• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

SERIKALI ITAENDELEA KUPOKEA MAELEKEZO YA CHAMA KATIKA KUTATUA CHANGAMOTO ZA WANANCHI WA CHUNYA

Imewekwa: May 31st, 2024

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mbarak Alhaji Batenga amesema Serikali wilaya ya Chunya itaendelea kupokea maelekezo ya Chama na kuyatekeleza pamoja na kuhakikisha yale yaliyoahidiwa kwenye Ilani ya Uchaguzi yanatekelezwa kwa asilimia mia moja ili kuondoa maswali kwa wananchi wa Chunya kuhoji uhitaji au ubovu wa miundombinu yoyote ile ya utoaji wa huduma.

Ametoa kauli hiyo tarehe 30/5/2024 wakati akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Igundu kwenye viwanja vya Shule ya Msingi Igundu wakati wa Hafla ya kukabidhiwa mradi wa Maji uliotekelezwa kwa ushirikiano kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia RUWASA, Shirika na Catholic Relief Services (CRS) pamoja na wananchi wa Igundu

“Sisi kama Serikali tunaahidi kuendelea kupokea maelekezo ya Chama na kuyatekeleza ili kuondoa Maswali kutoka kwa wananchi kuhusu Serikali yao, Wananchi waendelee kuiamini Serikali yao kwani ni sikivu na yenye kuwajali wananchi wake” Alisema Mhe Batenga

Diwani wa kata ya Sangambi Mhe Junjuu Muhewa kwa niaba ya wananchi wa Kijiji cha Igundu na Kata ya Sangambi kwa ujumla amewashukuru Shirika na Catholic Relief Services (CRS) pamoja na Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kupelekewa fedha nyingi za kutekeleza miradi mbalimbali ikiwa ni pamoja na mradi wa maji uliokabidhiwa kwa wananchi wa Igundu baada ya kukamilika kwa asilimia mia moja

“Nimehemewa na furaha kwasababu ya furaha, Naomba nitoes Shukrani zangu kwa Shirika hili la CRS linalofanya kazi kwa karibu na serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inayoongozwa na Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan. Pamoja na Mradi huu wa Maji tunaokabidhiwa leo kata yangu ya Sangambi imepokea fedha zaidi ya Bilioni Mbili kutekeleza miradi mbalimbali hivyo naomba nipelekee salamu zangu na za wananchi hawa wa Igundu na wananchi wa kata ya Sangambi kwa Mhe Rais Samia kwamba wanasangambi tunamshukuru sana” Amesema Mhe Junjulu

Meneja wa RUWASA wilaya ya Chunya Mhandisi Olineno Sanga amesema utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwenye sekta ya Maji wilaya ya Chunya imefikia asilimia themanini na tano (85%) huku akisema mipango yao ifikapo 2025 kata ya Sangambi itafikia asilimia mia moja katika upatikanaji wa Maji safi na salama kwa matumizi ya Binadamu

“Kwa maana ya utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi tumeshafikia azma ya Serikali kwa maana ya asilimia themanini na tano (85%) lakini pia tumekuwa na mipango mbalimbali tumebakiza kijiji kimoja cha Shoga lakini pia kitongoji kimoja cha Dendeluka, Rais ameshatoa fedha kwaajili ya upatikanaji wa Maji kwenye maeneo hayo na ni matumaini yetu ifikapo 2025 tutafikia asilimia mia moja upatikanaji wa maji katika kata ya Sangambi” Amesema Mhandisi Sanga

Mkuu wa ofisi ya CRS Mkoa wa Mbeya Bi Marilyn Chottah amesema, Mradi huo umegharimu shilingi milioni mia nne thelasini na nne huku asilimia Zaidi ya themani ya fedha hizo zikitolewa na shirika la CRS na mradi unalenga kuwahudumia wananchi 4883 wa Kijiji cha Igundu huku Taasisi za Serikali kama vile Zahanati ya Igundu na Shule ya Msingi ya Igundu zikinufaika moja kwa moja na mradi huo kwa kujengewe miundombinu mbalimbali ya maji ambayo imeunganishwa moja kwa moja na maji hayo

“Mradi huu umegharibu shilingi milioni mia nne thelasini na nne elfu mia mbili sabini na tano na laki tatu na hamsini na sita elfu (434,275,356,000/=) huku ashilingi miliomni ia tatu sabini na tano ambazo ni sawa na silimia 86.5% ya fedha zote za mradi zikitolewa na shirika na Catholic Relief Services CRS na Lengo na Mradi ni kuwahudumia wananchi wa Igundu ili waepukane na changamoto ya maji” Amesema Bi Chottah

Shirika na Catholic Relief Services (CRS) linatekeleza miradi mbalimbali katika Halmashauri ya wilaya ya Chunya huku Mradi wa Ifumbo umeshakamilika na unatumika, Mradi wa Igundu kata ya Sangambi umekamilika na umekabidhiwa Jana tarehe 30/5/2024 na Mradi mwingine unatekelezwa kata ya Kasanga kijiji cha Soweto umefikia asilimia karibu Themanini (80%) na Lengo kubwa ya CRS ni kuhakikisha linashirikiana na Serikali kutatua changamoto za wananchi wa wilaya ya Chunya zinatatuliwa kwa wakati.

Mhandisi wa RUWASA Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mhandisi Olineno Sanga akifafanua Jambo wakati Mkuu wa wilaya ya Chunya akikagua miundombinu ya mradi wa Maji wa Igundu Kabla ya kuukabidhi kwa wananchi baada ya kukamilika kwa asilimia mia moja tayari kwa matumizi ya Mradi huo

Baadhi ya wananchi waliojitokeza kuupokea mradi wa Maji uliotekelezwa kwa ushirikiano wa Serikali, CRS pamoja na wananchi wenyewe kwenye Kata ya Sangambi kwenye kijiji cha Igundu

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.