• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

TAKUKURU CHUNYA YAWAFIKIA WATUMISHI WA AFYA

Imewekwa: September 20th, 2024

Taasisi ya kuziua na kupambana na Rushwa TAKUKURU wilaya ya Chunya imewafikia waganga wafadhi  wa vituo vya Afya na zahanati zote zilizopo wilayani Chunya ili kutoa Elimu ya namna ambavyo wanaweza kuungana na Taasisi hiyo kuzuia na Kupambana na Rushwa jambo litakalopelekea wao kama watumishi wakawa salama lakini lengo la huduma bora kwa watanzania likatimizwa bila upendeleo.

Akizungumza wakati wa Mafunzo hayo leo tarehe 20/09/2024 kwenye ukumbi wa mikutano wa Halmashauri Afisa kutoka TAKUKURU wilaya ya Chunya Ndugu Gift Chihimba amewataka waganga wafawidhi kuzingatia Sheria, kanuni, taratibu na miongozo wanapowahudumia wananchi wao, kwa njia hiyo watakuwa wametekeleza majukumu yao vizuri lakini wanakuwa wamemsaidia Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupeleka Huduma stahiki kwa wanannchi wa Tanzania wakiwepo wananchi wa wilaya ya Chunya

Mganga Mkuu wa wilaya ya Chunya Dkt Darison Andrew amesema kikao hicho kinapaswa kufanyika kila robo ya mwaka kikilenga kufanya tathimini kwa ujumla ya hali ya Afya na kupitia kikao hicho ndipo maeneo ya kuongeza mkazo hudhihirika na kuwekewa mikakati na mipango ya pamoja.

“Kikao hiki kinapaswa kufanyika kila robo mwaka na lengo lake ni kufanya tathimini ya utoaji wa huduma kwa ujumla na tumewaalika TAKUKURU kwa lengo la kutoa elimu kwa watumishi hawa ili wawe na ufahamu wa mambo mbalimbali ya kufanya na mambo ambayo hayapaswi kufanya wakati wakiendelea kuwahudumia wananchi wa Chunya" amesema Dkt Darison

Pamoja na mafunzo hayo waganga wafawidhi wa vituo hivyo wamepaza sauti kutoka Elimu iendelee kutolewa ili wanaume (Wakina baba) Watambue umuhimu wa wao kuongozana na wenza wao kwenda vituo vya kutolea huduma ili kupata ushauri wa kidaktari pamoja na kwa kufanya hivyo dalili za Rushwa na upendeleo zitakuwa zimekomeshwa jambo ambalo litapunguza zaidi vifo vya Mama wajawaziti na watoto

“Wanaume hawaongozani na wenza wao kwenda vituo vya kutolea huduma kama utaratibu ulivyokuwa umetangazwa hapo awali na tunapochukua hatua ili angalau kuhimiza wanaume kuongoza/kuambata na wenza kuja kwenye vituo vya kutolea huduma tunaanza kunyooshewa vidole kwamba tunakiuka Sheria na taratibu za kazi sasa mnapokpata nafasi Elimu iendelee kutolewa juu ya umuhimu wa wanaume kuongozana na wenza wao” Amesema Febi Ambangile

Kwa niaba ya waganga wafawidhi wengine Dkt Paul Saigod na Neema Mwafulilwa wamesema baadhi ya makosa yanatokana na mazingira yenyewe hivyo wamewaomba wasimamizi wa Sheria kutazama pande zote mbili wanaposimamia sheria hizo kuamua juu ya changamoto zinazokuwa zimejiokeza kwani wakati mwingine changamoto inajitokeza sio kwa makusudi.

Elimu ya Mapambano dhidi ya Rushwa ikiwafikiwa vizuri watumishi wa umma na wananchi kwa ujumla itasaidia kuweka usawa na haki na upatikanaji wa huduma katika Halmashauri ya wilaya ya Chunya na Tanzania kwa ujumla jambo ambalo litapelekea kila mtanzania kufurahia maisha ndani ya nchi yake.

Afisa kutoka TAKUKURU Chunya Bwana  Gift Chihimba akiendelea kutoa Elimu wakati wa kikao cha Waganga wafawidhi wa vituo vya Afya na Zahanati wilayani Chunya kilichoketi kwenye ukumbi wa Halmashauri ya wilaya  uliopo kwenye Jengo Jipya la utawala

Febi Ambangile (Aliyekaa na amenyoosha mkono) ambaye ni moja katia ya washiriki wa Mafunzo hayo akifafanua jambo kwa Afisa TAKUKURU wakati wa wasilisho lake

Bwana Paul Saigod (Aliye simama akionekana akizungumza kwa vitendo) ni moja ya washiriki wa kikao hicho na hapo alikuwa akifafanua jambo wakati wa wasilisho kutoka kwa afisa TAKUKURU wilaya ya Chunya

Mfamasia wa wilaya ya Chunya Dkt Edward Tengulaga akiendelea na wasilisho lake wakati wa Kikao na Waganga wafawidhi wa vituo vya Afya na Zahanati zilizoko wilayani Chunya kilichoketi Mapema leo ili kufanya tathimini ya utoaji wa Huduma kwa Ujumla wake

Waganga wafawidhi wa vituo vya Afya na Zahanati wilayani Chunya wakiwa wanafuatilia Mafunzo kutoka kwa Afisa TAKUKURU pamoja na Mada nyingine zilizowasiliwashwa mapema leo wakati wa kikao cha Tathimini wa utoaji wa huduma

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.