• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

WAKULIMA CHUNYA WANUFAIKA NA ELIMU YA MATUMIZI SAHIHI YA MBOLEA.

Imewekwa: October 4th, 2025

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo  anayesimamia Maendeleo ya Mazao na Usalama wa Chakula, Dkt. Stephen Nindi amefanya mkutano wahadhara na wakulima wa Wilaya ya Chunya Oktoba 4, 2025 kuhamasisha matumizi sahihi ya mbolea kwa wakulima kutokana na kilimo kuwa ni sayansi inayohitaji matumizi sahihi ya mbolea yenye vipimo sahihi kulingana na afya ya udongo.


Awali akiwa katika kikao na Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mhe. Mbaraka Batenga katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Dkt. Nindi amepongeza juhudi za viongozi wa Wilaya ya Chunya kwa kupata mashine za kupimia afya ya udongo ili kumrahisishia mkulima kutambua aina ya udongo na mbolea inayopaswa kutumika.

Aidha, Mkuu wa Wilaya ya Chunya SACI Mbaraka Batenga amesema, upimaji wa afya ya udongo ni muhimu kwakuwa unamwezesha mkulima kutumia mbolea kwa usahihi na kuongeza uzalishaji wa mazao.

“Msimu wa Kilimo ulioisha mwaka 2024/2025, zao la Tumbaku limefanya vizuri, mbolea iliyosambazwa na Kampuni ya Mbolea Tanzania - TFC imeongeza uzalishaji zaidi ya makadirio yaliyokuwepo ambapo Wilaya ya Chunya, Mkoani Mbeya imezalisha tani milion 27,091.7 na kuondoa malalamiko kwa wakulima,” ameeleza SACI Batenga.

Pamoja na mafanikio hayo ameeleza kuwa bado yapo maeneo ambayo hayana mwamko wa kutumia mbolea kama eneo la kata ya Kambi Katoto na Sipa hivyo endapo watapewa elimu ya matumizi ya mbolea watahamasika kutumia mbolea na kuongeza uzalishaji.

Dkt. Nindi amefanya Mikutano miwili ya hadhara, mmoja katika kata ya Lupa, tarafa ya Kipembawe na mkutano mwingine ameufanya Itumba, tarafa ya Kiwanja huku akipongeza juhudi za wakulima kuongoza kuzalisha mazao kutokana na matumizi sahihi ya mbolea.

Kuhusu usambazaji wa mbolea, Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya Mbolea Tanzania - TFC, Bw. Samuel Mshote ameeleza kuwa katika msimu wa Kilimo uliopita TFC ilisambaza tani 61,000 ya mbolea ya NPK 10:18:24 kwa wakulima wa zao la Tumbaku. Ameongeza kwa mwaka huu, TFC imepanga kusambaza takribani tani 71,000 za mbolea ya NPK 10:18:24 ambapo usambazaji wa mbolea ya NPK 10:1824 kwa Wilaya ya Chunya umefikia asilimia 85, tani 10,395 zimewafikia wakulima kati ya tani 12,230 zinazotarajiwa kusambazwa katika msimu huu.

Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mhe. Mbaraka Batenga akifafanua jambo kwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Dkt. Stephen Nindi na wajumbe wake 

wakati wa  kikao cha ndani leo Oktoba 4,2025 katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Chunya.


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Dk. Stephen Nindi akifuatilia kwa karibu kikao cha ndani na Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe. Mbaraka Batenga.


Matangazo

  • KUPIGA KURA YA RAIS KITUO AMBACHO HAUKUJIANDIKISHA September 15, 2025
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • VIJANA WAIHESHIMISHA CHUNYA KUPITIA MKOPO WA ASILIMIA 10

    October 07, 2025
  • WAKULIMA CHUNYA WANUFAIKA NA ELIMU YA MATUMIZI SAHIHI YA MBOLEA.

    October 04, 2025
  • UANDAAJI MPANGO WA BAJETI WAWANUFAISHA WATAALAMU CHUNYA DC.

    October 01, 2025
  • WATAALAMU CHUNYA DC WAONGEZEWA UWEZO UANDAAJI MPANGO WA BAJETI.

    September 30, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.