• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

TIMU YA MPIRA WA MIGUU YA KENGOLD YA POKELEWA KWA KISHINDO CHUNYA

Imewekwa: May 9th, 2024

Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mhe. Mbarak Alhaji Batenga akimuwakilisha mkuu wa Mkoa wa Mbeya amewapongeza wachezaji wa timu ya KENGOLD kwa kurudi nyumbani na Ushindi mkubwa na kuuheshimisha Mkoa wa Mbeya, akiongeza kuwa ombi lao la kukamilisha Uwanja wa michezo Wilaya ya Chunya uliopo kata ya Mbugani amelichukua ili mashindano mbalimbali ya kimkoa na kitaifa yaweze kufanyika katika uwanja huo.

Ametoa Kauli hiyo leo tarehe 09/05/2024 katika uwanja wa Mpira wa miguu Sinjilili akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mbeya katika Mapokezi ya Timu ya Mpira wa Miguu ya KENGOLD iliyofanikiwa kutwaa kombe la Championship na kufanikiwa kupanda Ligi Kuu msimu ujao wa soka 2024/2025.

 “Ombi lenu la kukamilika kwa uwanja nimelipokea na linafanyiwa kazi na niwaahidi  uwanja wetu utakamilika , tunataka mashindano mbalimbali yafanyike katika viwanja vyetu  , timu ya Simba na Yanga zije zicheze katika viwanja vyetu pamoja na mashindano mengine yakayokuwa yanafanyika katika ngazi mbalimbali “.amesema Mhe.Batenga

Naye mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya Mhe. Bosco mwanginde amewataka  wadau mbalimbali  wa maendeleo kujitokeza kuchangia  ujenzi wa uwanja  unaojengwa katika kata ya mbugani ili timu mbalimbali ziweze kufika na kucheza katika uwanja huo  kwani  faida ya timu zinapokuja kucheza  ni biashara lakini pia burudani kwasababu timu zinapocheza wafanyabiashara wanapata fursa ya kuuza bidhaa zao na kutoa huduma mbalimbali na hatimae kujipatia kipato .

“Chunya kama itakuja timu ya Simba au Yanga tunajua tunauhakika wa kufanya biashara kwani timu ni biashara na burudani kwahiyo nawaombeni sana wadau mliopo hapa  tuchange michango yetu ili tukamilishe uwanja wetu kusudi timu  mbalimbali ziweze kuja kucheza chunya mimi na Mkurugenzi wangu tayari tumetenga bajeti  na tutasimamia kuhakikisha fedha zilizotengwa zinafanya kazi hiyo” amesema Mhe. Mwanginde

Katibu wa Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Mbeya ndugu Lukas Kubaja pamoja na kuupongeza uongozi wa Chama cha Mpira wilaya ya Chunya, amewataka vijana wenye vipaji kujitokeza kujiunga na timu ya KENGOLD lakini pia amewataka watoto wakike nao wajitokeze na kujiunga na timu ya KENGOLD kwani timu hiyo imejipanga kuwa na timu ya vijana wenye umri chini ya miaka ishirini lakini pia kuwa na timu ya kike ya mpira wa miguu.

Shamla shamla za mapokezi ya timu ya KENGOLD iliyoibuka na ushindi wa ligi daraja la kwanza zimepambwa na burudani mbalimbali huku kombe hilo likipitishwa maeneo mbalimbali ya Mkoa wa Mbeya huku viongozi mbalimbali pamoja na wananchi wakijitokeza kuilaki timu hiyo

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mbarak Alhaji Batenga akikabidhiwa Kombe kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wakati wa Mapokezi ya Timu ya KENGOLD mapema leo kwenye uwanja wa mpira wa Miguu wa Sinjilili wilayani Chunya

Umati wa wananchi wa Chunya waliojitokeza kwenye uwanja wa Mpira wa Miguu Sinjilili Kuipokea timu yao ya KENGOLD baada ya kufanikiwa kutwaa kombe la Ligi daraja la Kwanza na hatimaye kufanikiwa kupanda Ligi Kuu kwa msimu ujao 2024/2025

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.