• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

Uwindaji, uchimbaji madini chanzo uharibifu wa mazingira Chunya

Imewekwa: June 5th, 2022


 Shughuli za kibinadamu zikiwemo uchimbaji madini na kilimo ni chanzo cha uharibifu wa mazingira Wilayani Chunya.

 Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wikaya ya Chunya, Mayeka S. Mayeka alipomuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mbeya katika maadhimisho ya siku ya mazingira duniani inayofanyika Juni 5 ya kila mwaka.

 “Kwa upande wetu Chunya tuna shughuli kuu mbili za kiuchumi, uchimbaji wa madini na kilimo cha tumbaku, shughuli hizi mbili ndizo zinazoongoza kwa ukataji miti kwa kiasi kikubwa,” alisema Mayeka.

 Aidha, Mayeka ameainisha vitendo vya uchomaji moto mashamba na misitu kuchangia kwa kiasi kikubwa uchafuzi na uharibifu wa mazingira Mkoani Mbeya.

 “Katika mkoa wetu tuna changamoto ya moto, hiki ni kikwazo kikubwa katika jitidaha zetu za kuhifadhi mazingira hasa kwenye vyanzo vya maji na misitu, shughuli za uwindaji hasa Wilaya za Chunya, Mbalali na Mbeya vijijini, aidha shughuli ya uchimbaji wa madini ni kinara kwa uchomaji wa moto pindi wanapotafuta maeneo yenye dhahabu.” Alisema Mayeka.

 Kadhalika Mayeka amesema hali ya mazingira kidunia na kitaifa si nzuri sana ambapo bado kazi kubwa inahitajika kufanyika katika harakati za utunzaji wa mazingira, ikiwemo Mkoa wa Mbeya kuhakikisha mazingira yanakuwa endelevu ili vizazi vingine vikute mazingira yaliyo salama.

 Kwa upande wake, Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji Mkoa wa Mbeya Ndg. Said Madito ametoa wito kwa wananchi na wakazi wa Mkoa wa Mbeya kuhakikisha wanatunza mazingira kwa ajili ya wao na vizazi vijavyo.

 “Sisi kama mkoa tutahakikisha tunashirikiana na wadau wote kwa ajili ya kuyatunza mazingira ili kusudi zoezi la kilimo, uchimbaji wa madini, ufugaji ziendane na uhifahi wa mazingira.” Alisema Madito.

 Madito aliongeza kwa kusema kuwa, kaulimbiu ya mwaka huu inakumbusha mambo matatu yakiwemo kupanda kwa joto duniani, wajibu wa kutunza viumbe hai na jambo la tatu ni suala la uchafuzi wa mazingira.

 “Sisi kama Mkoa ni sehemu ya jamii ambayo inatakiwa istaarabike kwa kuyatunza mazingira, hivyo tuepuke uchafuzi wa mazingira,” amesema Madito.

 Kaulimbiu ya kitaifa ya siku ya uhifadhi wa mazingira duniani ilisema, “Tanzania ni moja tu, tunza mazingira” 

 MATUKIO KATIKA PICHA

 Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe. Mayeka S. Mayeka akipanda Mti katika eneo la Shule ya Msingi Makongolosi ikiwa ni katika Maadhimisho ya siku ya Mazingira Duniani.

 Wanakikundi cha TOFAA wakionyesha bango lenye ujembe usemao " Miti ni sehemu ya maisha yetu kila mmoja anawajibu wa kuitunza" kwenye kilele cha Maadhimisho ya siku ya mazingira

 Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Chunya Mhe. Noel Chiwanga akipanda mti eneo la shule ya Msingi Makongolosi ikiwa ni kilele cha maadhimisho ya siku ya Mazingira Dunini

 

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.