• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

WAKUU WA IDARA SHIRIKIANENI NA DT KUJIBU HOJA

Imewekwa: June 15th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe Juma Zuberi Homera amewataka wakuu wa idara mbalimbali wilayani Chunya Kushirikiana na Mtunza hazina (DT) wa halmashauri kujadili taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali (CAG) ili kurahisisha kupata taarifa sahihi ambazo zinapelekea kufutika kwa hoja hizo

Akizungumza kwenye kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya lililoketi jana tarehe 14/6/2023 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya (Sapanjo) lenye lengo la kujibu hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa serikali zilizoibuliwa katika ukaguzi  kwa Mwaka wa fedha 2021/2022

“Hoja hizi za CAG wengi wanafikiri Mtunza hazina (DT)ndo anahusika kupambana na hojo hizi, Lazima wakuu wa idara wote tuhusike kuzijibu, Mkurugenzi unda timu maalumu ya kushugulikia hizi hoja. Ndo hoja za mkaguzi wa ndani lazima zishughulikiwe kwani ndizo zinageuka kuwa hoja za CAG hivyo zishughulikiwe mapema. Na wewe mkaguzi wandani hoja zako ukishazibua mwandikie mkurugenzi na nakala aipate mkuu wa wilaya ili naye ajue kwamba kuna hoja na hii ifanyike kwa mkoa mzima

Aidha Mhe Homera amewapongeza viongozi wote wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya kwakuendelea kusimamia vizuri ukusanyaji wa mapato na kupelekea halmashauri ya wilaya ya Chunya kuongoza katika Mkoa wa Mbeya kwa kukusanya zaidi ya asilimia 109 zaidi ya lengo lililokusudiwa awali

Niwapongeze kwa kukusanya mapato mengi, kwakweli mmetutoa kimasomaso kwani mlitakiwa kukusanya Bilioni 5.3 lakini sasa mmekusanya Bilioni 5.9 sawa na asilimia 109 hongereni sana. Na bila shaka timu yenu iko vizuri na muendelee kushirikiana hivyo ili muendelee kututoa kimasomaso 

Katibu tawala mkoa wa Mbeya Ndugu Rodrick Mpogolo amewapongeza viongozi wote wa halmashauri ya wilaya ya Chunya kwa namna wanavyosimamia miradi ya maendeleo jambo lililopelekea halmashauri ya wilaya ya Chunya Kupata Hati safi, huku akiwata kuendelea kujenga umoja na mshikamano kati ya baraza la madiwani na watumishi wengine wa halmashauri ili muendelee kupata hata safi kwa wakati mwingine

Niwapongeze viongozi wote na Manejimenti kwa kazi nzuri wanayoifanya ndo maana wakaweza kupata hati safi, lakini ni imani yangu kwamba Mwenyekiti wa Halmashauri mtaendelea kujenga ushirikianao kati ya baraza la madiwani na viongozi wengine wakiwepo watumishi ili wakati mwingine mpate hati safi nyingine

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka S. Mayeka amemuhakikishia mkuu wa Mkoa mambo yote aliyoshauri kwaajili ya maendeleo ya wilaya ya Chunya yatatekelezwa kama alivyoshauri, pia amewashukuru madiwani, wakuu wa idara na watumishi wengine kwa kazi kubwa wanayoifanya katika suala zima la makusanyo ya mapato

Tutajitahidi kutekeleza maagizo na ushauri wako kama ulivyotuagiza, lakinin pia nimwapongeze madiwani, wakuu wa idara na watumishi wote kwa kazi kubwa wanayofanya katika suala la ukusanyaji wa mapato, Natambua kazi kubwa ambayo watumishi wanafanya na naomba tuendelee kupamabana ili tuendelee kuwa vinara kataka suala la ukasnayaji wa mapato

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mhe. Bosco Mwanginde amesema Chunya tutaendelea kushirkiana vizuri ili kuhakikisha tunaendelea kutekeleza miradi yote ya maendeleo kwa ufasaha na baraza hili liko tayari kuendeleza ushirikiano huo ili tuendelee kuwa vinara katika makusanyo ya mapato na hata utekelezaji wa miradi mingine ya maendeleo inayotekelezwa katika halmashauri ya wilaya ya Chunya

“Mimi siwezi kuanza kurudia mambo ambayo viongozi wengine wameshayazungumza, sisi tuko tayari kutoa ushirikiano unaohitajika ili tuweze kufunga hoja zilizoibuliwa na Mdhibiti na mkaguzi wa Hesabu za serikali.

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • MAMA NA MWANAYE WAKABIDHI DAWATI 41 SHULE YA MSINGI MATWIGA, CHUNYA

    May 19, 2025
  • DC BATENGA, "HAKIKISHENI MNAMILIKI ARDHI"

    May 14, 2025
  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.