• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

SIMAMIENI PESA HIZI KAMA PESA ZENU

Imewekwa: October 4th, 2023


Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango Halmashauri ya wilaya ya Chunya imewataka viongozi wa serikali na wananchi kusimamia pesa za serikali ipasavyo ili kufikia lengo la serikali la kuleta fedha kutekeleza miradi katika meeneo mbalimbali ya wilaya ya Chunya kufikiwa


Kauli hiyo imetolewa leo terehe 04/10/20234 na kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango kupitia mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe Bosco S. Mwanginde wakati alipoiongoza kamati hiyo kukagua utekelezaji wa miradi mbalimbali katika Halmashauri ya wilaya ya Chunya ambapo kupitia ziara hiyo kamati ilifanikiwa kukagua miradi yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni mbili


“Simamieni pesa hizi kama zenu kwani kwakufanya hivyo pesa nyingine zinazobaki zitatumika kuanza kujenga mradi mwingine eneo lingine lakini mnanunua dawati shilingi elfu hamsini (50,000) eneo hili la Mpembe wakati mnayo miti mingi kuliko maeneo mengine tuliyopita!  haiwezekani kabisa”


Aidha Mwenyekiti wa kamati hiyo aliongeza kusema “ Wataalamu hamtusaidii kabisa yaani mnaacha mafundi wanaharibu thamani zilizonunuliwa kwa fedha za serikali, wanaharibu saruji, malumalu yaani hamsimamii miradi ya maendeleo ipasavyo jambo linalopelekea kukwama kwa mradi au kutokamilika kwa fedha zilizotengwa” aliongeza Mhe Mwanginde


Katika kukamilisha ziara hiyo kamati ilitembelea mradi wa ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya msingi Mapogolo iliyopo kata ya Chokaa ambapo ilipongeza usimamizi mzuri wa mradi huo kwani umekamilika kwa wakati na samani zilizowekwa ndani ya madarasa hayo zimefuata maelekezo ya serikali


Diwani wa kata ya Chokaa Mhe Samwel Komba kwa niaba ya wananchi wa kata hiyo amewashukuru kamati kwa ujumla wake kwanza kuwapatia fedha za kutekeleza mradi huo lakini pia amesema bado kata ya Chokaa inauhitaji sana hivyo amewaomba wakiona inafaa waendelee kuwapatia fedha ili waendelee kutekeleza miradi ya maendeleo kwa kiwango ambacho serikali inaagiza


Ziara ya Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ikihusisha wataalamu kutoka Halmashauri ya wilaya ya Chunya ilianza  tarehe 2/10/2023 na kutamatika tarehe 4/10/2023 ambapo miradi mbalimbali imekaguliwa huku maoni na maagizo  mbalimbali kutoka kwa wajumbe wa kamati hiyo yakitolewa ili kuboresha zaidi ujenzi wa miradi hiyo.

Vyumba viwili na ofisi vilivyojengwa katika shule ya msingi Mpembe na wanaoonekana ni wajumbe na wataalamu wa kamati ya Fedha Uongozi na Mipango wakiendelea na ukaguzi wa mradi ukilinganishwa na fedha zilizopelekwa kutekeleza mradi huo

Diwani wa kata ya Kasanga na Mjumbe wa kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango Mhe. Mh. Benson B. Msomba akichangia jambo wakati wa ziara ya kamati hiyo walipokuwa wanakagua ujenzi wa matundu ya Vyoo shule ya Msingi Mpembe

Mwenyekiti wa kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango Mhe Bosco S Mwanginde akitoa maagizo ya Kufukiwa Shimo lililokuwa limechimbwa kwaajili ya kuhifadhi maji wakati wa ujenzi wa madarasa kwani linahatarisha usalama wa wanafunzi wawapo shuleni

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.