• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

USAFI UIMARISHWE KUEPUKA MAGONJWA YA MLIPUKO

Imewekwa: September 20th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mhe. Mbaraka Alhaji Batenga amemtaka Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kusimamia zoezi la usafi wa mazingira kwa wananchi wa wilaya hiyo ili kuepuka magonjwa ya mlipuko yanayoweza kujitokeza ikiwemo kipundupindu.

Mhe. Batenga ametoa agizo hilo, Septemba 20, 2024 kwenye maadhimisho ya siku ya usafishaji duniani wakati akihutubia mkutano wa wananchi soko la Uhindini Kata ya Chokaa Wilayani Chunya ambapo amesisitiza matumizi bora ya choo, kunawa maji tiririka na sabuni kunapunguza athari za kupata ugonjwa wa kipindupindu kwa asilimia 40 huku akimtaka Afisa Afya wa Wilaya kuhakikisha wanawatoza faini wote wanaokiuka.

“Mkurugenzi hakikisha kila mtu anafanya usafi  kwenye eneo lake utaniambia wangapi hawajafanya usafi, faini itasaidia kurebisha tabia za uchafu” amesema Mhe. Batenga.

Aidha, Mhe. Mkuu wa Wilaya ya Chunya amewakumbusha wananchi wa Wilaya hiyo, hivi karibuni wilaya hii ilikumbwa na mlipuko wa kipindupindu Chunya iripoti wagonjwa ishirini na tano (25) ambapo sababu kubwa ni uchafu wa mazingira.

“Kulikuwa na kipindupindu Wilaya ya Chunya, hii imetokana uchafuzi wa mazingira, kutozingatia kanuni bora za mlo na matumizi mabaya ya Choo, kila mwananchi afanye usafi kwenye eneo lake pamoja na kufyeka maeneo yanayozunguka nyumba zenu” amesema Mhe. Batenga.

Wafanyabiashara wa Soko la Uhindini wilayani Chunya walimueleza Mhe. Batenga changamoto zilizopo kwenye eneo hilo ikiwemo ukosefu wa maji safi, ubovu wa miundombinu na ukosefu wa dampo kwaajili ya kutupa taka ambapo Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, wakili Athumani Bamba amewahikishia wafanyabiashara hao kuwa kupitia mapato ya ndani ya Halmashauri kero zote walizozieleza zitafanyiwa kazi.

Wilaya ya Chunya imeadhimisha siku ya usafishaji duniani kwa kufanya usafi maeneo ya soko la Uhindini pamoja na kutoa elimu kwa wananchi wa maeneo hayo kuhusu umuhimu wa kutunza mazingira ili kuepuka magonjwa ya mlipuko, kauli mbiu ya usafishaji duniani mwaka  2024 ni “Uhai hauna mbadala, zingatia usafi”.

Kaimu Afisa Mazingira Ndugu Baraka Kipesha akisoma Taarifa ya Mazingira Mbele ya Mkuu wa wilaya ya Chunya mapema leo wakati wa Maadhimisho ya siku ya Usafishaji Duniani ambapo kiwilaya yamefanyika kwa kufanya usafi soko la Uhindini na baadaye Mkuu wa wilaya kuzungumza na wananchi waliojitokeza

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Batenga akizungumza na wananchi waliojitokeza kuadhimisha siku ya usafishaji Duniani ambapo kwa wilaya ya Chunya maadhimisho hayo yamefanyika Soko la Uhindini lililopo Kata ya Chokaa

Mkuu wa wilaya ya Chunya akitoa maelekezo kwa viongozi wa Serikali wa kata ya Chokaa, viongozi wa Halmashauri pamoja na viongozi wa Soko kuzingatia usafi wakati wa maadhimisho ya siku ya usafishaji

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.