• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

RC HOMERA AIPONGEZA HALMASHAURI YA CHUNYA KUSIMAMIA VYEMA MRADI WA MAJI MATUNDASI.

Imewekwa: February 10th, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mhe. Juma Zuberi Homera ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kwa usimamizi mzuri wa utekelezaji wa mradi wa maji Matundasi ambapo unahudumia zaidi ya wakazi 9,000 katika vitongoji vya Matundasi A, B pamoja na kitongoji cha Kisimani.

Akizungumza leo, Februari 2, 2025 kwenye ziara ya kikazi alipokuwa akikagua mradi wa maji Matundasi uliopo katika kitongoji cha Kisimani wilayani Chunya , Mhe. Homera amesema suala la maji ni muhimu sana kwa wananchi ndio maana miradi ya maji inatekelezwa katika maeneo mbalimbali kwenye mkoa wa Mbeya huku dhamira ya serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassani ni kumtua mama ndoo kichwani.

“Naupongeza uongozi wote wa Wilaya ya Chunya kwa kusimamia utekelezaji wa mradi wa maji Matundasi na kupambana na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu, Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ilikuwa miongoni mwa waathirika wa ugonjwa huu, na ukweli ugonjwa umepungua na hatuoni magonjwa hata mmoja katika hospitali zetu” amesema Mhe. Homera.

Katika hatua nyingine, Mhe. Homera ametoa wiki mbili kwa meneja wa RUWASA Wilaya ya Chunya kuunganisha mtandao wa maji kutoka kwenye mradi kwenda kwenye makazi ya wananchi wa kitongoji cha Kisimani kwakuwa mradi wa maji upo kwenye eneo lao na ndipo ulipojengwa.

Dhamira ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Rais Samia Suluhu Hassani ni kuwafikishia wananchi huduma ya maji safi na salama kwenye kaya zao na sio kubeba maji kichwani, amesisitiza Mhe. Homera.  

“Haiwezekani mtandao wa maji uende kwenye vitongoji vingine vya mbali halafu kitongoji hiki cha kisimani ambapo mradi umetekelezwa wakose maji, wananchi wa Kisimani ndio walinzi wa miundombinu hii ya mradi wa maji, natoa siku 14 Kitongoji cha Kisimani kuunganishiwe maji kama vijiji vingine” amesema Homera.

Awali akisoma taarifa ya utekelezaji wa mradi wa  maji Matundasi uliopo katika kijiji cha Kisimani, Kaimu Meneja wa RUWASA Wilaya ya Chunya, ndugu Shabibu Ayubu amesema mradi wa maji Matundasi umetekelezwa kwa Shilingi Milioni 350 kwa ufadhili wa P4R, mradi ulianza April 14, 2024 na kukamilika tangu Agosti 15, 2024.

Pump iliyofungwa kwenye mradi wa maji Matundasi ina uwezo wa kuvuna maji lita 17,500 kwa saa. Mradi wa maji Matundasi umekamilika kwa asilimia mia moja na unahudumia wakazi zaidi ya 9,000 wa vitongoji vya Matndasi A, B na kitongoji cha Kisimani. Amesema Ayubu.

Mkuu wa Mkoa Mbeya, Mhe. Juma Himera akisikiliza taarifa ya utekelezaji wa mradi wa maji Matundasi iliyosomwa na  Kaimu Meneja wa RUWASA Wilaya ya Chunya, ndugu Shabibu Ayubu.

Muonekano wa Tanki la maji katika mradi wa maji Matundasi ambao unahudumia zaidi ya wakazi 9,000 katika vitongoji vya Matundasi A, B pamoja na Kitongoji cha Kisimani.

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.