• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

SUALA LA LISHE NI LA JAMII NZIMA

Imewekwa: May 2nd, 2024

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mbarak Alhaji Batenga amewataka watendaji wa kata na vijiji pamoja na Jamii kwa ujumla kushiriki ipasavyo katika suala la Lishe kwa Familia zao na Jamii kwa ujumla kwani kwa kufanya hivyo ni kuisaidia Jamii ya sasa na ya baadaye kiafya, kiuchumi na Kijamii jambo ambalo litahakikisha ustawi wa Jamii ya wanachunya na Taifa kwa Ujumla

Akiongoza kikao cha Lishe kwa robo ya tatu ya mwaka 2023/2024 kilichoketi leo tarehe 2/5/2024 kwenye ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya ulipo jengo jipya la utawala amewataka watendaji wa kata na Vijiji kutokuwaachia wahudumu wa Afya ngazi za kata na vijiji kusimamia suala la Lishe bali washirikiane kwa pamoja ili kuhakikisha Jamii inatambua na inazingatia suala la Lishe kama mikataba inavyoelekeza.

“Kila mtendaji anapaswa kushiriki ipasavyo kwenye shughuli za lishe, msiwaachie wahudumu wa Afya ngazi za kata na vijiji wasimie suala la Lishe. Tunaondoka hapa tukiwa na kauli moja wanafunzi wote wa madarasa ya awali bila kuacha wanafunzi wa madarasa mengine kuanza kupata Chakula wanapokuwepo Shule. Lakini pamoja na kuwepo mikata tuliyosaini inayotutaka tusimamie suala la Lishe, Watendaji wote waandikiwe Barua ya kuwataka kusimamia vizuri suala la Lishe ili akitokea mtu analega basi tumchukulie hatua stahiki” amesema Mhe Batenga

Akichangia mjadala wa uongezaji wa virutubisho kwenye unga Afisa biashara wa wilaya ya Chunya ndugu Rodrick Mwakisole amesema kama Elimu ya namna ya kuongeza virutubisho ikiwafika vema waanchunya watapata fursa kubwa zaidi ya kibiashara na hatimaye kuongeza vipato vyao na baadaye kuongeza pato la Halmashauri na Taifa kwa Ujumla.

“Suala la Lishe pamoja na kuimarisha Afya za watoto wetu na jamii kwa ujumla lakini katika mchakato wa kuongeza virutubisho kuna fursa kwa wananchi kiuchumi kwani kupitia kufunga vifaa vya kuongeza virutubisho vitaongeza idadi ya watu kuja kusaga katika mashine hizo na baadaye fursa nyingine zitaendelea kufunguka hivyo ni vema wananchi wakaelimishwa juu ya suala hilo”

Naye Mganga Mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Dkt Darison Andrew pamoja na kushukuru usimamizi mzuri wa mwenyekiti katika suala la Lishe, ameendelea kuwahimiza watendaji wa kata na vijiji na hata wanajamii kuongeza juhudi ya kuzingatia lishe kwa jamii yao kwani athari za ukosefu wa lishe ni kubwa na ngumu kurudi katika hali ya kawaida ikitokea athari hizo zikijitokeza katika jamii zetu.

“Tukiwekeza kwenye lishe Itasaidia kuwa na kizazi sahihi na chenye uwezo mzuri wa kufikiri. Hivyo watendaji wa kata na vijiji kwa nafasi zenu endeleeni kutoa Elimu hii kwa wanajamii na tukifanya hivyo tutakuwa tumeoka familia zetu na hata Taifa kwa ujumla, Gharama za udumavu ni kubwa sana hivyo tupambane pamoja kuondokana na udumavu huo” Amesema Dkt. Andrew

Afisa Lishe Halmashauri ya wilaya ya Chunya Bi Rehema Hiluka amemshukuru Mkuu wa wilaya ya Chunya ambaye ndiye mwenyekiti wa Kikao cha Lishe kwa namna ambavyo amekuwa mstari wa Mbele kuhakikisha suala la Lishe linazingatiwa na viongozi pamoja na wananchi huku akihimiza ushirikiano kati ya viongozi na wananchi katika kuhakikisha suala la lishe linazingatiwa katika maeneo yao

Kikao cha lishe kwa robo ya tatu 2023/2024 kimehudhuriwa na watendaji wa Kata na vijini Halmashauri ya wilaya ya Chunya pamoja na wakuu wa idara na vitengo wanaotekeleza Afua za Lishe na kilihusisha upimaji wa uzito, urefu pamoja na Kisukari kwa hiari ikiwa ni kuwajali wajumbe wa kikao pamoja na watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya.

 Afisa Biashara wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Rodrick Mwakisole akiwasilisha jambo kwenye kikao cha Lishe robo ya tatu 2023/2024 kilichoketi leo kwenye ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya (Jengo Jipya la Utawala

Mganga Mkuu wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Dkt Darison Andrew akisisitiza Jambo wakati wa kikao cha Lishe kwa Robo ya Tatu kilichoketi tarehe 2/5/2024 kwenye ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya (Jengo Jipya la utawala)

Afisa Lishe wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Bi Rehema Hiluka akizungumza Jambo wakati wa kikao cha Lishe kwa Robo ya tatu ya mwaka 2023/2024

Mtendaji wa kata ya Kasanga Ndugu Lwitiko Mwalugaja akifafanua Jambo wakati wa kikao

Afisa Lishe wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Bi Rehema Hiluka akiwasilisha taarifa ya Umuhimu wa kuongeza virutubisho kwenye unga wakati wa kikao cha Lishe cha Robo ya Tatu mwaka 2023/2024

Afisa Lishe Ndugu Saimon Mayala anayesoma kwenye Mzani) akitazama urefu wa Mtendaji wa kata ya Lualaje tayari kulinganisha na urefu wake wakati wa zoezi la kupima urefu, uzito na kisukari leo wakati wa kikao cha Lishe kwa robo ya tatu mwaka 2023/2024

Wahudumu wa Afya wakiendelea kutoa huduma ya vipimo vya urefu, uzito, Kisukari na Presha wakati wa kikao cha Robo ya tatu ya mwaka 2023/2024 kilichoketi leo tarehe 2/5/2024

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.