• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

UCHAGUZI HUU USITUGAWE: UTUUNGANISHE ILI TUPATE VIONGOZI WA KUMSAIDIA RAIS SAMIA

Imewekwa: October 5th, 2024

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mbaraka Alhaji Batenga amewataka wananchi wa wilaya ya Chunya kukataa wagombea wote watakaokuwa na lengo la kuwagawa na kueneza chuki kwa wananchi wa wilaya ya Chunya bali kupitia uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Novemba 27, 2024 wananchi wa Chunya waungane ili waweze kuchagua viongozi wazuri watakaomsaidia Rais wa Jamhuri ya Muungano kuwaletea maendeleo wananchi wa Tanzania wakiwepo wananchi wa wilaya ya Chunya

Akizungmza mapema leo tarehe 5/10/2024 katika mikutano tofauti tofauti aliyoifanya Kitongoji cha Ilindi kata ya Matwiga, Kitongoji cha Tulieni na Kitongoji cha Mafyeko vilivyopo kata ya Mafyeko ili kuhamasisha wananchi kujitokeza kushiriki kujiandikisha na hatimaye kushiriki uchaguzi wa Serikali za mitaa mapema mwezi Novemba, amesema uchaguzi unaotaraji kufanyika uwaunganishe wananchi ili kwa pamoja wachague viongozi wazuri wataowaletea maendeleo huku akionya watu wanaokusudia kuleta mgawanyiko

“Msiwapokee wagombea wanaokuja kwa lengo la kuleta mgawanyiko, Maana yake hawana makusudi mema kwenu. Na ni matumaini yangu Uchaguzi wetu sisi Chunya utakuwa wa Mfano watu watakuja Chunya kujifunza namna ambavyo wananchi wameshiriki uchaguzi kwa Amani kabisa” Amesema Mhe. Batenga

Aidha Mhe Batenga amewakumbusha wananchi wa Chunya umuhimu wa Amani katika wilaya ya Chunya huku akiwakumbusha wananchi kwamba wanafanya shughuli zao kwa Amani, wanaweza kusafiriki kutoka eneo moja kwenda eneo lingine bila usumbufu wowote kwasababu wananchi pamoja na viongozi wao wanashirikiana kuhakikisha amani hiyo inalindwa hivyo amewataka wananchi waendelee kuwa watulivu ili nchi ya Tanzania iendelee kuwa na Amani

Pamoja na Elimu hiyo kuelekea Uchaguzi Mhe. Batenga ameendelea kusikiliza kero mbalimbali na kuzipatia ufumbuzi huku akiwaambia wananchi kwamba Serikali ya awamu ya sita ni ya ukweli na uwazi jambo linalofanya wakati wote ajibu hoja za  wananchi wake kwa ukweli na uwazi

Wananchi wa Ilindi, Tulieni na Mafyeko wameshukuru ziara ya Mkuu wa wilaya kufika katika maeneo yao huku wakikili wazi kwamba ni ziara ya kwanza kwa kiongozi mkubwa katika wilaya ya Chunya kufanya ziara katika baadhi ya vitongoji mbalimbali vya wilaya ya Chunya ikiwa ni pamoja na Tulieni na ilindi

Mkuu wa wilaya ya Chunya ameanza Ziara ya Siku tatu yenye lengo la kuhimiza wananchi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya kuhakikisha wanajitokeza kushirki uchaguzi kwa kuanza na kujiandikisha, kugombea na hatimaye kushiriki kupiga kura tarehe kwenye uchaguzi unaotaraji kufanyika Novemba 27, 2024 ambapo wananchi wanapaswa kujiandikisha katika vitongoji wanavyoishi na vituo hivyo ndipo wananchi watakapoenda kupiga kura


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.