mafuta ya kupikia, madaftari, na vitu vingine .

Wanafunzi wa Shule ya Msingi Mgugani wakiwa wameshika madaftari, kalamu ,rula na penseli vifaa ambavyo wamekabidhiwa na wadau wa michezo ili kutatua baadhi ya changamoto zinazowakabili wanafunzi hao.

Matangazo

  • AJIRA ZA MKATABA KWA WALIMU January 20, 2026
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • WADAU WA MICHEZO WAWAGUSA WANAFUNZI WENYE MAHITAJI CHUNYA.

    February 13, 2026
  • MAHAKAMA CHUNYA IMEJIPANGA KUMALIZA MASHAURI YOTE NDANI YA MUDA

    February 02, 2026
  • CHUNYA YAMSHUKURU MHE RAIS KUWAKUMBUKA WALIMU WENYE MAHITAJI MAALUM

    January 27, 2026
  • KIFUATACHO CHUNYA SASA NI KAZI

    January 20, 2026
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.