• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

WAFANYAKAZI WENU WAORODHESHWE NA KUPEWA VITAMBULISHO.

Imewekwa: June 14th, 2023

Mkuu wa wilaya ya chunya Mhe. Mayeka S. Mayeka amewataka wamiliki wa Leseni za uchimbaji wanaoendesha shughuli zao katika hifadhi ya Msitu wa mbiwe wilayani chunya kuorodhesha wafanyakazi wote wanaofanya kazi katika machimbo yao, ili kwa ambao hawapo  sehemu yoyote kuondoka kwenye msitu huo.

Mhe. Mayeka ametoa agizo hilo jana June 13, 2023 akiwa kwenye mkutano wa hadhara na wachimbaji wadogo  wanaofanya kazi katika machimbo hayo  ambako alienda na kamati ya ulinzi na Usalama ya wilaya na maafisa mbalimbali wa Taasisi za Umma kwa ajili ya kuona uvamizi na uharibifu mkubwa unaoendelea katika hifadhi ya msitu wa mbiwe.

“Hawa wamiliki watawaandika watu wanaofanya kazi kwenye machimbo yao na watu wasiokuwa na machimbo tutawaomba waondoke kwenye msitu huu waende sehemu nyingine wakafanye shughuli zao” alisema Mhe. Mayeka

Mhe. Mayeka amewataka wamiliki wa leseni za uchimbaji katika msitu huo kuhakikisha wafanyakazi wao wanakuwa na vitambulisho vitakavyo wawezesha kuingia katika msitu wa mbiwe na kuendelea na shughuli za uchimbaji

“Kuanzia leo watu wenu wawe na vitambulisho na hivyo vitambulisho kopi moja unabakia nayo wewe na nyingine TFS, ili tukiingia humu asiyekuwa na kitambulisho ndio tunaye mtaka” aliongeza kusema Mhe. Mayeka

Alisema Najua kuna watu hawapo kwenye zamu (shift) ya mtu yeyote hapa wanazunguka usiku na mchana  na ndio wanavamia leseni za watu wanaanza kuchimba na wakikutwa wanakimbia na ndio wanaotuharibia Msitu.

Diwani mwenyeji wa kata ya matundasi Mhe. Kimo Choga amesema wanatambua kuwa wapo kwenye eneo la hifadhi ya msitu ila kilicho wapeleka huko ni kutafuta ridhiki ya maisha yao.

“Nahapa tulipo kuna watu ambao wanafanya biashara ndogondogo kama mamantilie na vilevile kuna watu mbao wanafanya kazi za uchimbaji kwenye leseni zilizopo hapa ambazo nazitambua kama leseni mbili” alisema mhe. Kimo

Mhe. Kimo aliongeza kuwa "Mheshimiwa mkuu wa wilaya tunafahamu kabisa tupo hapa hatupo kisheria hivyo naomba nikiri kabisa mimi na wananchi wangu, lakini matumaini yetu sisi ni kupokea maelekezo ya namna ya kuishi kisheria kwenye eneo hili la hifadhi ya msitu".

“Kwa niaba ya wananchi mimi na kuahidi kwamba kama kunanamna yeyote yakupata maelekezo ya kuishi kisheria kwenye eneo hili sio kwa kujenga makazi ya kudumu nikufanya biashara ya muda mfupi na ndio maana makazi yetu sio ya kudumu” amesem Mhe. Kimo

Wachimbaji wadogo wanaofanya shughuli za uchimbaji kwenye Msitu wa Mbiwe wakimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe. Mayeka S Mayeka kwenye mkutano wa Hadhara

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.