• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

TUENDELEE KUSHIRIKIANA KUIJENGA CHUNYA YETU

Imewekwa: November 20th, 2024

Msimamizi wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2024 Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Tamim Kambona amewataka viongozi wa Vyama vya Siasa vinavyoshiriki Uchaguzi wilaya ya Chunya kuhakikisha wanazingatia ratiba ya Kampeni huku akiwataka kuwasilisha maboresho ya ratiba hiyo saa yoyote inapohitajika ili kikao cha maridhiano kuhusu maboresho hayo kifanyike na kampeni kuendelea kama ilivyopangwa

Akizungumza mapema tarehe 19/11/2024 kwenye kikao kilichohusisha viongozi wa vyama vya siasa vyote vinavyotaraji kushiriki Uchaguzi pamoja na viongozi wa vyomba vya Usalama, Kambona amewashukuru viongozi wa Vyama vya siasa kwa ushirikiano wanao utoa kwake katika kuhakikisha Halmashauri ya wilaya ya Chunya inafanya Uchaguzi huru, shirikishi na wenye kufua Sheria, taratibu na miongozo ya Uchaguzi jambo litakalopelekea Chunya kuigwa katika Taifa hili la Tanzania

“Mabadiriko haya ya ratiba yataendelea kufanyika mara kwa mara kulingana na mapendekezo yenu ninyi viongozi wa vyama vya siasa wakati mnaendelea na Kampeni na wakati wowote mnapoona kero yoyote wasilisheni kwangu ili ifanyiwe kazi kwa wakati, Aidha niwashukuru sana viongozi wa Vyama vya siasa kwa namna tunashirikiana tangu tulipoanza maandalizi yote ya Uchaguzi na pia tuendelee kushirkiana mpaka tunakamilisha uchaguzi wetu tarehe 27/11/2024” Alisema Kambona

Naye Afisa Uchaguzi Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Ridhiwan Mshigati amewashukuru viongozi wa vyama vya siasa kwa ushiriki wao lakini pia amewakumbusha kutumia njia sahihi zinazoelezwa kwenye Sheria pindi wanapokuatana na Changamoto ili kuleta suluhu wa Changamoto iliyojitokeza wakati wa Michakato mbalimbali ya Uchaguzi inayoendelea

Kamanda wa TAKUKURU wilaya ya Chunya Ndugu David Kambona pamoja na mambo mengine aliyoelekeza wakati wa kikao hicho, aliwakumbusha viongozi wa vyama vya siasa na wajumbe wa wa kikao kwa ujumla kuzingatia Sheria, taratibu na kanuni za Uchaguzi huku akiwakumbusha kosa la Rushwa ambalo mara nyingi hujirudia katika mambo ya Uchaguzi

“Mojawapo ya makosa ambayo hufanyika mara kwa mara ni kosa la Rushwa, ni kosa kutoa fedha au zawadi kutoka kwa wagombea, kununua kura au kutoa malipo yoyote kwa mpigakura, msimamizi wa kituo nalo ni kosa, kubeba au kusafirisha wapiga kura kwaajili ya kwenda kupiga kura pia ni kosa hivyo niwaombe tuzingatie sheria za Uchaguzi” Alisema Kambona

Naye Mkuu wa Polisi wilaya ya Chunya SSP Nestory John amewataka viongozi wa vyama vya siasa kuwakumbusha wanachama wao kwamba Tanzania itaendelea kuwepo na hata wananchi wataendelea kuwepo hivyo ni vema wakatambua hili na kila jambo wafanye wakiwa wanajua maisha yataendelea

Kikao hicho kilihusisha viongozi wa Chama Cha Mapinduzi, Viongozi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Viongozi wa ACT-WAZALENDO, Viongozi CHAUMA pamoja na viongozi vya Vyombo vya Usalama wilaya ya Chunya huku lengo likiwa ni kufanya mapitio ya Mwisho wa Ratiba za Kampeni kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa utakaofanyika Mapema 27.11.2024

Kamanda wa TAKUKURU wilaya ya Chunya Ndugu David Kambona akiwasilisha mada wakati wa kikao cha Kufanya mapitia ya mwisho ya Ratiba ya Kampeni kilichofanyika ofisi ya Msimamizi wa Uchaguzi Chunya kikihusisha viongozi wa Vyama vyote vitakavyoshiriki Uchaguzi

Kamanda wa Polisi Chunya SSP Nestory John akiwasilisha mada ya Usalama wakati wa Kampeni na Uchaguzi kwenye kikao cha Viongozi wa Vyama vya siasa kilichoketi jana kwenye Ofisi ya Msimamizi wa Uchaguzi Chunya

DSO wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya akisisitiza Jambo wakati wa kikao na Viongozi wa Vyama vya siasa kuelekea Kampeni zinazoanza tarehe 20.11.2024

Afisa Uchaguzi Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Ridhiwan Mshigati akifafanua Jambo wakati wa kikao kilichoketi kikihusisha viongozi wa Vyama vya siasa vinavyoshiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.