• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

M/kiti H/shauri Chunya awataka madiwani, wataalam kushirikiana ukusanyaji mapato

Imewekwa: March 12th, 2022

MWENYEKITI wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, Mh. Bosco Mwanginde, amewataka Madiwani na wataalam wa Halmashauri kushirkiana katika ukusanyaji wa mapato.

 Mwanginde ameyasema hayo akifungua Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, robo ya pili kwa mwaka 2021/2022, uliofanyika Machi 11, 2022 na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali toka vyama vya siasa, vyombo vya ulinzi na usalama, wananchi pamoja na wakuu wa Idara na Vitengo.

Katika Mkutano huo, Mwanginde amesema, makusanyo ya Halmashauri yameongezeka kwa asilimia 23 kutoka asilimia 37 kwa kipindi kilichopita cha robo mwaka ukilinganisha na kipindi cha sasa cha robo mwaka.

“Makusanyo ya jumla ya Halmashauri kuanzia Julai hadi Desemba 2021 yameongezeka kwa kiasi kikubwa ukilinganisha na kipindi kilichopita cha robo ya pili kama hii tulikuwa na asilimia 37 lakini leo tuna zungumzia asilimia 60.” Alisema Mwanginde.

Aidha, Mwanginde alisema, hadi kufikia Desemba 2021, mapato ya Halmashauri yaliongezeka kwa asilimia 31 baada ya kukusanya bilioni 3.2 ambayo ni sawa na asilimia 68.

“Mapato yetu ya ndani hadi kufikia Desemba 2021 yamefikia shilingi bilioni 3.2 sawa na asilimia 68% ambapo ni takriban mara mbili ya makusanyo ya mwaka uliopita kwa kipindi kama hiki tulikuwa na asilimia 37%.”

Mh. Mwanginde alisisitiza kuongeza nguvu katika ukusanyaji wa mapato ili kuhakikisha Halmashauri inafikia malengo ya asilimia 100 ya ukusanyaji wa mapato.

“Pamoja na hayo tunahitaji sana kuongeza juhudi kwa maana kwamba tusibweteke kwa sababu tayari tupo katika nafasi nzuri, kikubwa tutambue bado hatujafikia asilimia 100, hivyo ni jukumu letu sasa kuongeza nguvu kwenye ukusanyaji.” Alisema Mh. Mwanginde

Kadhalika, aliwataka Madiwani kuhakikisha wanatoa ushirikiano kwa watendaji na viongozi mbalimbali wa Halmashauri pindi wanapopita katika maeneo yao kwa ajili ya kukusanya mapato.

“Sisi kama madiwani tuendelee kutoa ushirikiano kwa wataalam na watendaji mbalimbali wanapokuja kwenye maeneo yetu.”

Aidha, Baraza la Madiwani, limewataka wakala wa barabara za vijijini (TARURA) kuhakikisha barabara zote ambazo zipo kwenye matengenezo ziwe zimekamilika hadi kufikia mwisho wa mwezi huu.

“Tunawaagiza ndani ya mwezi huu, barabara tayari zina wakandarasi na wakandarasi wanasuasua, ziwe zimekamilika ili kuwaondolea kero wananchi hasa ikiwemo barabara ya Lualaje.” Alisema Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, Bosco Mwanginde.

Kadhalika, Baraza limewataka TARURA kuhakikisha wanabadilika na kufanya kazi kwa wakati ili kuweza kutatua changamoto ambazo zinawakumba wananchi pindi barabara zinapoharibika.

“Fedha hizi ni za Serikali, zinatakiwa zihudumie wananchi wa Chunya kwa wakati kama ambavyo zimekwenda kutengeneza madarasa ya UVIKO-19, kama ambavyo zimekwenda kutengeneza vituo vya afya na zahanati kwa wakati hata fedha za TARURA zinatakiwa ziende kwa wakati.

Hili ni onyo la mwisho kama mpaka mwezi mmoja hamjakamilisha barabara zote ambazo muda wake umeisha basi tutachukua hatua kama baraza la madiwani”. Alisisitiza Mh. Mwanginde

Waheshimiwa Madiwani  pamoja na wageni mbalimbali waliohudhuria, wakifuatilia  Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Chunya

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndg Tamim Kambona akizungumza wakati wa Mkutano wa Baraza la Madiwani

Waheshimiwa Madiwani wakiwa kwenye Mkutano wa Baraza la Madiwani la Halmashauri ya wilaya ya Chunya

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.