• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

USHIRIKIANO NDIYO MSINGI WA MAFANIKIO YA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024 CHUNYA

Imewekwa: September 26th, 2024

Msimamizi wa Uchaguzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ndugu Tamim Kambona amesema katika Uchaguzi huu hakuna mgombea atakayepita bila kupingwa bali kila mgombea atapaswa kupigiwa kura kwa mujibu wa Sheria, kanuni na miongozo, hivyo amewataka viongozi wa vyama vya siasa kuwa wavumilivu na kutoa ushirikiano pindi watakapotakiwa kufanya hivyo ili kuhakikisha zoezi la Uchaguzi linaisha kwa Amani

Akizungumza kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya leo tarehe 26/09/2024 Msimamizi wa Uchaguzi amesema wapiga kura, wagombea na wadau mbalimbali wa Uchaguzi wanapaswa kupata maelekezo kuhusu utaratibu wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakavyofanyika kuanzia hatua ya kujiandikisha mpaka hatua ya kupiga kura.

“Maelekezo yote muhimu yatawekwa ili wagombea na wapiga kura wayajue na kufuata ili kuhakikisha uchaguzi unafanyika kwa haki na uwazi na kwa kuzingatia sheria zilizowekwa za uchaguzi wa serikali za mitaa,” amesema Kambona.

Aidha Kambona ametoa wito kwa wagombea wanaotaka kugombea nafasi mbalimbali katika Uchaguzi wa Serikali za mitaa utakaofanyikaNovemba 27, 2024 ambazo ni  wenyeviti wa vijiji, vitongoji na wajumbe Halmashauri ya vijiji kuchukua fomu katika Ofisi za msimamizi msaidizi wa Uchaguzi huku akiwataka wakazi wote wenye umri kuanzia miaka 18 au zaidi kushiriki kwenye uchaguzi huo wa serikali za mitaa.

Akitoa salamu za Serikali Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mhe Mbaraka Alhaji Batenga amesema katika uchaguzi wa Serikali za mitaa Wilaya ya Chunya inapaswa kuwa mfano wa kuigwa kwa kufanya siasa safi na kudumisha Amani wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi, lakini pia amewataka wanasiasa kuziishi na kuzitekeleza kwa vitendo sera ya 4R za Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na kuwaelimisha wafuasi wao ili kuendelea kudumisha Amani

 “Sera ya 4R aliyokuja nayo Mhe Rais Samia ilikuwa ni kutibu matatizo ya kisiasa yaliyotokea kwenye uchaguzi uliopita, sera hii kwetu ni lazima kuitekeleza sio chaguo”amesema Mhe Batenga.

Viongozi wa dini akiwemo Sheikh wa Wilaya, Mwenyekiti wa Wachungaji Kanisa la Moravian Wilaya na mwakilishi wa wazee wa mila wameahidi kutoa ushirikiano kwa msimamizi wa Uchaguzi na Serikali kwa ujumla kuhimiza waumini wao kushiriki kwenye uchaguzi wa Serikali za mitaa kuanzia hatua ya kujiandikisha mpaka kupiga kura.

Mkutano huu wa maelekezo kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa wa mwaka 2024 umefanyika leo tarehe 26 Septemba, 2024 na umehudhuliwa na Viongozi wa Vyama vya siasa, viongozi wa dini, wawakilishi kutoka makundi mbalimbali kama vile wasafirishaji, vijana, wasanii, walemavu na makundi mengine mengi.

Msimamizi wa Uchaguzi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Tamim Kambona akitoa maelezo kuhusu Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika tarehe Novemba 27, 2024 mapema leo kwenye kikao kilichoketi kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

Mwenyekiti wa Makanisa ya Moraviani wilaya ya Chunya Mchungaji Kayange akitoa nasaha zake kwa niaba ya Wachungaji baada ya Msimamizi wa Uchaguzi wa wilaya ya Chunya kuhitimisha kutoa maelezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Sheikh  mkuu wa wilaya ya Chunya akitoa neno wakati wa Mkutano wa kutoa maelezo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotaraji kufanyika Novemba 27, 2024, mapema leo kwenye ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

Wananchi na wadau wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa waliojitokeza kwenye kikao cha Maelezo ya Uchaguzi kilichoketi mapema leo kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.