• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MHE. BATENGA: TWENDENI TUKAHANGAIKE NA SHIDA ZA WANANCHI.

Imewekwa: March 4th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mhe. Mbaraka Alhaji Batenga amewataka watumishi wa umma kuacha kufanya kazi kwa mazoea na badala yake kushughulika na shida za wananchi kwa kuzingatia haki, usawa na utawala bora ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma bora na stahiki.

Mhe. Batenga ameyasema hayo leo Machi 4, 2025 wakati akizindua mafunzo ya siku ya moja ya elimu ya uraia na utawala bora yaliyofanyika katika ukumbi wa Mwanginde Hall uliopo Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, jengo jipya na yaliyoendeshwa na Wizara ya Katiba na Sheria ikiwa ni sehemu ya jitihada za serikali kuboresha utendaji kazi na utawala bora kwa watumishi wa umma nchini.

“Wananchi wana kero zao na ndio shida zao, twendeni tukahangaike na shida za wananchi kwasababu utendaji kazi wa serikali upo katika ngazi ya Wilaya kuanzia kwenye Tarafa, Kata, Kijiji, Kitongoji na mitaa na ndipo wananchi walipo” amesema Mhe. Batenga.

Aidha, Mhe. Batenga amesema, wenyeviti wa vijiji, vitongoji anaweza wakafanya wananchi wakaipenda au wakaichukia serikali kwasababu viongozi hao wanakutana na wananchi mara kwa mara hivyo ni muhimu viongozi hao kufahamu majukumu na nafasi walizonazo kiutendaji.

“Wiki moja baada ya uchaguzi wa serikali za mitaa, mimi niliwaita watendaji wa kata, vijiji, wenyeviti wa vijiji, wenyeviti wa vitongoji pamoja na wajumbe wote wa serikali za vijiji kuwapa semina elekezi ya mafunzo ya uongozi ili kujua namna ya kwenda kuwahudumia wananchi na kujenga uhalali wa serikali kukubalika kuanzia ngazi za chini” amesema Mhe. Batenga.

Mhe. Batenga amewasisitiza washiriki wa mafunzo hayo kutoa haki kwa wakati kwakuwa uelewa wa wananchi umeongezeka katika kutambua haki zao. Ameongeza kuwa, wananchi wanazijua na kuzidai haki zao, hivyo, viongozi wasisubiri wananchi wadai haki zao, wananchi wakidai haki zao hiyo haki inakuwa imecheleweshwa na haki iliyocheleweshwa ni haki iliyonyimwa.

“Naomba niwaahidi kuwa, watumishi wangu ni waaminifu na wataenda kutekeleza majukumu yao kulingana na mafunzo waliyoyapata kupitia Wizara ya Katiba na Sheria” amesema Mhe. Batenga.

Naye, Wakili wa serikali na mratibu wa mafunzo ya elimu ya uraia na utawala bora kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Wakili Prosper Alexander Kisinini amesema lengo la mafunzo ya elimu ya uraia na utawala bora ni kuwajengea uwezo viongozi na watendaji ili kuweza kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

“Huu ni mwanzo wa kujenga nchi salama kupitia kuongeza uzingatiaji wa masuala ya haki, ulinzi na usalama Wizara ya Katiba na Sheria ina matumaini makubwa na mafanikio ya mafunzo haya” amesema Wakili Kisinini.

Winnie Michael, Mtendaji wa Kata ya Bwawani, Wilaya ya Chunya amewashukuru wawezesehshaji wa mafunzo ya uraia na utawala bora huku akiahidi kwenda kutekeleza kwa vitendo ili kuwahudumia wananchi wa Kata ya Bwawani.

Mafunzo ya siku moja ya elimu ya uraia na utawala bora yametolewa na Wizara ya Katiba na Sheria kwa wataalamu mbalimbali wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya wakiwemo watendaji wa kata, maafisa ardhi, maafisa ustawi wa jamii, maafisa maendeleo ya jamii na kuhudhuriwa na viongozi wa ulinzi na usalama Wilaya ya Chunya.

Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mhe. Mbaraka Batenga akiwa kwenye picha ya pamoja na wakufunzi kutoka Wizara ya Katiba na Sheria pamoja na washiriki wa mafunzo ya elimu ya uraia na utawala bora kutoka Wilaya ya Chunya katika Ukumbi wa Mwanginde uliopo jengo jipya la Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, leo Machi 4, 2025.

Afisa Uchaguzi, Tume ya Haki za binadamu na utawala bora, ndugu Paul Sulle akiwasilisha mada ya demokrasia na Utawala Bora kwa washiriki wa mafunzo ya elimu ya uraia na utawala bora katika ukumbi wa Mwanginde uliopo Halmashauri ya Wilaya ya Chunya.

Washiriki wakisikiliza kwa makini mada mbalimbali zilizowasilishwa kwenye mafunzo ya elimu ya uraia na utawala bora katika ukumbi wa Mwanginde uliopo Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, jengo jipya.

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.