• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

RC Homera aipongeza H/shauri Chunya kwa Ujenzi bora wa Miradi ya Maendeleo

Imewekwa: January 17th, 2022

MKUU wa mkoa wa Mbeya, Juma Homera ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Chunya na viongozi wake kwa ujenzi wa miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa kituo cha afya Sangambi.

Homera ametoa pongezi hizo wakati wa ziara ya Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa alipokuwa wakikagua miradi ya maendeleo katika Wilaya ya Chunya.

“Maeneo mengine nimepita, hii ni Halmashauri yangu ya sita, kote nilipopita waje wajifunze Chunya, kule nimepita hawajajenga majengo yote, wamejenga OPD tu, lakini Chunya mmejenga majengo ya kutosha kuanzisha kituo cha Afya." Alisema Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Juma Homera.

Pia Mkuu wa Mkoa amewapongeza wananchi wa kata ya Sangambi kwa kujitolea nguvu kazi zao na kuhakikisha ujenzi wa kituo cha afya Sangambi unakwenda vizuri na kukamilika kwa wakati.

Miradi iliyotembelewa na kamati hiyo ni pamoja na ujenzi wa kituo cha afya Sangambi na ujenzi wa soko la madini ikiwa miradi hiyo inatekelezwa kwa fedha za mapato ya ndani.

Ujenzi wa kituo cha afya unakadiriwa kutumia kiasi cha shilingi milioni mia sita, ambapo kati ya hizo shilingi milioni 500 kutoka Halmashauri ya wilaya ya Chunya kama mapato ya ndani na milioni 100 kutoka kwa wananchi wa kata ya Sangambi.

"Mkurugenzi usione shida kuendelea kuleta miradi kwa wananchi wanaojitoa, kwa wananchi wanaojitolea sana wewe shusha miradi tu kwa sababu hawatuangushi.” Amesema Homera.

Aidha Mkuu wa Mkoa huyo ameutaka uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kuhakikisha ifikapo Mei mosi, kituo cha afya kianze kufanya kazi na kutoa huduma kwa wananchi wa Sangambi.

Kwa sasa wananchi wa kata ya Sangambi wanapata huduma kwenye kituo cha afya cha Charangwa ambacho kipo umbali wa kilomita 19 au kwenda kwenye hospitali ya Wilaya ya Chunya ambayo ipo umbali wa kilomita 32 kutoka Sangambi.

Kwa upande wa ujenzi wa soko la madini, Homera ameutaka uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kuhakikisha ifikapo mwezi wa tano soko hilo liwe limekamilika na kuanza kutumika.

Pia, Homera amezita benki zote ambazo zimeonesha nia ya kuwekeza katika jengo hilo kuhakikisha wanaweka matawi yao ambayo yatakuwa msaada kwa wafanyabiashara wa dhahabu.

“Sisi tunawapa muda mpaka ifikapo mwezi wa tano hizo benki zote zilizoonesha dhamira ya kuwekeza katika soko hili wawe wameshafanya utaratibu wa kufungua matawi hapo vinginevyo tutaalika benki nyingine zije zifanye biashsara hapa.

“Hatutamvumilia mtu yeyote ambaye atakuwa anatorosha dhahabu Wilayani Chunya tutachukua hatua kama ambavyo tumechukua hivi karibuni kutaifisha zaidi ya gram 900, dhamira yetu sisi kuuza kwenye soko letu hili ili Chunya iendelee kukusanya mapato, hatuwezi kujenga hapa watu wakauzie dhahabu vichochoroni tutachukua hatua kali.” Alisema Homera.

Jengo la Mama na Mtoto pamoja na Wodi  katika Ujenzi wa Kituo cha Afya Sangambi

Jengo la OPD Ujenzi wa Kituo cha  Afya Sangambi

Muonekano wa majengo Mengine katika Ujenzi wa Kituo cha Afya Sangambi

Soko la Dhahabu Linalojengwa na Halmashauri  ya Wilaya ya Chunya kwa Mapato ya Ndani

Muonekano wa ndani katika Ujenzi wa Soko la Dhahabu

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.