• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

KILIMO CHA TUMBAKU KIPO KWA MUJIBU WA SHERIA ZA BUNGE.

Imewekwa: March 11th, 2025

Mwenyekiti wa wadau wa Tumbaku ambaye pia ni Afisa kilimo wa Wilaya ya Chunya ndugu Cuthberth Mwinuka  amewataka wakulima wa zao la Tumbaku kulima zao hilo kwa kufuata taratibu, miongozo na kanuni za zao hilo ili kupata zao bora kwani kwa kuto kuzingatia taratibu na miongozo iliyowekwa ni kinyume cha Sheria .

Ameyasema  hayo mapema  tarehe 10/03/2025 wakati wa kikao cha mrejesho wa tathimini ya zao la tumbaku kwa msimu wa kilimo wa 2024/2025 kilichoketi katika  ukumbi wa mikutano wa kampuni ya  Mkwawa  kwa lengo la kuhitimisha zoezi la tathimini ya zao lililodumu Zaidi ya siku 18.

“Nimeshawaelekea kwamba kilimo cha Tumbaku kipo kwa mujibu wa sheria za bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kina miongozo pamoja na adhabu kwa mtu anaye kiuka miongozo hiyo ikiwa ni pamoja na faini, au kifungo au vyote kwa pamoja, hivyo kwa wale wote wanaoacha mabua wakayatoe, maotea  nayo wakayatoe kwasababu yanaathiri uzito wa tumbaku na wale wanaoacha mbegu ni kinyume cha sheria kwasababu kila mwaka mkulima anatakiwa kupanda mbegu mpya zinazotolewa na makampuni ili kupata zao bora”amesema Mwinuka

Aidha Mwinuka amesisitiza kwa viongozi wa vyama vya ushirika waliohudhuria kikao  hicho kuhakikisha wanakwenda kuwaeleza wakulima yale yote yaliyoelezwa katika kikao hicho lakini pia kwenda kuyafanyia kazi ili yaweze kuleta tija katika kupunguza changamoto mbalimbali zilizojitokeza  lakini pia kuleta tija katika zao hilo la kibiashara.

Naye Mkurugenzi wa zao la Tumbaku  bodi ya Tumbaku Tanzania  ndugu Nicholaus Mauya   ametoa rai kwa viongozi wa vyama vya ushirika kuwasimamia wakulima kuhakikisha wanalinda na kulithamini kila jani katika mmea ili kuongeza tija ya zao la tumbaku na kumwezesha mkulima kupata kipato ikiwa ni pamoja na kuwasisitiza wakulima kuvuna kuanzia jani la chini hadi jani la juu kwasababu  kila jani la zao hilo ni pesa.

 “Sisi kama viongozi lazima tuoneshe mfano wa kuvuna majani ya chini  lakini pia viongozi na maafisa ugani mkawasaidie wakulima kuhakikisha wanazingatia kanuni bora za kilimo cha tumbaku ili kuhakikisha tunaboresha kilimo cha tumbaku na kuongeza tija ili kuendana na hali halisi.”amesema Mauya

Meneja mkuu CHUTCU ndugu Juma Nshinshi  amewataka viongozi wa vyama vya ushirika kusimamia vyama vyao kama ambavyo wameaminiwa na wanachama ikiwa ni pamoja na umakini katika kusimamia mali ya chama lakini pia  viongozi wahakikishe mnawasisitiza  wakulima kufunga tumbaku mapema ili masoko yaweze kufanyika mapema.

Boniface Richard kutoka Global Leaf Tanzania Limited, Godfrey Gobbo  kutoka kampuni ya Mkwawa wakiwakilisha kampuni zingine za  Tumbaku wametoa msisitizo mkubwa kwa viongozi wa vyama vya ushirika  kuwa na makadirio yanayoendana na uhalisia lakini pia kuendelea kuwaelimisha wakulima wao juu ya changamoto zilizojitokeza wakati wa tathimini  ili kuondkana na kasi ya upotevu wa jani na kuongeza pato la mkulima kwani kila jani katika mche lina thamani yake.

Kikao cha mrejesho wa tathimini ya zao  kimetokana na tathimini iliyofanyika kwa majuma mawili kwa wilaya ya Chunya na Wilaya ya Songwe na  kuhusisha wadau  mbalimbali wa tumbaku ikiwa ni pamoja na Makampuni ya tumbaku,  Bodi ya Tumbaku Tanzania, wataalamu kutoka Halmashauri , chama kikuu cha ushirika na wadau wa taasisi za fedha na kujadili mambo mbalimbali yalioonekana wakati wa tathimini ya zao ili kuboresha uzalishaji wa zao hilo na kuongeza tija ya zao hilo

Mwenyekiti wa wadadu wa Tumbaku ndugu Cuthberth Mwinuka akizungumza na wadau kujadili mambo mbalimbali yaliyoonekana wakati wa tathimini ya zao  wakati wa kikao cha mrejesho wa tahimini ya zao kwa mwaka 2024/2025 ili  kuendelea kuboresha na kuongeza tija ya zao.

Mkurugenzi wa zao la tumbaku ndugu Nicholaus Mauya akitoa rai kwa viongozi wa vyama vya ushirika na wakulima wa tumbaku juu ya uchumaji wa kila jani katika mche ili kuongeza kipato cha mkulima.

Viongozi wa vyama vya ushirika na wadau wa Tumbaku wakifuatilia na kutoa mikakati yao katika kikao cha mrejesho wa tathimini ya zao kwa mwaka 2024/2025 kilicichoketi katika ukumbi wa Mikutano wa  kampuni ya Mkwawa  

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.