• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

WANANCHI MAFYEKO WAIOMBA SERIKALI FEDHA KUKAMILISHA UJENZI WA SEKONDARI

Imewekwa: February 21st, 2023

Wananchi wa kata ya Mafyeko wilayani Chunya wameiomba serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania fedha kiasi cha shilingi milioni 53 ili kukamilisha ujenzi wa shule ya sekondari ya kata hiyo ili kutatua changamoto watoto kutembea umbali mrefu kwenda kupata huduma ya Elimu, kwani awali walipaswa kusafiri umbali wa kilometa 40 kuifikia sekondari ya Isangawana

Akitoa taarifa mbele ya Kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi wilaya ya Chunya Mwalimu Keneth Kaduma ambaye ni afisa Elimu kata ya Mafyeko na Katibu wa kamati ya Ujenzi wa Shule hiyo amesema mpaka sasa fedha shilingi milioni miamoja arobaini na moja, laki tano na elfu kumi na moja na mia sita (141,511,600) zimetumika ambapo halmashauri ya wilaya ya Chunya imechangia milioni 17, milioni 11 zilitolewa kwenye mfuko wa jimbo huku fedha nyingine ni michango ya wadau na wananchi wa kata ya Mafyeko

Mpaka sasa Madarasa mawili yamekamilika na yako tayari kwa matumizi huku zaidi ya dawati 70 yakiwa yamekamilika, madawati mengine 60 yako hatua za umaliziaji tayari kuletwa kwa matumizi, Madarasa mawili mengine yako hatua za jamvi. Ofisi ya walimu imekamilika sambamba na Ofisi ya Mkuu wa Shule zimekamilika

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi ambaye ndiye kiongozi wa ziara ya kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi Chunya Ndugu NOEL CHIWANGA amesema watawaagiza viongozi wa serikali wilayani Chunya kuaandaa andiko la kupeleka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili kuomba fedha za kukamilisha ujenzi wa shule hiyo

“Tunajua Rais na mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi Mhe, Dkt. Samia Suluhu Hassan hawezi kushindwa kutuletea fedha za kukamilisha ujenzi wa shule yetu hii, Hivyo sisi kama chama tutawaagiza viongozi wa halmashauri waandike andiko la kuomba fedha za kukamilisha ujenzi hapa ili watoto wetu waanze kusoma hapa”

Aidha mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Chunya amewapongeza wananchi wa kata ya Mafyeko kwa namna walivyojitoa kwaajili ya ujenzi wa shule hiyo huku akisema huo ndio uzalendo kwa nchi yao, Amemwagiza Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Chunya kuwasiliana na shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kuona uwezekano wa kuhamisha nguzo za umeme mkubwa ambazo zimepita karibu kabisa na majengo ya shule akisema ni hatari sana kwa wanafunzi pale itakapotokea changamoto au hitilafu.

Miradi iliyotembelewa leo na kamati hiyo ni pamoja na Mradi wa Kituo cha Afya Kambikatoto ambapo Jengo la wagonjwa wa Nje (OPD), Maaabara, jengo la upasuazi na wazazi, jengo la kufulia pamoja na Nyumba ya kuishi watumishi, Mradi wa Barabara kutoka Kambikatoto kwenda Sipa, Mradi wa Ujenzi wa Nyumba ya walimu(3 in 1) shule ya msingi Sipa yenye uwezo wa kubeba familia tatu za watumishi, Mradi wa ujenzi wa madarasa shule ya msingi Bitimanyanga, Mradi wa Kituo cha Afya Mafyeko, na Shule ya Sekondari Mafyeko

Katika Miradi iliyotembelewa na kamati ya siasa ya Chama pamoja na shukrani nyingi kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kutoa fedha za kujenga miradi mbalimbali pia kamati hiyo imeshauri wataalamu kuhakikisha changamoto ndogo ndogo kwenye miradi hiyo zinatatuliwa haraka ili kuletaufanisi katika miradi hiyo

Kamati ya siasa ya Chama cha Mapinduzi wilaya ya Chunya Chini ya mwenyekiti wake Ndugu Noel Chiwanga iko katika Ziara ya kawaida katika kukagua miradi mbalimbali inayotekelezwa katika wilaya hiyo kama ilani ya Uchaguzi ya Mwka 2020-2025 inavyoelekeza.

Jengo lenye Vyumba viwili vya Madarasa vilivyokamilika Shule ya Sekondari Mafyeko

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.