• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

ZAIDI YA HEKTA NANE ZA MISITU HUARIBIWA KILA MWAKA WILAYANI CHUNYA.

Imewekwa: June 6th, 2018



Zaidi ya hekta 8 za misitu huaribiwa kwa mwaka wilayani Chunya ambapo viongozi mbalimbali wametumia siku ya mazingira Duniani kuwaasa Wananchi kutumia  nishati mbadala ili kunusuru Wilaya kugeuka jangwa.
Kauli hizo zilitolewa jana katika maadhimisho ya siku ya mazingira Duniani ambapo Wilaya ya Chunya yalifanyika kijiji cha Soweto Kata ya Kasanga mgeni rasmi akiwa mkuu wa Wilaya ya Chunya Rehema Madusa ambaye alitumia fursa hiyo kusisitiza  kauli mbiu ya siku hiyo  Kimataifa iliyokuwa ikisema"Pambana na uchafuzi wa mazingira unaotokana na plastiki na kitaifa ni mkaa ni gharama tumia nishati mbadala".
Mkuu wa Wilaya ya Chunya Rehema Madusa alisema zaidi ya kilometa nane za misitu huharibiwa katika Wilaya ya Chunya na hali hiyo ikifumbiwa macho itasababisha Wilaya kugeuka kuwa jangwa .
Madusa alisema waachane na tabia za kufyeka misitu ovyo kwani watasababisha ukosefu wa mvua na kuharibu vyanzo vya maji,na alitumia fursa hiyo kuwaagiza watendaji kusimamia Sheria na atakaye kiuka achukuliwe hatua za kisheria mara moja.
Akizungumza kwa niaba ya wananchi diwani wa kata ya Kasanga Obed Mwangesile alishukuru maadhimisho hayo kufanyika katika Kata yake kwani wananchi wa Kata yake ni miongoni wa wanufaika na mazingira katika kutokana na shughuli za kibinadamu kama kilimo, Ufugaji na Uchimbaji Madini ya dhahabu ambapo alisema kupitia maadhimisho hayo wananchi  wamepata elimu ya mazingira.
 Awali  Ofisa mazingira Wilaya ya Chunya Yohana Ngurukia akielezea uharibifu wa mazingira katika Wilaya ya Chunya alisema unasababishwa na shughuli za kibinadamu kama uchimbaji madini, uchomaji mkaa na ufugaji mifugo wa kuhamahama ambao husababisha uchomaji misitu wakidai hufukuza adui wasidhuru mifugo.
Ngurukia alisema umefika wakati wa kuachana na matumizi ya nishati ya mkaa badala yake watumie nishati mbadala kama gesi,umeme ili kuokoa misitu iliyobakia.
Aidha kwaupande wake  Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya Sophia Kumbuli alisema  Halmashauri yake itaendelea kuzimamia Sheria ikiwa ni pamoja na kutoa elimu juu ya utunzaji wa mazingira na kuwataka watendaji wa vijiji wanawahimiza wananchi kufuata Sheria badala ya kuharibu mazingira.
Hata hivyo BI. Sophia Kumbuli alisema kuwa hivi karibuni walindesha mafunzo kwa vikundi vya ujasiriamali kwaajili ya kukabiliana na uharibifu wa mazingira kwa kuanza uzalishaji wa mkaa kwa kutumia taka ambao hautumii  nishati ya miti.  
Mwenyekiti wa Wachimbaji Mkoa wa Mbeya Leonard Manyesha alisema kupitia maadhimisho haya yeye kama Mwenyekiti atasaidia kuwaelimisha Wachimbaji ili kuhakikisha wanafuata Sheria na kwamba wanapaswa kufuata Sheria ili kuepuka uharibifu wa mazingira.
 Alisema Wachimbaji kuunga mkono juhudi za Serikali ili kuepuka uharibifu wa mazingira kwa kutotirisha maji ovyo kwenye machimbo na kufukia mashimo baada ya machimbo.
Mwisho.



Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.