• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MAANDALIZI KUZIKABILI MVUA ZILIZOTABIRIWA YAANZA CHUNYA

Imewekwa: October 30th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka S Mayeka amewataka wananchi wa wilaya ya Chunya kuanza kuchukua tahadhari mbalimbali ili kukabiliana na majanga yanayoweza kujitokeza kutokana na mvua zinazoweza kunyesha msimu huu kama wataalam wa Mamlaka ya Hali ya hewa Nchi walivyotahadharisha uwepo wa Mvua kubwa katika Msimu wa Mvua unaotarajiwa kuanza hivi karibu.


Ametoa rai hiyo leo tarehe 30/10/2023 maeneo  ya kijiji cha Lola na kijiji cha Upendo vilivyo kata ya Upendo wakati alipofanya mikutano na wananchi ikiwa ni sehemu ya ziara ya kawaida ya kusikiliza kero za wananchi, kuzitatua na zile zitakazoshindikana  kwa wakati huo kuzitafutia suluhu yake kupitia viongozi mbalimbali wanaohusika.


“Kutokana na maelekezo ya wataalam wa Hali ya hewa nchini inawezekana tukapata Mvua nyingi kuliko kiwango tulichozoea hivyo naomba tujiandae kwanza kutunza chakula cha kutosha ili kukabiliana na changamoto zinazoweza kujitokeza kutokana na mvua hizo, pili tujiandae kuwa na Mbegu zinazoweza kustahimili maji mengi lakini pia tuandae maeneo yanayoweza kutumika yatakapotokea mafuriko katika maeneo yetu”.


Aidha Mkuu wa wilaya ya Chunya ametaka serikali za vijiji kuanza kutenga maeneo ya kutosha kujenga miundombinu mbalimbali ya kijamii kama vile shule, vituo vya afya, vituo vya polisi na miundombinu mingine tofauti na ilivyo sasa ambapo serikali za vijiji hawana ardhi matokeo yake kila mradi unapokuja serikali inaanza kuomba maeneo kwa wananchi jambo hili halikubariki kabisa.


“Anzeni sasa kutenga maeneo au kuomba ardhi karibu na zahanati hii maana Lola inakuwa, watu wanaongezeka mtahitaji kujenga kituo cha afya hivyo eneo zaidi litatakiwa. Hii tabia ya kuwaomba wananchi aridhi kila wakati serikali inapotaka kujenga miundombinu ni jambo ambalo haliwezekani ni lazima serikali za vijiji muanze kuwa na benki za aridhi” aliongeza Mhe Mayeka.


Akitoa salamu za wananchi wa kata ya Upendo Diwani wa kata hiyo Mhe Richard N. Itelekelo amemshukuru Mhe Rais kwa kuendelea kumwamini Mkuu wa wilaya ya Chunya na kuendelea kumuacha aendelee kuwepo wilaya ya Chunya lakini pia ameshukuru kuwapa fedha Milioni 50 katika kijiji cha Lola ili wajenge zahanati ambayo itawapunguzia wananchi umbali wa kutembea kufuata huduma za afya.


Ziara hiyo ya Mkuu wa wilaya na kamati ya usalama imedumu kwa siku moja, Pamoja na kero mbalimbali za wananchi katika kata ya Upendo kupatiwa majibu Mkuu wa wilaya ametembelea Zahanati ya kijiji cha Lola ambayo imepelekewa fedha shilingi milioni Hamsini na serikali kwaajili ya kuikamilisha, lakini pia ametembelea shule ya sekondari ya kata ya Upendo inayojengwa katika kata hiyo lengo likiwa ni kuhakikisha wananchi wa upendo wanapata huduma bora wakiwa kwenye mweneo yao.

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka (anaye andika) akinukuu kero zinazowasilishwa na wananchi katika kijiji cha Lola mapema leo

Mkuu wa wilaya ya Chunya (aliyesimama na amenyoosha mkono) akijibu kero za wananchi katika kijiji cha Lola wakati alipofanya zaiara ya kusikiliza kero za wananchi na kuzipatia majibu

Mkuu wa wilaya ya Chunya akizungumza na wananchi waliojitokeza baada ya kukagua ujenzi wa Zahanati inayojengwa Lola

 Mkuu wa wilaya (aliyenyoosha mkono wake wa kulia) akioneshwa mipaka ya Shule ya sekondari Upendo(aliyenyoosha mkono wake wa kushoto Diwani wa kata ya Upendo)

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.