• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

WATOTO WOTE WAPATE CHAKULA SHULENI

Imewekwa: July 21st, 2023

Katibu wa kikao cha cha tathimini ya Mkataba wa  lishe wilaya akimwakilisha Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Chunya ndugu Athumani Bamba amemwagiza kaimu afisa lishe wa wilaya ndugu Witness Kisukulu kuhakikisha anawaandikia barua watendaji wa vijiji na wakuu wa shule kuwataka wasimamie na kuhakikisha watoto wote wanapata chukula shuleni.


Maagizo hayo yametolewa  julai 20/07/2023 katika  kikao cha tathimini ya hali ya lishe wilaya  ikiwa ni kikao cha robo ya nne (4) kilichofanyika  katika ukumbi wa halimashari  ya wilaya ya chunya


“Kaimu Afisa lishe wilaya hakikisha unawaandikia watendaji na wakuu wa shule wote barua ipitie kwa mkurugenzi mtendaji wa halimashauri  ya kuwataka wasimamie na kuhakikisha watoto wote wanapata chakula shuleni kusiwepo na watoto ambao hawapati chakula wanapokuwa shuleni ukizingatia kipindi hiki ni kipindi cha mavuno kwahiyo ni kupambana kuhakikisha wazazi wanaleta chakula shuleni”


Mwenyekiti wa kikao ameongeza kuwa watendaji wa vijiji na kata waweke sheria ndogo ambazo zitawasaidia kusimamia  suala la  ukusanyaji wa chakula  shuleni ili kuwawezesha watoto wote kupata chakula  na kwa wazazi ambao watakaidi agizo hilo basi sheria ndogo zilizowekwa zitumike kuwachukulia hatua wazazi hao.


Naye kaimu Afisa lishe wa wilaya ndugu Witness Kisukulu amewataka watendaji  wa vijiji na kata kuendelea kuwaibua wototo wenye utapiamlo waliopo katika jamii ili wapatiwe matibabu  lakini pia kwendelea kutoa elimu ya lishe katika jamii ili kupunguza na kumalikza kabisa tatizo la utapiamlo kmali na udumavu katika jamii zetu’’


“watoto wenye utapiamlo kwenye jamii zetu bado wapo  hivyo watendaji tunapaswa kwendelea kutoa elimu ya lishe kuelimisha jamii  lakini pia kuibua watoto wenye utapiamlo ili waweze kupata matibabu  sambamba na kuhamasisha wakina mama wawanyonyeshe watoto kwasababu garama za utapiamlo ni kubwa”


Aidha afisa elimu awali na Msingi Ndugu Ferd Yona Mhanze ameeendelea kuwasisitiza  watendaji  wa kata na vijiji kushirikiana na wakuu wa shue kuhakikisha watoto wote wanapata chakula wanapokuwa shuleni na hiyo ni kwa shule zote za halimashuri ya wilaya ya chunya.


‘’Kwa  shule zile zenye watoto wenye mahitaji maalumu serikali  inawatambua  na  inawachangia kiasi cha Tsh 12000/= kila mwezi hii inaweza ikatumika kama mchango wake  wa chakula kwa mtoto ili kumsaidia mtoto mwenye ulemavu asipate usumbufu  wakukosa chakula anapokuwa shuleni’’


Aidha  ndugu Semwano Carlos Mlawa  akimwakilisha Mkuu wa Wilaya  ya halmashauri ya Chunya amezipongeza kata zilizofanya vizuri katika masuala ya lishe  kwa mwaka huu na kuwasihi waendelee kufanya zizuri huku akiwataka watendaji wa kata zingine kuhakikisha wanafanya vizuri katika masuala ya lishe kwa mwaka ujao.


Gervas Cosmas Mahellah akizungumza kwa niaba ya watendaji ameomba maagizo ambayo yametolewa kwenye kikao cha kamati  ya lishe  yaweze kubandikwa katika mbao za matanago za vijiji na kata ili  vikao vya halmashauri ya vijiji wanapokuwa wameketi waweze kuingiza na agenda ya chakula mashuleni.


Kikao hicho  cha kamati ya lishe kimehudhuriwa  na watendaji wa vijiji , watendaji wa kata , afisa elimu awali na msingi, Kaimu mganga mkuu na Kaimu katibu tawala wa wilaya. Kikao hicho kiliambatana na zoezi la ugawaji wa zawadi kwa watendaji wa kata ambao wamesimamia vizuri musuala ya lishe katika kata zao ambapo Watendaji wa kata za Mkola, Lupa na kata ya Nkung’ungu wamepata zawadi

Kaimu Afisa lishe wilaya ya Chunya Ndugu Witness Kisukulu akizungumza katika kikao cha tathimini ya makataba wa lishe cha Robo ya nne ya mwaka 2022/2023 kilichowahusisha watendaji wa kata nai vijiji wa Halmashautri ya wilaya ya Chunya

Mtendaji wa kata ya Matwiga Ndugu Gervas Cosmas Mahellah akichangia mada kwenye kikao cha tathimini ya mkataba wa  lishe cha Robo ya mwaka 2022/2023

Afisa Elimu awali na Msingi ndugu Ferd Yoha Mhanze akifafanua jambo wakati wa kikao cha Lishe Robo ya nne ya mwaka 2022/2023

Afisa tawala wilaya ya Chunya Ndugu Semwano Carlos Mlawa kwa Niaba ya Katibu tawala wilaya ya Chunya akimkabidhi Cheti cha Pongezi Mtendaji wa Kata ya Mkola Ndugu Steven Ndoni

Wajumbe wa kikao cha tathimini ya Mkataba wa lishe Robo ya nne ya mwaka 2022/2023 wakifuatilia mjadala unaendelea kuhusu kuboresha lishe


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.