• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

WAJIBU WA BABA KUZINGATIA LISHE YA MAMA NA FAMILIA YAKE WAKATI WOTE

Imewekwa: June 19th, 2024

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mbarak Alhaji Batenga amewataka wakina baba wote wilayani Chunya kuhakikisha wanawasaidia wake zao na wakina mama wengine waliopo katika maeneo yao kupata lishe bora kabla ya kubeba ujauzito, wakati wa ujauzito na hata baada ya kujifungua kwani suala la lishe kwa mtoto huanzia Tumboni kwa mama yake

Akizungumza kwenye maadhimisho ya Afya na lishe kwa ngazi ya kijiji yaliyofanyika tarehe 18/6/2024 katika kijiji cha Ifumbo kilicho katika kata ya Ifumbo, ikiwa ni mwendelezo wa maadhimisho hayo ambapo wilaya ya Chunya hufanya kila robo ya mwaka lengo ikiwa ni kuhimiza Afya bora na Lishe bora kwa mtoto na jamii kwa jamii kwa ujumla Mhe Batenga amesema wakina baba (wanaume) watambue kuwa hilo nalo ni jukumu lao

“Tukaboreshe lishe, hivi vitu (Vyakula katika Makundi mbalimbali ya Lishe) havitoki Mbinguni na vingine tukapande wenyewe ili tuwapatie lishe bora familia zetu. Wakinababa tuwasaidie wakinama ili wapate lishe bora maana suala la lishe linaanza tumboni na kwakufanya hivyo tutakuwa tumetekeleza vyema suala la kujali familia zetu” alisema Mhe Batenga

Akitoa taarifa ya hali ya Lishe wilaya ya Chunya, Mganga Mkuu wa wilaya ya Chunya Dkt Darison Andrew amesema wanaume wengi hawawajibiki ipasavyo katika kuhakikisha mama wajawazito wanapata lishe bora na sababu ni kukosekana kwa Elimu, ni tamaa yao kuona wanaume wakiambatana na wenza wao wanapokuja kliniki ili waweze kupata Elimu hiyo muhimu

“Ni tamaa yetu kuona wanaume wengi wanapata elimu hii sababu mtoto aliyedumaa hana mchango mkubwa sana katika maendeleo ya Taifa na hata akisoma uelewa wake utakuwa mgumu sana, hivyo ni tamaa yetu mama mjamzito apate vyakula vyote kama vilivyowekwa kwenye meza ile na mtoto atakapotimiza miezi saba baada ya kuzaliwa akipata lishe bora itamjenga katika maisha yake yote”

Aidha, Dkt Darison Andrew ameongeza kuwa katika wajawazito 100, wajawazito 2 mpaka 9 wanakuwa na upungufu wa damu mwilini hivyo anakuwa na upungufu wa kinga mwili jambo ambalo linamuweka hatarini kupoteza maisha wakati wa kujifungua. Amewaomba wananchi wa Ifumbo na Chunya kwa ujumla kuwapatia lishe bora wajawazito na kwakufanya hivyo itasaidia kupata Taifa lenye watu wenye afya bora

Kwa niaba ya wananchi wa kata ya Ifumbo waliojitokeza kwenye maadhimisho hayo ya Afya na Lishe, Diwani wa kata ya Ifumbo Mhe. Weston Mpyila amesema suala la Lishe katika kata ya Ifumbo ni la lazima na wananchi wa Ifumbo wanazingatia hilo kwani mpaka sasa watoto wanapata Lishe wawapo nyumbani na hata wakiwa shuleni kwani vyakula vipo.

 “Tunafanya jitihada kuhakikisha watoto wetu wanazingatia suala la lishe, sisi suala la lishe ni lazima sio ombi tena na wananchi wameitikia hivyo chakula kinatolewa katika Taasisi zote za shule za binafsi na Serikali, lakini pia kwenye kilimo tunafanya vizuri kwani vyakula vyote ulivyoona hapa mbele tunalima wenyewe hivyo sisi lishe sio tatizo”

Muhudumu wa Afya ngazi ya kata bwana Charles Jailos Ngazi amesema Elimu hii ya lishe huwa inatolewa mara kwa mara kwenye zahanati na vituo vyao vya afya huku akisema elimu hiyo imepokelewa vizuri na wananchi kwani mwitio wao ni mkubwa huku akirejerea idadi kubwa ya wananchi waliojitokeza katika siku ya Afya na lishe.

Siku ya Afya na Lishe huadhimishwa na kila kijiji kwa kila Robo ya mwaka huku uongozi wa Halmashauri kwa maongozi wa maafisa lishe wa wilaya ya Chunya huchagua kuhudhuria katika maadhimisho ya kijiji kimojawapo ili kuongeza chachu ya kuthamini lishe pamoja pamoja na kutoa elimu Zaidi kuhusu lishe, kwa Robo hii ya nne uongozi ulitembelea siku ya afya na lishe katika kijiji cha Ifumbo ndani ya kata ya Ifumbo.

Baadhi ya vyakula vilivyletwa kwenye darasa la lishe wakati wa maadhimisho ya siku ya Afya na Lishe ngazi ya kijiji ambapo Mkuu wa wilaya ya Chunya alikwa Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mbarak Alhaji Batenga akifafanua faida za ubuyu kwenye Afya ya Binadamu wakati akizungumza na wananchi kwenye Maadhimisho ya siku ya Afya na Lishe ilifanyika kwenye  kijiji cha Ifumbo

Mganga Mkuu wa wilaya ya Chunya Dkt Darison Andrew akifafanua jambo wakati wa maadhimisho ya siku ya Afya na Lishe yaliyofanyika kijiji cha Ifumbo kilichopo kata ya Ifumbo

Diwani wa kata ya Ifumbo Mhe. Weston Mpyila akitoa salamu za wananchi wa kata ya Ifumbo kwa Mkuu wa wilaya ya Chunya wakati wa maadhimisho ya siku ya Afya na Lishe yaliyofanyika ndani ya kata anayoiongoza ambayo ni kata ya Ifumbo

Wananchi wa Ifumbo wakiendelea kuburudika wakati wa maadhimisho ya siku ya Afya na Lishe iliyofanyika kata ya Ifumbo katika kijiji cha Ifumbo

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.