• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

Madiwani Chunya wapitisha 27.9bn/- bajeti 2022/2023

Imewekwa: January 21st, 2022

PICHANI: Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya Chunya Mh. Bosco Mwanginde Akifungua Kikao Cha Baraza la Madiwani


Baraza la Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Chunya limepitisha rasimu ya mpango na bajeti kwa mwaka 2022/2023, kwenye kikao kilichofanyika leo Januari 21, 2022 katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri.

Baraza hilo limepitisha rasimu ya bajeti yenye makisio yenye thamani ya shilingi bilioni 27,972,230,500.00 (bilioni) katika bajeti hiyo.

Mishahara kwenye bajeti hiyo imepangwa kuwa Sh.12,687,309,000,00, kiasi cha Sh. 11,190,782,900,00 kitaenda kwenye miradi ya maendeleo na mapato ya ndani ya Halmashauri yakiwa Sh. 1, 576,120,400.00.

Matumizi mengineyo ni Sh.4, 094, 138, 600, 00 na kufanya rasimu hiyo ya mpango na bajeti kwa mwaka 2022/2023 kuwa na jumla kuu ya Sh.bilioni 27,972,230,500.00.

Kwa upande mwingine, Madiwani hao wamewapongeza wataalamu wa Halmashauri kwa uandaaji mzuri wa bajeti hiyo ya 2022/2023 na kukiri kwamba bajeti hiyo ina mambo mengi mazuri kwa maendeleo ya wananchi.

Madiwani hao wameshauri pia Halmashauri hiyo kuendelea kuongeza nguvu na kubuni vyanzo vipya vya mapato ambavyo vitaisaidia Halmashauri kuweza kupata mapato kwa wingi, hatimaye kuweza kutekeleza vyema bajeti zinazopangwa na Halmashauri hiyo.

Mbunge wa jimbo la Lupa, Mh. Masache Njelu Kasaka amempongeza Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kwa kuongoza na kuendesha vyema kikao cha Baraza la Madiwani na kupitisha rasimu ya bajeti kwa mwaka wa 2022/2023.

“Bajeti tuliyoipitisha hapa ndio mwelekeo wa Chunya ipi tunayoitaka, Mwenyekiti, Mkurugenzi pamoja na wataalamu kupitishwa kwa bajeti hii maana yake sasa jukumu kubwa linabaki mikononi mwenu, ikiwa ni usimamizi na utekelezaji”. Alisema Mh Masache.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Chunya, Mh. Mayeka Simon Mayeka, ameupongeza uongozi wa Halmashauri pamoja na Baraza la Madiwani kwa ukusanyaji mzuri wa mapato.

“Nakumbukwa mwaka uliopita kipindi kama hiki tulikuwa nyuma sana, lakini kwa hatua hii niliyoiona nawapongeza sana, kwa namna tunavyoenda nadhani tutakuwa na makusanyo mazuri na kuweza kupindukia asilimia zaidi ya 100”. Alisema Mh Mayeka.

Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, Bw. Tamim Kambona, amewashukuru waheshimiwa madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kwa ushirikiano wanaompa yeye pamoja na watendaji wengine wa Halmashauri.

"Sisi kama watendaji wa Halmashauri tutahakikisha tunatekeleza yale yote ambayo ninyi mnatarajia yafanyike kwenye maeneo yenu.

“Mwenyekiti niwahakikishie madiwani sisi tutapeleka miradi kwenye kata zote bila kupendelea kata nyingine yoyote ile”. Alisema Kambona.

Akifunga kikao hicho, Mwenyekiti wa Halmashauri, Mh.Bosco Mwanginde ambaye pia ni Diwani wa Kata ya Mbugani, amesema kuwa bajeti hiyo ili iweze kutekelezwa kama ilivyopangwa inategemea ukusanyaji bora wa mapato kwa Halmashauri.



Afisa Mipango Wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Bi Janeth Mwaigoga Akiwasilisha Rasimu ya Bajeti kwa Mwaka 2022/2023 katika baraza la Madiwani

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Bw Tamim Kambona akizungumza kwenye kikao cha Baraza la Madiwani wakati wa Kujadili rasimu ya Bajeti ya mwaka 2022/2023

Mh Mayeka Simon Mayeka Akizungumza kwenye Baraza la Madiwani wakati ya Kujadili Rasimu ya Bajeti kwa Mwaka 2022/2023

Mbunge wa Jimbo la Lupa Mh Masache Njelu Akizungumza kwenye kikako cha Baraza la Madiwani wakati wa kujadili Rasimu ya Bajeti kwa mwaka 2022/2023

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.