• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

RC HOMERA “MADINI HAYAPIMWI KWA MGANGA WA KIENYEJI”

Imewekwa: February 8th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Zuberi Homera amesema serikali inataka wawekezaji wengi waendelee kuwekeza kwenye sekta ya madini ili kuendelea kuleta tija katika uzalishaji wa madini huku akisisitiza kuwa serikali itaendelea kuwajali kwakuhakikisha inaweka mazingira wezeshi kwao ikiwa ni pamoja na kusogeza masoko ya dhahabu, kurahisisha upatikanaji wa vifaa vya kuchimbia dhahabu na hata kemikali zinazotumika katika zoezi zima la Uchenjuaji wa dhahabu

Mhe: Homera amewataka viongozi wa serikali pamoja na jeshi la polisi kuhakikisha wawekezaji waliowekeza katika uchimbaji dhahabu wanakuwa salama wakati wote ili waweze kutoa mchango wao kwa serikali kama wanavyoendelea kutoa sasa, kwa kulipa kodi kwa wakati na kutoa ajira mbalimbali kwa wananchi na hatimaye kuleta maendeleo kwa Taifa.

Mkuu wa Mkoa yuko katika ziara ya siku mbili kutembelea sekta ya madini katika mkoa wa kimadini chunya ambapo ameshatembelea ghala la RM KYANDO COMPANY LTD ambapo amekagua mitambo na kemikali mbalimbali za kuchenjulia dhahabu, pia ametembelea maabara inayohusika na shughuli mbalimbali za upimaji wa sampuli za madini ya RM KYANDO COMPANY LTD, ametembelea Mine labs assay Geochemical analysis laboratory, Giant Machine and equipments na maeneo mengine

Aidha Mkuu wa Mkoa wa Mbeya amewataka wananchini kutumia maabara za kisasa zilizopo katika mkoa wa madini chunya kwani zinasaidia sana katika kuchimba kwakujua eneo husika lina kiasi gani cha madini na sio kuchimba kienyeji, kwanza kuna uharibifu mkubwa wa mazingira lakini pia unaweza kutumia nguvu kubwa kuchimba eneo ambalo halina madini

“Madini hayapimwi kwa mganga wa kienyeji, bali kwa mitambo hii ya kisasa kabisa, hivyo wananchi njooni mpime sampuli za madini eneo unalotaka kuchimba na Nyinyi wenye mitambo endeleeni kuwa wabunifu zaidi wa teknolojia ya uchimbaji madini ili muweze kuwasiaidia wananchi”

Afisa madini Mkaazi wa Mkoa wa Chunya Eng. Nyansiri Sabai akizungumza mbele ya Mkuu wa mkoa wa Mbeya amesema kwasasa kemikali zote zinazotumika kuchenjulia dhahabu zinapatikana chunya jambo ambalo limewarahisishia wachimbaji kutokuhangaika kuzitafuta na ameongeza kuwa ghara lingine linalojengwa na Giant Machine and Equipments litaendelea kuleta suluhu na ahueni ya bei ya kemikali kwa wachimbaji.

“Kukamilika kwa ujenzi wa ghala hili linalojengwa na Giant Machine equipments litasaidia sana kupunguza bei ya gharama ya kemikali ikiwezekana hata chini ya bei elekezi ya serikali laki sita (600,000)” amesema Eng. Nyansiri

Awali akizungumza mbela ya Mkuu wa Mkoa Aidan Msigwa (Mdimi) ameeleza changamoto mbalimbali ambayo yeye pamoja na wachimbaji wengine wanapitia huku akipeleka ombi kwa ofisi ya Mkuu wa Mkoa na serikali kwa ujumla wake kusaidia kuleta suluhu ili waendelee kuzalisha kwa tija na kuendelea kulipa kodi kwa mujibu wa sheria

Baadhi ya chnagamoto alizoeleza msigwa ni pamoja na taasisi za fedha kushindwa kuwaamini kuwapa kiasi cha fedha wanachohitaji ili kuendesha shughuli zao jambo linalofanya waingie kwenye taasisi zenye riba kubwa jambo ambalo linarudisha nyumba mipango yao na baadaye kushindwa hata kulipa kodi kwa wakati

Changamoto nyingine ni pamoja na bei ya mafuta (Disel) imekuwa kubwa sana kupelekea uendeshaji wa shughuli za uchimbaji kuwa ngumu, kemikali za kuchenjulia dhahabu pia ilikuwa gharama kubwa jambo linaloleta changamoto katika uzalishaji

Pamoja na mambo mengine mengi yaliyofanyika katika ziara hiyo, Mkuu wa Mkoa amewashukuru wadau wote waliowekeza kwenye sekta ya madini kwani juhudi zao zimefanya mkoa wa kimadini chunya kuwa nafasi ya pili katika uzalishaji wa madini Tanzania ikitanguliwa na Geita na ameawataka kuendela kuongeza kasi

Katika ziara hiyo ambayo inataraji kuendelea tena Kesho tarehe 9/2/2023 Mkuu wa Mkoa ameendelea kuwaalika kwenye maonesho makubwa ya madini yanayotaraji kufanyika katika mkoa wa kimadini Chunya ambapo mambo mbalimbali yatajadiliwa huku akiwataka wadau wa madini kuhakikisha wanashiriki maoneshon hayo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Mine labs Geochemical Analyisis Labaratory Eng. Simon Shinshi (Mwenye kofia) akitoa maelezo kwa mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Zuberi Homera wakati wa ziara ya kutembelea sekta ya madini katika mkoa wa kimadini chunya.

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.