• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

WASIMAMIZI WA UCHAGUZI WAONYWA MATUMIZI YA 'WHATSAPP'

Imewekwa: August 6th, 2025

Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Lupa lililopo wilaya ya Chunya Wakili Athuman M Bamba amewatahadharisha wasimamizi wasaidizi wa Uchaguzi ngazi ya kata kutumia mitandao ya kijamii (WhatsApp) kuepuka kuchanganya wakati wa kutuma taarifa stahiki kwa tume au penginepo kwa mujibu wa miongozo na maelekezo waliyopewa na watakayoendelea kupewa kabla, wakati na baada ya Uchagzu mkuu unakaofanyika mapema Mwezi Oktoba 2025

Akizungumza wakati akitoa hotuba ya kuahirisha Mafunzo leo 6.8.2025 yaliyodumu kwa siku tatu katika ukumbi wa Mikutano wa Mwanginde Hall ulipo Jengo jipya la Utawala Wakili Bamba amewataka wasimamizi wasaidizi ngazi ya kata kuhakikisha wanapunguza matumizi wa ‘WhatsApp’ katika kipindi hiki wakati wanatekeleza Majukumu ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi

“Hivi sasa kuna makundi Sogozi (WhatsApp), Jitahidini katika kipindi hiki muyapunguze ili msije mkakosea kutuma taarifa ambazo hamkutakiwa kutuma huko” Amesema Wakili Bamba

Aidha Wakili Bamba ameendelea kuwasisitiza kwamba Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi haikukosea kuwaamini kutekeleza majukumu ya tume katika maeneo yao ya uteuzi hivyo amewataka kuendelea kulinda Imani ya Tume kwao kwa kufanya kazi kwa haki na kwa weledi”

Mwenyekiti wa Mafunzo na Mshiriki wa Mafunzo hayo kwaniaba ya washiriki wengine Ndugu Obed Mwaikuka ametoa shukrani kwa Mkurugenzi mtendaji, pamoja na Tume huru ya Taifa kuwaamini kutekeleza Majukumu hayo muhimu, nyeti na yenye dhamana ya kupata viongozi watakao ongoza Taifa kipindi cha miaka mitano

Aidha Mwaikuka amemuhakikishia Msimamizi wa Uchaguzi Jimbo la Lupa kwamba vile walivyoaminiwa ndivyo watakavyotekeleza majukumu hayo kwa weledi na kwa kujituma huku akisema watafundisha na kutoa maelekezo hayo kwa wasimamizi wa vituo kama walivyoelekezwa wakati wa Mafunzo.

Mafunzo kwa wasimamizi wasaidizi ngazi ya kata katika Jimbo la Uchaguzi la Lupa yamedumu kwa siku tatu na yamehusisha washiriki arobaini (40) toka kata zote ishirini za Jimbo la Uchaguzi la Lupa. Mafunzo hayo ni miongoni mwa mambo mbalimbali yanayofanywa na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi ili kuhakikisha Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2025 unakuwa huru, wa Haki na usio na dosari yoyote

Washiriki wa Mafunzo wakiendelea na mjadala wakati wa Mafunzo kuelekea Uchagzu Mkuu utakaofanyika mwezi Oktoba 2025

Washiriki wakifanya Mazoezi ya kutengeneza eneo salama la kupigia kura wakati wa Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktaba 2025 wakati wa Mafunzo

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI TOKA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI July 03, 2025
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • WASIMAMIZI WA UCHAGUZI WAONYWA MATUMIZI YA 'WHATSAPP'

    August 06, 2025
  • MAFUNZO KWA WASIMAMIZI CHUNYA ISHARA YA UCHAGUZI MZURI

    August 04, 2025
  • RUNGWE WACHALAZWA CHUNYA

    July 19, 2025
  • DED CHUNYA APONGEZA WANANCHI UTEKELEZAJI MIRADI YA TASAF

    July 16, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.