• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

RC HOMER; MKIKAMATA MTU ANATOROSHA TUMBAKU, TAIFISHENI HIYO TUMBAKU

Imewekwa: May 19th, 2024

Wakulima wa zao la Tumbaku Mkoa wa kitumbaku Chunya waaswa kutotorosha Tumbaku kwani watakaobainika kutorosha au kuweka uchafu kwenye Tumbaku watachukuliwa hatua kali za kisheria ikiwa ni pamoja na kufikishwa mahakamani sambamba na kutaifishiwa Tumbaku yao.

Kauli hiyo imetolewa Mwishoni mwa wiki iliyopita na Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera kwenye uzinduzi wa soko la tumbaku uliofanyika katika ghala la AMCOS ya kijiji cha Kalangali kata ya mtanila wilayani Chunya

 “Niwaombe vyombo vya ulinzi na usalama mtu anayeweka mawe kwenye Tumbaku, Mnyimeni dhamana, ni uhujumu uchumi. Hatuwezi tukaharibi taswira ya mkoa wa Mbeya na Songwe kwa kuweka mawe kwenye Tumbaku, Mkimkamata huyo mtu hakuna kumuonea huruma” Mhe Homera

Homera pia amemuagiza Mkuu wa wilaya ya Chunya kutaifisha Tumbaku itakayokamatwa ikitoroshwa kutoka Chama kimoja kwenda Chama Kingine au ikitoroshwa kwenda nje ya Mkoa wa Kitumbaku Chunya jambo ambalo halikubaliki kulingana na miongozo ya kilimo cha zao la Tumbaku

“Anaye torosha Tumbaku kupeleka kwenye chama kingine mkimkamata Mhe. Mkuu wa wilaya beba hiyo tumbaku inarudi kwenye chama alichotoka itaifishwe asilimia 70 wapate wenyewe kwenye chama na asilimia 30 iende Halmashauri” Homera

Homera amewataka wananchi kuhakikisha hawachanganyi tumbaku na vitu vingine kwani kufanya hivyo ni kujiharibia wao wenyewe, kitu ambacho kitapelekea makampuni kuondoka na kuacha kununua Tumbaku huku akiwaonya viongozi wa Vyama vya Msingi kuhakikisha Tumbaku haichanganywi na mawe kwani chama kitakachobainika kuruhusu wakulima wake Kuchanganya mawe chama hichi kitafutuiwa usajili.

 “Niwaambie ni chama ambacho kitapokea Tumbaku ya namna hiyo hicho chama tutakifuta, wanachama mtaenda kwenye vyama vingine, lazima na chama cha msingi muwe makini, huwezi mkaruhusu tumbaku iwekwe mawe” alisema Mhe. Homera

Kwa upande wa mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mbarak Alhaji Batenga ametoa rai kwa wakulima wa zao la Tumbaku kuendelea kuhifadhi mazingira na kuhakikisha wanapanda miti ili kukabiliana na uharibifu wa mazingira unaoambatana na kilimo cha zao la Tumbaku

“Zao hili la Tumbaku tumekuwa tukiendeleza kama takwimu ambavyo zinasema, yapo mambo ya msingi wakati tunazalisha na yenyewe tuyazingatie, Mhe Mkuu wa mkoa nimejipa jukumu la kusimamia swala la mazingira ili lisilete changamoto katika biashara yetu hii ya dhahabu ya kijani” Mhe Batenga

Hafla ya ufunguzi wa Msimu wa masoko ya Tumbaku katika mkoa wa kitumbaku Chunya imefanyika mwishoni mwa juma (Mei 17, 2024) katika ghala la AMCOS ya kijiji cha Kalangali kata ya mtanila wilayani Chunya ambapo Mkuu wa Mkoa wa Mbeya alikuwa Mgeni rasmi katika Hafla hiyo.

Mkuu wa mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Homera aliyevaa miwana, kushoto kwake ni mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe. Mbarak Batenga na kulia kwake ni Mwenyekiti wa Chama kikuu cha Ushirika CHUTCU Mhe. Sebastian Masika, akikata utepe kuashiria ufunguzi Rasmi wa Msimu wa soko la Tumbaku katika mkoa wa kitumbaku Chunya Hafla iliyofanyika katika ghala la AMCOS ya kijiji cha Kalangali kata ya mtanila 

Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma zuberi Homera akiandika aina ya Daraja katika belo la Mkulima wakati wa Ufunguzi wa Msimu wa Masoko ya Tumbaku 

Muonekano wa mitumba ya tumbaku katika Ghala la AMCOS ya kalangali

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.