• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

RC HOMERA AIPONGEZA WILAYA YA CHUNYA KUFANYA VIZURI KATIKA SEKTA YA MADINI

Imewekwa: March 18th, 2023

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe, Juma Zuberi Homera amesema mkoa wa kimadini Chunya unafanya vizuri sana katika sekta ya madini jambo linalopelekea uzalishaji wa madini kuongezeka kutoka kilograma 20 mpka kufikia kilogramu 330 kwa mwezi ambapo zaidi ya Bilioni thelasini hupatikana kupitia sekta ya madini

Homera amesema hayo Mapema jana wakati akifunga maonesho ya kwanza ya Teknolojia ya Madini yalitofanyika kuanzia tarehe 14/03/2023 katika viwanja vya Chunya kati vilivyopo  halmashauri ya wilaya ya Chunya ambayo hutambulika kama mkoa wa kimadini Chunya

“Kwakweli Chunya mnafanya vizuri sana katika sekta ya madini kuanzia wachimbaji wakubwa na wachimbaji wadogo hakika kwakweli tunastahili kuwapongeza sana sana wanachunya wote kwa kazi kubwa mnayoifanya”

Homera amesema maelekezo aliyoyatoa Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan ya kulegeza mashariti katika sekta ya uchimbaji ndiyo yanayopelekea kuwa na wawekezaji wengi wilayani chunya Huku wawekezaji wazawa  kuongezeka katika sekta ya Madini

“Tumeshuhudia wawekezaji wengine wamewekeza kwenye sekta ya madini hapa wilayani Chunya, tumejionea makampuni makubwa kama vile Ramani Investment, kina Achimwene, Kindai Investment, Sunshine, Msigwa na mengine mengi, Yote haya ni kutokana na maelekezo aliyoyatoa Mhe. Rais ya kulegeza mashariti ya kuingiza vifaa vya uchimbaji hivyo ni lazima tumpongeze sana Mweshimiwa Rais kwa kuamua kuwekeza kwenye sekta ya Madini”

Kwakukumbuka kifo cha Rais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Mhe. Dkt John Joseph Magufuli, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya amewaongoza wananchi waliojitokeza katika maonesho hayo kutulia kwa dakika moja ikiwa ni ishara ya kumkumbuka, kuenzi na kumwombea kheri apumzike kwa amani huko aliko

Kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi, Katibu tawala wa Mkoa wa Mbeya ndugu Rodrick Mpogolo amsema sekta ya madini ina Mchango mkubwa kwa Taifa na kwa jamii kuanzia ngazi ya familia na kaya moja moja hivyo kupitia maonesho haya ni imani yetu wachimbaji wamepata elimu, fursa mbalimbali zimefunuliwa na mambo mengine

Aidha katibu tawala huyo amesema maonesho haya yalianza rasmi tarehe 14 mwezi machi na kutamatika tarehe 18 machi hivyo wafanyabiashara na wadau wote wa madini wametakiwa kuendelea kutumia fursa hiyo ya kukutana na wafanya baishara mbalimbali na wadau wa madini kutoka Chunya na nje ya Chunya ili kuendelea kukuza vipato vyao

Awali akitoa salamu za wachimbaji kwa Mgeni rasmi, Mwenyekiti wa wachimbaji katika mkoa wa imadini Chunya Ndugu Leonard Manyesha amewasilisha kilio cha wachimbaji kwa Mkuu wa Mkoa huo ambazo ni pamoja na Tozo kuto Mamala ya mapata Tanzania, Taasisi za kifedha kutowaamini wachimbaji na kuwakopesha ili waendeleze shughuli zao za kiuchimbaji

“Sisi wachimbaji tunaimani kubwa sana kwa serikali hii hivyo kupitia Maonesho haya tunaamini changamoto zetu zinaenda kutatuliwa mfano Tozo za TRA, tunaamini uchimbaji katika Mkoa huu utaendela kukua zaidi, Pia tunaomba taasisis za kifedha kuwakopesha wachimbaji. Na tuna amini maonesho haya yataendelea kuwepo kila mwaka ili wachimbaji waendelee kujifunza fursa mbalimbali zilizopo katika madini”

Maonesho ya Teknolojia ya Madini yamefanyika kwa mara ya kwanza katika Mkoa wa Kimadini Chunya kuanzia tarehe 14 march na kutaraji kutamatika tarehe 18 machi 2023 ambapo wadau mbalimbali wa sekta ya madini wamekutana kubadilishana uzoefu katika sekta hiyo na kauli mbiu ya maonesho hayo ilikuwa ni “Uongezaji wa thamani ya madini kwa maendeleo ya taifa”

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.