• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MKAITUMIE ELIMU YA ARDHI MNAYOIPATA KUWAELIMISHA WANANCHI.

Imewekwa: February 29th, 2024

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Mhe.Bosco Said Mwanginde amewataka wajumbe wa kikao cha wadau wa masuala ya ardhii kuhakikisha elimu wanayokuwa wameipata katika Mafunzo mbalimbali wanaitumia katika kuelimisha wananchi wengine kuhusu ardhi katika maeneo wanayotoka

Kauli hiyo ameitoa  tarehe 28 februari 2024 wakati akifungua kikao cha wadau wa ardhi kilicho andaliwa na taasisi ya MIICO inayotekeleza mradi wa Uendelezaji wa upatikanaji wa ardhi bora kwa wazalishaji wadogo Nyanda za juu kusini mwa Tanzania  ikiwemo Halmashauri  ya Wilaya ya Chunya katika kata ya Sangambi na Upendo kilichoketi katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya uliopo jengo jipya la utawala

“Kaitumieni elimu mnayoipata huko mnakokwenda na kwenye majukwaa yenu wajue nini mnakifanya,madiwani mliopo hapa kule mnakotoka kunakuwaga na migogoro ya masuala ya ardhi mkajitahidi kuelimisha watendaji wa kata na nyinyi pia mkasimamie haya mtakayoyapata huko kwenye maeneo yenu”alisema Mhe Mwanginde.

Glory Mdindile Afisa mradi kutoka MIICO akieleza malengo ya Mkutano pamoja na mpango kazi  wa taasisi hiyo amesema kuwa lengo kuu ni kutammbulisha mradi katika awamu ya nne ya utekelezaji lakini pia kushirikishana mipango kazi  na wadau  wengine kwenye masuala ya ardhi ikiwa ni pamoja na kujua shughuli  mbalimbali zinazofanywa na wadau  katika masuala ya ardhi.

Kaimu Mkurugenzi Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ndugu Athuman Bamba   ambaye ni mwanasheria wa Wilaya  ameishukuru taasisi ya MIICO kwa kuendelea kutoa elimu kwa wananchi juu ya masuala ya arhi katika Halmashauri ya Wilaya ya Chunya na kutoa rai kwa watendaji na wenyeviti wa vijiji wa maeneo husika kuhakikisha wanatoa ushirikiano kwa taasisi hiyo. 

 Afisa kilimo na Mifugo wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya ndugu Cuthbert Mwinuka ameeleza mipango mikakati iliyowekwa na Halmashauri katika kupambana na changamoto hizo ikiwa ni pamoja na kuanzisha mashamba ya lanchi kwaajili ya wafugaji lakini pia kuendelea kuwaelimisha wananchi kila mmoja kuheshimu mipaka yake kulingana na jinsi maeneo yalivyotengwa kupitia mpango wa matumizi bora ya ardhi

Faraja Kyando   mwakilishi wa wakulima Sangambi ,Reonald Manyesha Mwenyekiti wa wachimba madini Mkoa wa Mbeya  na Shangai Rapoy mwenyekiti wa Chama cha wafugaji Wilaya ya Chunya ni miongoni wa wadau waliowasilisha mambo mbalimbali wanazofanya pamoja na kueleza changamoto mbalimbali wanazo kabiliananazo katika masuala ya ardhi kubwa ikiwa ni  migogoro ya ardhi baina ya wafugaji , wakulima pamoja na wachimbaji wa madini katika maeneo  yao

Kikao hicho kimehusisha wadau mbalimbali wakiwemo  waheshimiwa madiwani wa maeneo unakotekelezwa mradi ,wadau wa azaki,wakulima na wafugaji, wachimbaji wa madini  wakuu wa idara mbalimbali ,watendaji kata na wenyeviti wa vijiji nakuazimia mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwaomba watu wa madini wasitoe lesseni mpaka wafike eneo husika na kujiridhisha kama halina Migogoro yoyote.

Gloria Mdindile Afisa mradi kutoka taasisi ya MIICO akiwasilisha malengo na mpangokazi  Shirika kwa awamu ya nne ya utekelezaji wa mradi kwa wadau walioshiriki kikao hicho kilichoketi katika Ukumbi wa Halmashauri ya

 Wilaya ya Chunya

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya  akitoa neno la Shukrani kwa Shirika la MIICO linalotekeleza mradi wa ardhi katika Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kwa kuendelea kutoa elimu kwa wananchi ambako mradi huo unatekelezwa

Afisa kilimo na Mifugo Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ndugu Cuthbert Mwinuka akielezea mikakati mbalimbali ya Halmashauri  katika kutatua changamoto mbalimbali juu ya wakulima nawakati wa kikao cha wadau wa MIICO kilicho keti katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri

Mwenyekiti wa wachimbaji madini Mkoa wa Mbeya ndugu Reonald Manyesha akichangia juu ya changamoto ya utaratibu unaotumika kutoa lesseni  unavyochangia migogoro ya ardhi kwenye kikao kilicho andaliwa natShirika la MIICO kilicho keti katika ukumbi wa Mikutano wa Halmashauri

Wadau mbalimbali  walioshiriki kikao kilichoandaliwa na Shirika la Miico  kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali kuhusu ardhi pamoja na kutambulisha mradi wa ardhi awamu ya nne ya utekelezaki  


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.