• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MRADI WA TUHIFADHI MALIASILI WAZINDULIWA CHUNYA, TANZANIA.

Imewekwa: November 4th, 2023

Serikali na wadau mbalimbali wakiwa katika harakati za kukabiliana na tatizo la ushoroba nchini, Afisa mipango na uratibu wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Bi Janeth Mwaigoga kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji amewapokea wawakilishi wa mashirika ya TDFT, ADAP na TML (UPENDO HONEY) waliofika wilayani  humo, Tayari kwa kuanza kuendeleza Juhudi za kuokoa Ushoroba wa wanyama ulio hatarini kutokana na shughuli za kibinadamu zinazovamia maeneo hayo.


Akizungumza mapema November 3, 2023, katika Hafla ya kutambulisha mradi unaoitwa USAID/TUHIFADHI MALIASILI iliyofanyika katika ukumbi wa Omary City Hotel, amewataka wakuu wa Idara na vitengo kutoka Halmashauri ya wilaya ya Chunya kuhakikisha wanatoa ushirikiano wa kutosha kwa watendaji wa Mashirika hayo wakati wa utekelezaji wa mradi  huo, ili kufanikia lengo lililo kusudiwa katika mradi unaoanza utakelezaji wake hivi karibuni na unaofadhiriwa na watu wa Marekani (USAID).


“Wakuu wa Idara na Vitengo mlioalikwa kwenye shughuli hii na wale ambao mtatakiwa kushiriki moja kwa moja kwenye utekelezaji wa mradi huu kipindi chote cha mradi hakikisheni mnapatikana kwa wakati na mnatoa usaidizi unaotakiwa na kwa kufanya hivyo mtasaidia azma ya uwepo wa mradi”.


Wakati akiwasilisha mada ya namna shirika la TDFT litakavyo shiriki katika utekelezaji wa mradi, meneja mradi Ndugu Samson Mwakihaba amesema  Shirika la TDFT linalenga kuwafikia wananchi katika makundi mbalimbali wakiwepo vijana pamoja na wanafunzi ili kuhakikisha wanapata Elimu ya kutosha kuhusu uhifadhi wa ushoroba huo huku akiamini wananchi wanaweza kujihusisha na uharibifu wa mazingira ya ushoroba kutokana na kukosa ufahamu hivyo tumeomba ninyi viongozi wa serikali kwa mpate uelewa na pia mtaendeleza mradi baada ya sisi kumaliza muda wetu.


“Sisi tunaishia miaka miwili tu lakini tumewaita ninyi ili muulewe mradi kwa ujumla wake na pia muendeleze shughuli za mradi pindi sisi tutakapokuwa tumemaliza muda wetu wa kutekeleza mradi huu huku lengo la ninyi kuendleza shughuli za mradi huu likiwa ni kutimiza azma ya serikali la kuhakikisha tunahifadhi na kutunza mazingira kwa ujumla wake ikiwepo Mapitio ya wanyama" Amesema Ndg. Mwakihaba.


Kwa upande wa kampuni ya UPENDO HONEY wao katika mradi huu watajikita katika kuwajengea uwezo wananchi wanufaika wa mradi wa uzalishaji wa asali bora , kuhamasisha wanawake kushiriki katika zoezi la uzalishaji wa asali ikiwa ni sehemu ya kujiongezea kipato lakini pia kufanya mafunzo na mahusiano ya jamii na soko la asali maeneo mengine nje ya Tanzania lakini pia kutoa ufadhili kwa masomo yanayohusu Nyuki kwa wanafunzi sita katika Chuo cha Nyuki Tabora.


Wakati Shirika la ADAP watashiriki kwenye mradi kwa kuhakikisha Shoroba zinatambuliwa kwa kutoa hati miliki huku  wakihakikisha wananchi wanaoishi karibu na shoroba hizo wanapata hati miliki za aridhi zao ili kuzuia wao kujiongezea maeneo kwa upande wa shoroba,  watasimamia ukamilishaji wa mpango wa matumizi bora ya aridhi , wataimarisha ushiriki wa jamii katika kulinda Ikolojia na shughuli nyinginezo.


Mradi wa Tuhifadhi maliasili unafadhiliwa na watu wa Marekani, kwa wilaya ya Chunya utatekelezwa katika kata za Mafyeko, Kambikatoto, Mtanila, Lualaje na Matwiga ambapo vijiji saba vitanufaika na mradi huo na utadumu kwa miaka miwili kuanzia  mwaka huu 2023 na kutamatika mwaka 2025.

Bwana Mwakihaba meneja Mradi wa shirika la TDFT unaofadhiriwa na watu wa Marekani (USAID) akiwasili mada mbele ya viongozi na wadau mbalimbali wilayani Chunya wakati wa utambulisho wa Mradi wa Tuhifadhi Maliasili wilayani Chunya

Meneja mradi wa Shirika la ADAP ndugu Romanus Mwakimata akiwasilisha namna shirika la ADAP litakavyoshiriki katika mradi wa Tuhifadhi Maliasili unaotaraji kuanza kutekelezwa hivi karibu wilayani Chunya

Mkurugenzi mtendaji uzalishaji wa kampuni ya TML (UPENDO HONEY) BI Isabell Von Oerten akifafanua namna ambavyo kampuni hiyo itakavyoshiriki katika mradi wa Tuhifadhi Maliasili na namna ambavyo wananchi wa Chunya watafaidika kupitia Kampuni hiyo wakati wa utambulisho wa Mradi huo

Kaimu afisa Elimu awali na Msingi wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mw John Gwimile akichangia Jambo wakati wa utambulisho wa mradi wa Tuhifadhi Maliasili unafadhiriwa na USAID unataraji kutekelezwa kuanzia mwaka huu wilayani Chunya

Washiriki toka Taasisi za Serikali, taasisi binafsi na Asasi za kirai wakiwa wanaendelea kufuatilia utambulisho wa Mradi wa Tuhifadhi Maliasili unaotaraji kutekelezwa wilayani Chunya kuanzia mwaka huu, na anayewasilisha mbele ni meneja wa Mradi kutoka shirika la TDFT Ndugu Samson Mwakihaba

Washiriki waliohudhuria kutambulishwa kwa mradi wa Tuhifadhi Maliasili unaofadhiriwa na watu wa Marekani (USAID) wakiwa kwenye picha ya Pamoja baada ya kutamatika kwa zoezi la utambulisho wa Mradi huo

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.