• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

MAADHIMISHO YA SIKU YA SHERIA NCHINI KATIKA WILAYA YA CHUNYA.

Imewekwa: February 3rd, 2018

MGENI RASMI KATIKA MAADHIMISHO YA SIKU YA SHERIA MH. MKUU WA WILAYA YA CHUNYA BI.REHEMA MADUSA MWENYE KOTI LA BLUU (katikati), HAKIMU MFAWIDHI WA MAHAKAMA YA WILAYA NDG. OSMUND NGATUNGA (kushoto kwake), AKIWA KWENYE PICHA YA PAMOJA NA WANASHERIA, MAWAKILI NA WADAU MBALIMBALI WA SHERIA.

Chunya.

Siku ya Sheria Nchini Tanzania iliadhimishwa kiwilaya tar. 1/2/2018 ikiwa ni kilele cha maadhimisho ya wiki ya sheria

Nchini..

Shughuli mbalimbali zilifanyika katika wiki hiyo ikiwa ni Pamoja na kutoa Elimu ya sheria kwa Wananchi walioko maeneo

(kata) mbalimbali ya wilaya ya Chunya.


Katika maadhimisho hayo mgeni rasmi alikuwa ni Mkuu wa Wilaya ya Chunya Mh. Rehema Madusa aliyeambatana na kamati ya

Uilnzi na Usalama, Pamoja na Viongozi wa Dini.


Kauli Mbiu katika Maadhisho hayo ilikua ni "Matumizi ya TEHAMA katika utoaji haki kwa wakati na kwa kuzingatia Maadili"


Mada mbalimbali ziliwasilishwa na Wataalam mbalimbali wa Sheria ambapo kwa kuanzia Mwendesha Mashtaka katika Wilaya ya

Chunya Ndg.Raymond Lukomwa, alitoa salamu zake kwa kusisitiza kuwa Mahakama ni Chombo kinachosimamia Haki. Hivyo

aliwasisitizia Wananchi kupeleka Malalamiko yao Polisi na Uchunguzi unapokua umekamilika Malalamiko hayo hupelekwa

Mahakamani kwa ajili ya uendeshaji wa Kesi.


Mwanasheria katika H/W Chunya Ndg.Egito Bilali aliwasilisha Mada juu ya Ndoa. na kueleza kuwa ndoa ni Taasisi ya mwanzo na

ya zamani zaidi kwa mujibu wa Vitabu vya Dini, na ni Muungano wa hiari kati ya mwanaume na Mwanamke kwa muda wote watakao

kuwa Duniani.

katika kuelezea aina za ndoa zilizopo kisheria alisema ni pamoja na Ndoa ya Mme mmoja na Mke mmoja(kwa wakristo), Mme na wake

wengi(kwa waislamu), Ndoa ya kiserikali(ni Jukumu la Wahusika kuamua.) na Pamoja ile ya kimila ambayo ni ya Wake Wengi.

Pia aliendelea kutanabaisha kuwa Uchumba wenye masharti pindi utakapovunjika basi huambatana na fidia, na Mahali hutoka kwa Mwanaume

kwenda kwa Mwanamke na ndoa ambayo haijalipiwa mahali ni batili na zaidi mahali si kigezo cha kuhalalisha ndoa.

   Alisema kuwa Ndoa batili ni ile ambayo imefungwa lakini Sheria Haiitambui. alisema kuwa mwanamke mwenye umri Mdogo kama miaka 15

anaweza kuolewa ila kwa ridhaa ya wazazi/walezi.


aliendelea kueleza kuwa ndoa batili ni ile iliyofungwa kati ya watu wenye Undugu wa damu, kama mmoja wa wenye ndoa hakuwa

hiari, Wahusika hawakuwepo wakati wa ufungishaji wa ndoa, kwa Mkristo kwenda kufunga ndoa ya pili, Mtu asiye sahihi

kufungisha ndoa(Mfungishaji lazima awe na leseni), Ndoa ikifungwa katika kipindi cha Eda, na pia lazima ndoa iwe na

mashahidi.


Aidha Mwanasheria aliendelea kuweka wazi juu ya wakati gani ndoa inakuwa batilifu(halali ila inakasoro). Wakati mmoja wa

Wanandoa kukosa uwezo wa kutimiza tendo la ndoa, katika kipindi cha Uchumba hukugundua kuwa mwenza wako ni mgonjwa wa

akili, ukigundua kuwa mwenza wako anaugonjwa wa zinaa, kama mmoja wa wanandoa hajafikisha miaka 18 hasa mwanamke,

mmoja wa wanandoa anagoma kutimiza tendo la ndoa.

Aidha alimaliza kwa kusistiza kuwa mwanamke anayohaki ya kumiliki mali binafsi, na Talaka ni halali kama ndoa

hairekebishiki na Jukumu la kutunza familia ni la Baba.


Mbali na wataalam mbalimbali kuwasilisha Mada zao pia Mh.Hakimu Mkazi Mfawidhi wa wilaya ya Chunya Ndg. Osmund Ngatunga
alipata fursa ya kuhutubia  na kugusia mambo mbalimbali ikiwemo Tehama na umuhimu wake, Jukumu la utoaji Haki, Faida ya matumizi
 ya TEHAMA kama njia ya kuimarisha ubora wa utoaji haki,  Changamoto, Mikakati na Mipango ya baadaye ya mahakama.

Mh. Hakimu mfawidhi alianza kwa kuitambulisha kauli mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ambayo ni:-
 “Matumizi ya TEHAMA katika utoaji haki kwa wakati na kwa kuzingatia Maadili”

Alizidi kueleza kuwa, Kwa maneno mengine kauli mbiu ina lengo la kutuonyesha matumizi ya TEHAMA katika utoaji huduma za jamii, hasa utoaji haki

na kuimarisha uwazi na maadili.

 TEHAMA ni nini? Ni Teknolojia ya Habari na Mawasiliano. Kihistoria, dhana hii imegawanyika katika makundi mawili ambayo

ni analogia na digitali.

Analogia ni upashanaji habari isiyotumia vifaa vya kielekitroniki kama typewriter, posta, mkono kwa mkono, matumizi ya

karatasi, mafaili ya kawaida n. k.

Digitali ni upashanaji wa habari kwa kutumia vifaa vya mawasiliano, na mifumo mtandao au program, (kielekitroniki) ili  

kugawana habari kupitia tovuti (www.judiciary.go.tz), barua pepe (info@judiciary.go.tz), faksi, video confencing, simu

(smart phones), scanner, mitandao ya kijamii kama facebook, whatsapp, twiter, instagram, blogs, you tube n.k.


Mahakama Maboresho kupitia Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025, Mkataba wa Huduma kwa Mteja 2002 na Mpango Mkakati wa Mahakama

2015-2020 inakusudia pamoja na mambo mengine kutumia TEHAMA katika kuboresha misingi ya utawala bora, amani na utulivu,

uthabiti na umoja wa kitaifa ili kuchochea maendeleo ili kufikia lengo lake la kuwa na Mahakama iliyokaribu na inayofikiwa

na wananchi katika kutoa huduma za utoaji haki Nchini.  


2.Jukumu la Utoaji Haki.

Kama vilivyo vyombo vingine vya dola ambavyo vimekasimiwa mamlaka ya Kikatiba ya utendaji (Utawala), uwakilishi, kutunga

sheria na kuisimamia Serikali (Bunge) Mahakama imepewa jukumu la Kikatiba na kisheria la utoaji haki. Ina mamlaka yenye

“kauli ya mwisho” ya utoaji haki kwa wananchi kwa mujibu wa Ibara ya 4, 107A, 107B ya Katiba yetu.  

Kwa mujibu wa Ibara ya 107B ya Katiba ya Nchi, Mahakama inapaswa ilinde uhuru, haki, hadhi na mamlaka ya Kikatiba dhidi ya

mihimili mingine ya dola na wananchi. Dhana ya uhuru wa Mahakama imejikita hasa katika mambo ya ki-utawala, fedha na

utendaji wake hasa wakati shauri linaposikilizwa na kuamuliwa bila kuathili ibara ya 8 na 146 ya Katiba ya Nchi.

 TEHAMA ina lengo, pamoja na mambo mengine, kuharakisha upatikanaji wa huduma mbalimbali zitolewazo na Mahakama ili

kukidhi Dira yake isemayo “Haki sawa kwa wote na kwa wakati”. Mbali na kutumia TEHAMA pia tumekusudia kutumia Mahakama

itakayotembea yaani kuna gari maalum litakalotumika kufika sehemu mbalimbali ndani ya Wilaya yetu ili kwenda kusikiliza

mashauri na kutoa elimu. Mahakimu, watunza kumbukumbu na Katibu Muhtasi watakao tekeleza jukumu hili katika eneo letu

wameshateuliwa.  

TEHAMA itafanikisha kurekodi ushahidi, umalizikaji mashauri haraka, mazingira mazuri ya utendaji kazi, kupata huduma za

mahakama bila urasimu, kupata nakala za mwenendo na uamuzi wa Mahakama kwa wakati.

Ni imani ya Mahakama kwamba endapo TEHAMA itatumika kama ilivyokusudiwa itasaidia kuondoa misemo ya wanazuoni isemayo

“haki siyo tu itendeke bali ionekane imetendeka”, pia “haki iliyocheleweshwa ni haki iliyonyimwa” lakini vilevile “haki

iliyoburuzwa ni haki iliyozikwa”.  


kwa hotuba kamili ya Mh. Hakimu Mfawidhi bonyeza hapa.    HOTUBA YA HAKIMU MKAZI MFAWIDHI -2018.pdf



Akiongea na hadhira ya wananchi walihudhuria maadhimisho ya siku hiyo ya sheria Mkurugenzi Mtendaji wa H/W Chunya Bi.

Sophia kumbuli alianza kwa kuwapongeza wananchi walijitokeza kwa wingi kuhudhuria Hafla hiyo na kusistiza kuwa ule

utaratibu wa kusikiliza kero za wananchi kila siku za Alhamisi utaendelea na kuwasihi wananchi kuja kupewa ushauri wa

kisheria hasa kuhusu ardhi.


Pia Katibu tawala wa wilaya Bi. Mahija Nyembo aliwashukuru wananchi kwa kufika kwa wingi na kwamba kero zao zote

wanazoziwasilisha na watakazo ziwasilisha zitafanyiwa kazi, pia hakusita kuwasisitiza wapite kwanza kwenye ngazi za chini

za maamuzi kama kata, tarafa kabla ya kufika kwenye ngazi ya wilaya na kwamba kero zao ziwe za kweli.


      Naye Mgeni rasmi katika Hafla hiyo ambaye ni Mkuu wa wilaya ya Chunya Bi. Rehema Madusa alianza kwa kuwapongeza

wananchi wote kwa kuuona Mwaka Mpya, na kumshukuru Mungu kuweza kuwalinda wote. na kueleza kuwa wananchi wengi

wanachangamoto ya kisheria na kwamba Mabaraza ya Kata bado hayajaweza kuwafikia wananchi Wengi kwa sababu mbalimbali, 

aliipongeza serikali kwa kusimamia uendeshaji wa kesi kwa haraka na wakati, akiwasihi wananchi kutowaogopa mahakimu na

wanasheria, na aliwaeleza wananchi waende ili kupewa msaada wa kisheria. Mh.Mkuu wa wilaya alisisitiza kuwa masuala ya

Mimba kwa wanafunzi si ya kujadili nje ya mahakama na kwamba mashauri hayo yapelekwe mahakamani na sheria ichukue mkondo

wake kwa wahusika, na kurudia kusisitiza tamko la Raisi kuwa binti atakayepewa ujauzito hastahili kurudi shuleni hivyo anapaswa kulindwa.

Alitumia Fursa hiyo kuwakaribisha Mawakili wa kujitegema, Maafisa Takukuru na vyombo vinginevyo kuja kuungana naye kila siku ya

Alhamisi ili kusikiliza kero za Wananchi.

aliendelea kuwasihi viongozi wa Dini juu ya kuwakumbusha Wananchi masuala mbalimbali ya kiusalama, na kusema mambo mengi

yanaanzia chini kwa Wananchi, hivyo Elimu jamii itolewe kwa Wananchi, na kusisitiza ni lazima kurekebisha vyombo

vinavyosimamia haki za Wananchi,

akiongelea suala la maadili aliwasisitiza wananchi kutotekwa na tabia za umagharibi na kwamba watanzania tunapaswa

kuheshimu maadili yetu.

Pia hakusita kuwasisitiza Wananchi juu ya kujenga nyumba bora ikiwemo na zile za wageni yaani Guest Houses kwani Wilaya ya

Chunya inatarajia kuja kuwa na wageni wengi hapo baadaye ikiwemo wawekezaji.  Kwa kumalizia aliwaasa wananchi kuzingatia

masuala ya ulinzi na Usalama, na uhifadhi wa mazingira. Pia hakusita kumshukuru Hakimu mfawidhi wa Wilaya na kumsihi

wajipange katika miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa jengo la mahakama.


katika Hafla hiyo wananchi wengi walipata fursa ya kuuliza maswali mengi yanayohusiana na sheria na kupatiwa majibu kutoka kwa

Wataalam Mbalimbali wa Sheria waliokuwepo.


                                                                                                     
MGENI RASMI MKUU WA WILAYA YA CHUNYA AKIWA NA VIONGOZI WA DINI, HAKIMU MFAWIDHI, KATIBU TAWALA NA MWANASHERIA WA H/W.

                                                                           

                                                                         HAKIMU MFAWIDHI AKIWA NA WADAU MBALIMBALI WA SHERIA 

                                                                           

                                                                         HAKIMU MFAWIDHI AKIWA NA WAWAKILISHI WA CHAMA TAWALA

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.