• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

WANAFUNZI KIDATO CHA KWANZA AMBAO BADO HAWAJA RIPOTI SHULENI KUSAKWA POPOTE WALIPO

Imewekwa: January 18th, 2023

Maafisa Elimu kata, watendajiwa kata na vijiji Halmashauri ya Wilaya ya Chunya wametakiwa kuwafuatilia na kujua walipo wanafunzi wote wa kidato cha kwanza hambao bado hawajaripoti shuleni hadi sasa.

Haya yame semwa na Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe. Mayeka S. Mayeka leo tarehe18, January 2023 kwenye ziara yake iliyolenga kukagua na kuona hali halisi ya kuripoti kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza ndani ya wilaya.

Katika ziara hiyo Mkuu wa wilaya amewaelekeza Maafisa elimu kata, watendaji wa kata na vijiji kuhakikisha watoto wote ambao bado hawajaripoti shuleni mpaka sasa wanatafutwa popote walipo na kuripoti katika shule walizo pangiwa.

Mayeka amesema hali ya watoto kuripoti shuleni sio ya kuridhisha sana kwani idadi kubwa ya wanafunzi bado hawajaripoti shuleni

Aidha Mhe.   Mayeka amesema hakubaliani kabisa na sababu zinazotolewa na wazazi za kutokufanya maandalizi ya sare na vifaa mbalimbali vya shule, hivyo kupelekea kuchelewa kwa watoto kuripoti shuleni kwani walipaswa kufanya maandalizi hayo mapema.

“Hii haikuwa ni dharura, kwamba shule zilikuwa zinajulikana zinafunguliwa lini hivyo mzazi alipaswa kufanya maandalizi mapema” alisemaMayeka

Hata hivyo Mhe Mayeka amesema hivi karibuni wataanza zoezi la kupita nyumba hadi nyumba kuwasaka watoto waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza na mpaka sasa bado hawajaripoti shuleni na kuwachukulia hatua wazazi wote ambao hawajawapeleka watoto shuleni.

 “Tayari tumeshaandaa migambo kwa ajili ya kuzunguka  nyumba hadi nyumba kukamata wazazi wote ambao hawajatekeleza wajibu wao wa kuwapeleka watoto Shuleni” amesema Mayeka.

Hatuwezi kukubali jambo hili tunaenda kuchukua hatu, hatuta muonea huruma mzazi yeyote, ilipasiwepo na usumbufu wa aina yeyote tunaomba watoto wote waliochaguliwa kuingia kidato cha kwanza wafike shule

Mkuu wa wilaya amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe, Dkt Samia Suluhu Hassan kwa Ujenzi wa vyumba vya madarasa, halmashauri ya wilaya ya chunya haina upungufu wa vyumba vya madarasa.

Kwaupanda wa Afisa Elimu Sekondari wa halmashauri ya wilaya ya chunya Ndugu Hamis Mapoto  amesema wilaya ya chunya wanafunzi walio chaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kwa mwaka 2023 ni wanafunzi 3885 na mpaka kufikia jana tarehe 17,  ni wanafunzi 1653 wamesha repoti sawa na asilimia 42.5/%.

Katika ziara hiyo Mkuu wa Wilaya akiwa ameambatana na kamati ya Ulinzi na Usalama na Wataalamu wa Halmashauri wamekagua Shule za sekondari Itewe, Isenyela, Kipoka, Makongolosi pamoja na shule ya sekondari Makalla.

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe, Mayeka S Mayeka wakwanza kushoto akiwa sambamba na Afisa Elimu Sekondari wa halmashauri ya wilaya ya chunya kwenye ziara ya kuona hali halisi ya kuripoti kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza ndani ya wilaya.

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka S. Mayeka akifuatilia taarifa ya kuripoti kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza katika moja ya shule alizo zitembelea

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.