• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

“TOKENI KWENYE SHOROBA NA HIFADHI YA MISITU”

Imewekwa: September 11th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka S Mayeka amewataka wananchi waliojenga, kuishi na kufanya shughuli mbalimbali kwenye njia za mapitio ya wanyama (Shoroba) na kwenye hifadhi ya misitu kutoka maeneo hayo kabla hawajaanza kuondolewa


Ametoa kauli hiyo mwishoni mwa juma wakati alipokuwa akisikiliza na kutatua kero mbalimbali za wananchi katika kijiji cha Bitimanyanga alipoongoza kamati ya ulinzi na usalama kusikiliza kero pamoja na kutembelea miradi itakayopitiwa na mwenge wa uhuru 2023 ambapo unatarajiwa kupokewa na kukimbizwa wilayani Chunya tarehe 13.09.2023


“Tokeni kwenye Shoroba na Misitu inayotunzwa na kuhifadhi Kisheria kwani misitu hiyo ipo Kisheria na zipo sheria ambazo zinaweza kupelekea mtu kufungwa kwasababu tu anaharibu mazingira, hivyo tokeni kabla hatujaanza kuwatoa”alisema Mhe.Mayeka


Aidha Mhe Mayeka amewataka wanachunya kuanza kuweka mipango bora ya ujenzi wa vijiji vyao ili kuhahakisha inapitika vizuri kuliko kusubiri utaratibu wa serikali ambao unaweza kuchukua muda mrefu kukamilika kuliko wanavyoweza kujisimamia wenyewe kupitia serikali za vijiji na kata kwenye maeneo wanayoishi


Meshack Furahisha, Julius Nguvumali na Janeth Haison wamewawakilisha wananchi wengine kutoa kero za maeneo yao ambazo zilijikita katika uchafuzi wa mazingira, kero za wafugaji kulisha mazao lakini pia wakulima kushindwa kulipwa fedha zao kutoka Kampuni ya Mkwawa jambo ambalo linaleta changamoto kwa maandalizi ya kilimo kwa msimu ujao


Kero zote zilipata majibu kutoka kwa Mkuu wa wilaya ambapo aliwataka wananchi kuwa wavumilivu kwani serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzanaia inajali wananchi wake hivyo suala la malipo yao linafuatiliwa kwa ukaribu sana kuhakikisha wanalipwa fedha zao


Awali akitoa salamu za wananchi wa kata ya Mafyeko Diwani wa kata hiyo Mhe Geofrey Z. Kamaka alipongeza kamati ya usalama kukubali kupeleka mkesha wa Mwenge eneo la Biti manyanga na amesema wananchi wa Bitimanyanga watautendea haki mwenge wa uhuru kwa kukesha katika eneo la Mkesha kwa utulivu


Ziara hiyo ya kamati ya Usalama ilihitimishwa kwa kukagua eneo la mkesha wa Mwenge na kutoa ushauri zaidi wa maeneo ya kuboresha tayari kwa shughuli ya mwenge ambao utapokelewa tarehe 13/9/2023 katika uwanja wa Sinjilili na baadaye Mkesha utakuwa uwanja wa mpira wa Miguu Bitimanyanga.


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.