• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

CHUNYA YAMSHUKURU MHE RAIS KUWAKUMBUKA WALIMU WENYE MAHITAJI MAALUM

Imewekwa: January 27th, 2026

Mkuu wa idara ya elimu ya awali na Msingi Mw Marko I. Busungu amewataka walimu waliopewa vifaa visaidizi katika kutekeleza majukumu yao kuhakikisha wanavitunza vizuri ili viweze kuwasaidia kwa muda mrefu kwakufanya hivyo watakuwa wamemtendea haki Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwani yeye ndiye aliyewapatia vifaa hivyo.

Ametoa rai hiyo mapema leo 27.01.2026 ofisi za Halmashauri ya wilaya ya Chunya wakati wa zoezi la kukabidhi vifaa hivyo kwa wahusika ili viweze kuanza kufanya kazi kama Serikali ilivyoelekeza.

“Naomba nitoe rai kwa walengwa wa vifaa hivi, wakatunze vizuri ili viweze kutumika kwa muda mrefu zaidi na kwakufanya hivyo mtakuwa mmemtendea haki Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwani yeye ndiye aliyetoa vifaa hivyo kwaajili ya matumizi yenu kuwarahisisha mkiwa mnatekeleza majukumu yenu ya kila siku” Amesema Mw Busungu

Aidha Mw Busungu ameishukuru Serikali ya awamu ya sita kipindi cha pili kuwakumbuka walimu wenye mahitaji maalum kwani nao ni watumishi kama watumishi wengine hivyo kuwapatia vifaa kutawapa uhuru wa kufanya kazi lakini pia watajiona nao kuwa sehemu ya jamii wanayoitumikia


Naye Afisa Elimu Maalum Bi Hawa Mtonyole amesema Halmashauri ya wilaya ya Chunya ina walimu wanne wenye mahitaji maalumu, wawili kati ya hao wamepatiwa vifaa visaidizi kama vile Kishikwambi Pamoja na Kompyuta Mpakato huku walimu wengine wakiendelea kusubiri vifaa hivyo kulingana na uhitaji walio nao.

“Chunya tuna walimu wanne wenye mahitaji maalumu. Mwalim Mwatimba yeye amepatiwa Kishikwambi, Mwalimu wa Bitimanya sekondari amepewa Kompyuta Mpakato wakati mwalim wetu wa Shule ya Sekondari Itewe atapatiwa Kitimwendo kwaajili ya kurahisisha utekelezaji wa majukumu yake, pia Mwalim mwingine mwenye ulemavu Ngozi naye atapatiwa. Mhe Rais amesema walimu wote wenye mahitaji maalum watafikiwa ili kurahisisha utekelezaji wa Majuku yao” Amesema Mw Mtonyole

Mwalim Edward Mwatimba ameishukuru Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwakuwakumbuka watu wenye mahitaji maalum na hatimaye kuwapatia vifaa visaidizi ambavyo vitasaidia wakati wa utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku

Halmashauri ya wilaya ya Chunya ndani ya siku 100 za Mhe Rais imepokea fedha, imepokea watumishi ajira mpya Pamoja na mambo mbalimbali na sasa watumishi walimu wenye mahitaji maalum wamefikiwa kwakupatiwa vifaa visaidizi.

Endelea kufuatilia mitandao yetu ili kujua mambo mengine mengi

Youtube: Chunyadc Online

Facebook: Chunya Dc na Halmashauri ya wilaya ya Chunya

Instagram: Chunyadc_official

Baadhi ya vifaa visaidizi walivyopatiwa walimu wenye mahitaji maalumu

Mw Hawa Mtionyole Afisa Elimu Maalum wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya wakati akifafanua jambo wakati wa zoezi la kukabidhi vifaa visaidizi kwa walimu wenye mahitaji maalum

Mw Abibu Edward Mwatimba wa Shule ya Msingi Kibaoni akitoa shukrani zake kwa niaba ya walimu wengine (Mkononi ameshika Kishikwambi) baada ya kukabidhiwa kifaa saidizi kwaajili ya matumizi yake

Matangazo

  • AJIRA ZA MKATABA KWA WALIMU January 20, 2026
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • CHUNYA YAMSHUKURU MHE RAIS KUWAKUMBUKA WALIMU WENYE MAHITAJI MAALUM

    January 27, 2026
  • KIFUATACHO CHUNYA SASA NI KAZI

    January 20, 2026
  • ‘UZOEFU UWEKWE PEMBENI’

    January 19, 2026
  • AFISA ELIMU MKOA WA MBEYA ATOA NASAA KWA WALIMU CHUNYA.

    January 16, 2026
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.