• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MINADA YA MIFUGO CHUNYA , FURSA KWA WAFUGAJI NA WAFANYABIASHARA.

Imewekwa: July 23rd, 2024

Wananchi wa Halmashauri ya  Wilaya ya Chunya wameendelea kunufaika na uwepo wa minada ya Mifugo iliyoboreshwa kwaajili ya biashara  ya kuuza na kununua mifugo  kwa bei inayoendana na mifugo hiyo lakini pia kumwezesha mnunuzi kununua  mifugo ambayo ni halali na imekaguliwa  ili kumlinda mlaji .

Ndugu Kinawanga Samhenda Mfugaji na ndugu Hamis Pauyole Mfanya biashara ya Nyama ya Ngombe mwamewashauri wafugaji wanaouza mifugo yao majumbambani kupeleka mifugo yao kwenye minada iliyotengwa na serikali kwani inawasaidia wao kama wafugaji kuuza mifugo yao kwa utaratibu na   kwa bei shindani kulingana na mifugo yao kwani wanaouza Mifugo yao majumbani wanauza kwa bei ndogo kwasababu ya kukosa ushindani wa soko.

Afisa mifugo wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya  Dkt Benedicto Matogo akizungumza na wandishi wa Habari  kwenye Mnada wa Mapogolo kata ya Chokaa  amesema kuwa  uwepo wa minada umesaidia kuwaleta  wafugaji pamoja, kuleta ushindani wa wanunuzi jambo ambalo humletea faida mfugaji lakini pia minada hiyo imerahisha ukusanyaji wa mapato yanayotkana na biashara hiyo ya mifugo

“Minada hii iliyoboreshwa imekuwa nguzo kubwa ya uchumi wa serikali , wafugaji pamoja na wafanyabiashara wa mifugo kwani imekuwa chanzo kikubwa cha mapato kwa Serikali , wafugaji na wafanyabiashara  minada imepelekea uwepo wa  soko lenye ushindani wa  bei  kutokana na ujio  wa wafanyabiashara wengi wanaotoka maeneo tofauti tofauti na kumwezesha  mfugaji  kuuza mifugo yake kwa bei inayoendana na thamani ya mfugo’’ alisema Dkt Matogo

Naye afisa biashara wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ndugu Lodrick Mwakisole ametoa wito kwa wanawake na vijana kuchangamkia fursa mbalimbali za kiuchumi  zinazopatikana katika maeneo ya Minada ya Mifugo ikiwa ni pamoja na kuuza na kununua mifugo, kuuza bidhaa mbalimbali kama vile  chakula vinywaji na biashara nyingine  kwani soko ni la uhakika kutokana na uwepo wa watu wengi wanaofika eneo la Mnada

‘’Kuna fursa kubwa kwa vijana na kinamama katika sekta ya mifugo kama unenepeshaji wa mifugo, vyakula vya mifugo lakini si hivyo tu kwenye eneo la mnada kuna biashara nyingine nyingi ambazo zinafanyika kama vile kuuza vyakula, nguo na biashara zingine’’ alisema Mwakisole

Mfugaji Kinawanga Samhenda na Mfanya biashara ya Nyama ya Ngombe ndugu Hamis Pauyole mwamewashauri wafugaji wanaouza mifugo yao majumbambani kupeleka mifugo yao kwenye minada iliyotengwa na serikali kwani inawasaidia wao kama wafugaji kuuza mifugo yao kwa utaratibu na   kwa bei shindani kulingana na mifugo yao kwani wanaouza  mifugo yao majumbani wanauza kwa bei ndogo kwasababu ya kukosa ushindani wa soko.

Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ina minada ya Mifugo miwili (2) iliyoboreshwa na Mnada wa Sipa na Mnada wa Mapogolo  pamoja na Minada midogo midogo 13   ambayo hufanyika kila mwezi mara moja   na  kuwawezesha wafugaji na wafanyabiashara kuuza na kununua mifugo pamoja na bidhaa mbalimbali ambazo huuzwa katika meeneo hayo ya Minada  ili kujipatia kipato na kukuza uchumi wa mtu mmoja mmoja na kukuza uchumi wa Taifa.

 Ndugu Kinawanga Samhenda Mfugaji kutoka kijiji cha Sangambi akiwa katika Mnada wa Mapogolo uliopo kata ya Chokaa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya  kwaajili ya kuuza Mifugo yake.

 Afisa Mifugo wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya Dkt Benedicto Matogo  akizungumza na wanahabari wakati wa Mnada wa Mifugo  uliofanyika katika Mnada wa Mapogolo kata ya Chokaa

Afisa biashara wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ndugu Lodrick Mwakisole akielezea fursa mbalimbali zinazopatikana kwenye Minada ya Mifugo wakati alipokuwa kwenye Mnada wa Mifugo wa Mapogolo uliopo kata ya Chokaa.


Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.