• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

UKUSANYAJI MAPATO WILAYANI CHUNYA NI AGENDA YA KUDUMU

Imewekwa: March 3rd, 2023

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mhe. Bosco Mwanginde amewataka madiwani wa Halmashauri hiyo kuhakikisha wanasimamia ukusanyaji wa mapato kwenye maeneo yao kwani ajenda ya ukusanyaji wa mapato wilayani Chunya ni agenda ya Kudumu

Mhe. Mwanginde ametoa kauli hiyo mapema leo wakati wa kikao cha kawaida cha baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Chunya kilichoketi leo tarehe 3/3/2023 katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Chunya (Sapanjo) ambapo taarifa mbalimbali kutoka kamati mbalimbali zimejadiliwa

“Twende tukasimamie miradi lakini twende tukasimamie, mapato ukusanyaji wa mapato ni ajenda ya kudumu ya baraza lolote lile hasa likiwemo baraza la halmashauri ya wilaya ya Chunya” amesema Mhe. Mwanginde

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka Simon Mayeka alikuwa sehemu ya kikao hicho amesema wilaya ya Chunya kwa mujibu wa Ongezeko la watu kwa asilimia mia moja na ishirini (120) kwa sense ya watu na makazi ya Mwaka 2022 ukilinganisha na idadi ya watu kwa mujibu wa sense ya mwaka 2012

“Chunya sasa ina jumla ya watu laki tatu arobaini na nne elfu, mia nne sabini na moja 344,471   ambayo ni ongezeko la karibu asilimia mia moja na ishirini (120) kutoka Laki moja hamsini na sita elfu na mia saba themanini na sita (156,786) kwa sense ya mwaka 2012, Katika idadi hiyo wanaume ni 176,457 sawa na asilimia 51 huku wanawake wakiwa ni 168014 sawa na 49%”

Mhe. Mayeka ameishukuru serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kusimamia na kufanikisha zoezi la sense ambapo Chunya sasa kupitia matokeo ya sensa tunaweza kujua namna sahihi ya kupanga mipango ya kiuchumi na maendeleo kwa ujumla

“Mweshimiwa Mwenyekiti naomba kuzishukuru serikali zote mbili kwa kusimamia kwa mafanikio makubwa na hatimaye sasa tunayo matokeo ya sense kwa ngazi za wilaya, kata na nimeambiwa kwamba tutapata pia sense ya watu na makazi kwa ngazi ya vijiji kadiri uchakataji unavyoendela”

Aidha Mkuu wa wilaya ya Chunya amekemea vikali mawakala wa fedha kuchaji fedha ya ziada kwa wananchi wanaohitaji huduma hiyo amesema ni kinyume na Sheria hivyo amemuagiza Mkuu wa polisi wilayani Humo kuanza kuwakamata wale wote watakaobainika kufanya hivyo.

“OCD kuanzia leo polisi kata popote walipo waanze kuwakamata mawakala wote wanaowatoza fedha wananchi wanapohitaji huduma ya kutuma fedha jambo ambalo ni kinyume na utaratibu hivyo kuanzia leo polisi kata wapewe maelekezo ya kutekeleza agizo hilo”

Mkuu wa wilaya ya Chyuna ametoa agizo hilo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa madiwani kwamba kuna mawakala wa fedha wanamtaka mwananchi kutoa shilingi miatano ili awekewe shilingi Elfu kumi (10,000/=) hivyo kumfanya mwananchi atoe elfu kumi na mia tano wakati pesa atakayowekewa kwenye simu yake ni shilingi elfu kumi (10,000/=)

Naye Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Chunya Ndugu Noel Chiwanga amewapongeza waheshimiwa Madiwani namna wanavyotekeleza majuku yao hasa usimamizi wa fedha za miradi mbalimbali zinazotolewa na serikali ya Jamhuri ya Munngano wa Tanzania inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan

Pia amepongeza serikali kwa ujumla, kamati ya ulinzi na usalama na Baraza la Madiwani namna walivyosimamia suala la wanafunzi kuripoti shule kwani serikali imejenga madarasa ya kutosha hivyo lazima wanafunzi wakasome, hivyo mmefanya kazi kubwa na nzuri kuhakikisha watoto wetu wanenda shule

“Mkurugenzi wetu unafanya kazi nzuri kwenye usimamizi wa miradi, tumepita huko nje na tumeona, Hongera sana Mkurugenzi, Lakini kuna baadhi ya wakuu wako wa idara hawakutendei haki na tumejipanga siku moja tutakuja tuongee na wakuu wa idara pamoja na watumishi wengine ili kujenga umoja sahihi maana sisi Chama na Serikali ni kitu kimoja”

Kikao hiki cha Baraza la Madiwani ni kikao cha Kawaida cha Baraza hilo, ikiwa ni kikao cha Robo ya pili ya mwaka wa fedha 2022/2023 na kupitia vikao kama hivyo wilaya ya Chunya imeendelea kufanya vizuri katika maeneo mbalimbali Mkoani Mbeya ambapo Mpaka sasa inaongoza kwa ukusanyaji wa Mapato katika Mkoa, imeongoza katika suala la Lishe na maeneo mengine mengi

Waheshimiwa madiwani, wataalamu wa Halmashauri pamoja na wageni waalikwa wakiwa katika kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya wilaya ya chunya

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi wilaya ya Chunya Ndugu Noel Chiwanga akitoa salamu za Chama cha CCM katika kikao cha Baraza la Madiwani

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.