• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA KATA WATAKIWA KUSIMAMIA UREJESHWAJI WA MIKOPO..

Imewekwa: December 30th, 2025

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya wakili Athumani Bamba ameitaka kamati ya usimamizi wa mikopo ya  asilimia  10 ngazi ya kata  kuhakikisha wanasimamia vyema urejeshwaji wa mikopo  hiyo unaotelewa kwa wanawake , vijana na watu wenye ulemavu  ili kuwezesha wananchi wengi kunufaika na mikopo hiyo

Hayo ameyasema leo tarehe 30/12/2025 wakati wa kikao kazi cha kamati ya  mikopo ngazi ya kata kilichoketi katika ukumbi wa mikutano wa Mwanginde Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kikijumuisha  watendaji wa kata ambao ndio  wenyeviti na Maafisa maendeleo ya jamii ambao ni Makatibu wa kamati hiyo

Aidha Wakili Bamba meongeza kuwa kutakuwa na motisha kwa  wajumbe   ambao watatekeleza majukumu yao vizuri  hususani  kusimamia urejeshwaji ya mikopo hiyo kwa wakati uliopangwa kwani kwakufanya hivyo  kutasaidia kuongeza morali ya ufwatiliaji wa mikopo hiyo na kuongeza wigo wa wanufaika wa mikopo hiyo  .

Mkuu wa idara ya Maendeleo ya Jamii Bi Marietha Mlozi amesema kuwa moja ya majukmu ya kamati hiyo ni  ni pamoja kupokea, kujadili na kuchambua  maombi ya mikopo iliyopokelewa,kufanya tathimini ya vikundi vilivyowasilisha maombi  ikiwa ni pamoja na kuvitembelea na kuvikagua , kufanya fwatiliaji wa marejesho ya mikopo hiyo na majukum mengine .

 Akizungumza katika kikao hicho Mkuu wa Idara ya utawala ndugu Jummanne Chaula amesema kuwa  Mkurugenzi ametoa vitendea kazi ili  kurahisisha utendaji kazi wa idara ya maendeleo ya jamii ikiwa ni pamoja na kutoa mikopo kwa vikundi vyenye uhitaji wa mikopo hiyo lakini pia kuhakikisha wanafuatilia urejeshwaji wa mikopo hiyo kwa wakati  kwa kushirikiana na kamati ya mikopo ngazi ya kata ili kuwawezesha na watu wengine waweze kunufaika na mikopo hiyo ya asilimia 10.

Naye Mkuu wa kitengo cha ukaguzi ndugu Herbeth Matugwa amesema kuwa mikopo ya asilimia 10 ni  sehemu ya miradi ya serikali kama ilivyo miradi mingine ya maendeleo inayotekelezwa na Halmashauri Hivyo kama wajumbe wanapaswa kusimamia na kutimiza majukum yao ili kuhakikisha mikopo inarejeshwa kwa manufaa ya Halmashauri na wanachunya kwa ujumla

“Miradi yote inayotekelezwa kwenye kata usimamizi wake uko kwenu , hii mikopo inayotolewa ni sehemu ya miradi ya serikali kama ilivyo  miradi mingine  ya Shule , zahanati  na miradi mingine hivyo mkasimamie  majukum yenu vizuri kuhakikisha mikopo inarejeshwa ili kuiepusha Halmashauri dhidi ya hati chafu” amesema Matugwa .

Wakizungumza kwa niaba ya wajumbe wengine  Ndugu Egitho Bilali  Mtendaji wa kata ya Makongolosi Bi Nasra Mkupete Afisa Maendeleo ya jamii kata ya Mbugani wamesema kuwa uwepo wa kamati hiyo ya mikopo ngazi ya kata   utarahisisha kwa kiasi kikubwa ufwatiliaji wa marejesho ya mikopo hiyo lakini pia kuwepo kwa motisha kutaongeza chachu  katika ufuatiliaji na urejeshwaji wa  mikopo hiyo.

Kikao hicho cha kamati ya mikopo ngazi ya kata ni mwendelezo wa vikao vungine vitakavyokuwa vikifanyika mara kwa mara kwaajili ya kufanya tathimini juu ya utekelezaji wa majukum ya kamati hiyo sambamba na kufanya tathimini ya urejeshwaji wa mikopo ya aslimia kumi 10 inayotolewa kwa vikundi vya wanawake , vijana na watu wenye ulemavu pamoja na kuzipatia ufumbuzi changamoto mbalimbali zinzokuwa zimejitokeza wakati wa ufuatiliaji wa mikopo.

Kaim Mkurugenzi Wakili Athuman Bamba akizungumza na kamati ya mikopo ngazi ya kata juu ya mikakati ya ufuatiliaji wa marejesho ya mikopo ya asilimia 10 inayotolewa kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.

Mkuu wa idara ya Utawala akisisitiza juu ya matumizi ya vitendeakazi kwaajili ya kuhakikisha vikundi vinapata mikopo na mikopo hiyo inarejeshwa kwa wakati.

Mkuu wa kitengo cha ukaguzi wa ndani Ndugu Herberth Matungwa akiitaka kamati kusimamia urejeshwaji wa mikopo ya asilimia 10 kama inavyosimamiwa miradi mingine ya maendeleo wakati wa kikao cha kamati ya mikopo ngazi ya kata kilichoketi ukumbi wa Mwanginde.

Mtendaji wa kata ya Makongolosi Ndugu Egitho Bilali ambae ni mwenyekiti wa kamati ya mikopo ngazi ya kata  akichangia juu ya suala la kupata orodha ya vikundi na hali ya urejeshwaji wa mikopo mpaka sasa  pamoja na suala la motisha kwa wajumbe wa kamati hiyo

Wajumbe wa kamati ya mikopo ngazi ya kata wakiendelea kufuatilia agenda za kikao  katika ukumbi wa Mikutano wa Mwanginde Halmashauri ya Wilaya ya Chunya.


Matangazo

  • KUPIGA KURA YA RAIS KITUO AMBACHO HAUKUJIANDIKISHA September 15, 2025
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA KATA WATAKIWA KUSIMAMIA UREJESHWAJI WA MIKOPO..

    December 30, 2025
  • MHE MASACHE AUNGANA NA VIONGOZI WA DINI NA SERIKALI KUSISITIZA UWEPO WA AMANI.

    December 04, 2025
  • WATALAM NA MADIWANI WAASWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI.

    December 02, 2025
  • CHUNYA KUONGEZA NGUVU MAPAMBANO VVU

    December 01, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.