• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

UWINDAJI WA KITALII WAPEWA MSUKUMO MPYA CHUNYA.

Imewekwa: June 27th, 2018



Leo tarehe 26/6/2018 kimefanyika kikao cha uwindishaji wa kitalii cha kila mwaka kilichofunguliwa rasmi na Mkuu wa wilaya ya chunya

 Mh. Rehema Madusa ambaye alikuwa ni mwenyekiti wa kikao hicho kilichofanyika katika ukumbi wa Sapanjo, Makao makuu ya Halmashauri ya Chunya.

 Katika salamu zake kwa wadau, wataalam, na watu wote waliohudhuria Mh. Mkuu wa wilaya alianza kwa kumshukuru Mungu
 kwa kuwawezesha watu wote waliohudhuria kufika salama ili kuweza kujadili kwa pamoja masuala yote yanayohusu uwindishaji na uhifadhi.

 aligusia umuhimu wa uhifadhi kwa kusema na ninanukuu “huwezi kufanya uwindishaji au uwindaji kama hakuna uhifadhi, na pia bila

kusimamia utunzaji mazingira ipasavyo huwezi kufanya uwindishaji na kuwa na wanyama wa kutosha ambao watasaidia

kufanikisha uwindaji endelevu, pamoja na maendelo kwa wananchi wanaozunguka hifadhi na serikali kwa ujumla”.  Mh. Mkuu wa

wilaya aliwashukuru wadau walioshiriki katika Operesheni za kuwaondoa wavamizi katika maeneo ya hifadhi kwani lengo

lilikuwa ni zuri ikiwemo kurejesha uoto wa asili, kusimamia sheria ili kuweza kuwadhibiti wale wote wanaokwenda kinyume cha

sheria na taratibu za nchi. Alisistiza wananchi wanaoishi maeneo yanayozunguka hifadhi wanahitaji Elimu, kusimamiwa na

wanahitaji viongozi wenye dhamira na nia ya dhati katika kusimamia sheria na taratibu za nchi kuhakikisha kwamba maeneo

yaliyohifadhiwa yanasimamiwa kisheria na wanaofanya uhalifu wanachukuliwa hatua za kisheria. Aliendelea kusistiza kuwa

kunauharibifu mkubwa sana wa mazingira kama vile vyanzo vya maji, akitolea mfano eneo la Mafyeko kuna sehemu/eneo

muhimu sana la chanzo cha mto lupa; pia maeneo ya Bitimanyanga kata ya mafyeko na kambikatoto kunafanyika ujangilli wa

hali ya juu kabisa na majangili hao wanajifanya wakulima na wafugaji kwani wakati ilipofanyika operesheni zilikamatwa

silaha za moto. Kwahiyo watu hao ni wahalifu na kwa pamoja ziunganishwe nguvu ili kuweza kuwadhibiti.  

Naye Afisa Wanyamapori wilaya ya Chunya alipata fursa ya kuwasilisha taarifa ya idara ya maliasili ambapo pamoja na mambo
mengine alieleza vitalu vinavyopatikana katika wilaya ya chunya ni Rungwa South open area, Rungwa Mzombe Open area, Piti
west(Open area) GR, piti East Open area, Chunya Lukwat(open area) GR, sehemu ya eneo la kitalu cha Rungwa Inyonga GR, na
vitalu vinavyopatikana katika wilaya ya Songwe ni pamoja na Chunya Msami (open area) GR, Lukwati north GR, Lukwat South
GR, na Chunya East open Area; hii ni kifuatia mgawanyo wa wilaya ya Chunya ambapo wilaya mpya ya Songwe ilizaliwa. pia
aligusia juu ya mgawanyo wa fedha za asilimia 25 za uwindishaji wa kitalii unaotoka serikali kuu. fedha hizo ni mapato ya
uwindishaji yatokanayo na malipo ya wanyapori waliowindwa kisheria katika maeneo ya vitalu husika, aliongeza kuwa mgeni
hulipia fedha wizarani na baada ya malipo hayo kanuni za uwindishaji kitalii zinaitaka wizara kurudisha asilimia 25 kwenye
maeneo ya vijiji ama wilaya walipowindwa wanyama hao na katika fedha hizo asilimia 60 hupewa vijiji vinavyozunguka maeneo ya vitalu
husika na asilimia 40 hubaki kwenye mapato ya Halmashauri husika kwa ajili ya shughuli za uhifadhi wanyamapori na
mazingira yake. kuhusu michango ya makampuni kwa ajili ya shughuli za maendeleo ya vijiji alitanabiasha kuwa sheria ya wanyamapori
 na.5 ya mwaka 2009 inatambua uhifadhi wa wanyamapori kwa njia ya matumizi endelevu hivyo inaainisha kila kampuni yenye kupewa kitalu
 kwenye eneo husika inatakiwa kuchangia Dola 5000 za kimarekani kwa ajili ya shughuli za amendeleo kwenye vijiji na fedha hizo zinagawanywa
 kulingana na idadi ya vijiji vinavyozunguka hifadhi husika, hivyo ni takwa la kisheria na siyo hiari kuchangia fedha hizo kila mwaka ama
 msimu wa uwindaji unapoanza. misaada mingine nje ya hapo hutolewa na makampuni husika kwa hiari ili kuboresha mahusianao.
 Makampuni hayo ni pamoja na Robin Hurt Safaris, Mwatisi Hunting Safari, Old Nyika Safari and Royal Holdings Safaris na Northen Safari enterprises. ambapo vijiji vilivyopata
mgao huo ni pamoja na Kambikatoto, Bitimanyanga, Mafyeko, Lualaje na Mtanila.

  katika kikao hicho kilichohudhuriwa na wawakilishi wa makampuni ya uwindaji kitalii, wataalam wa misitu na wanyamapori pamoja na wadau mbalimbali;
  Watendaji wa vijiji vinavyopitiwa na hifadhi walipata fursa ya kutoa mchanganuo wa Mapato na matumizi ya fedha kulingana na mgao wa makampuni ya uwindaji  katika vijiji vyao.

                                                                                                          
  Kaimu Mkurugenzi Bw.Weston Njeje aliyesimama, Mkuu wa wiaya ya Chunya Bi.Rehema Madusa(kulia kwake), Kaimu Afisa Maliasili Bw.Lucas Theodory (kushoto), na Afisa Maliasili Mkoa (kulia) 

                                                                          

                                                                           Wawakilishi wa Makampuni ya Uwindishaji kitalii

                                                                                                      
     Afisa Wanyamapori Chunya Ndg.Jacob Mpinga (aliyesimama) akichangia mada, kulia kwake ni mwakilishi wa WCS na kushoto kwake ni Bi Simphorose Kavishe
 

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.