• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

KAMATI ZA UJENZI ZATAMBULIWA CHUNYA: MWENYEKITI ATUMA OMBI POLISI

Imewekwa: January 15th, 2026

Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya imetambua mchango wa kamati za ujenzi katiika miradi ya Maendeleo inayojengwa katika Halmashauri ya wilaya ya Chunya huku akiwashukuru kwa juhudi kubwa wanayofanya katika usimamizi wa Miradi hiyo

Akizungumza wakati wa ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Shule Mpya ya awali na Msingi inayojengwa kwenye eneo la Shule ya Sekondari Sangambi Jana 14.1.2026 Mwenyekiti amesema wanastahili pongezi sana

“Naomba niwapongeze sana Viongozi wa Sangambi hasa wale wote waliojitambulisha kama wanakamati wa Kamati za Ujenzi, tunawapongeza sana kwa usimamizi mzuri wa miradi ya Maendeleo inayotekelezwa kwenye maeneo yenu, Niwaombe muendelee kuwa na moyo huu hata wakati wa utekelezaji wa miradi mingine”Alisema Mhe. Nshinshi

Aidha Mhe. Nshinshi amewaomba Jeshi la Polisi hasa kituo cha Polisi Sangambi kuendelea kutoa Elimu kwa wananchi wa kata ya Sangambi katika nyanja mbalimbali ikiwepo Matumizi ya Vyomba vya moto, kwani wananchi hao wanategemea sana vyombo hivyo katika shughuli zao za kila siku za kujitafutia kipato ili kujikimu na familia zao

“Niwapongeze kwa ujenzi na kukamilisha kituo cha Polisi Sangambi na hatimaye Kimefunguliwa, lakini sasa naomba niwaombe wanaohusika kuendelea kuwaelimisha wananchi wa Kata hii juu ya matumizi sahihi ya Vyombo vya Moto jambo litakalofanya wananchi kuipenda huduma inayotolewa na kituo hicho” aliongeza Mhe Nshinshi

Awali akitoa taarifa za utekelezaji wa mradi huo Mtendaji wa kata ya Sangambi Bi Sarah Emmanuel amesema, Kata hiyo ilipokea shilingi milioni mia tatu ishirini na tisa na laki tano (329,500,000/=) kutoka Serikali kuu ili kutekeleza mradi huo huku akisema mpaka sasa ujenzi unaendelea vizuri kwa kushirikiana vyema na wananchi wa kata ya Sangambi kwa Ujumla wake

Diwani wa kata ya Sangambi Mhe Junjulu Ndete Muhewa wakati wa salamu zake za ukaribisho alisema Kata ya Sangambi haina mchezo katika usimamizi wa miradi ya Serikali, kwani utekelezaji wa miradi huwa shirikishi na wazi kwa wananchi wote jambo linalopelekea miradi inayotekelezwa katika kata hiyo kuwa bora zaidi

Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango imefanya ziara ya siku mbili, ni ziara ya kwanza tangu kuundwa kwa kamati mbalimbaliza Baraza la madiwani jambo linaloendelea kuashiria kuanza rasmi kwa shughuli mbalimbali za Baraza la madiwani katika Halmashauri ya wilaya ya Chunya na katika ziara yao wamepongeza na kushauri pale inapobidi

Bi Sarah Emmanuel Mtendaji wa Kata ya Sangambi akisoma taarifa ya utekelezaji wa Mradi wa ujenzi wa Shule ya awali na msingi inayojengwa katika kata ya sangambi mbele ya Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya

Mhe Junjulu Ndete Muhewa Diowani wa kata ya Sangambi akitoa salamu za wananchi wa kata ya Sangambi kwa kamati ya Fedha, Utawala na Mipango wakati ilipotembelea mradi wa ujenzi wa Shule ya Awali na Msingi inayojengwa kwenye eneo la Shule ya Sekondari Sangambi

Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe Kelvin Nshinshi (Aliyeshika Karatasi) akiongoza Kamati ya Fedha, Utawala na Mipango ya Halmashauri ya wilaya ya Chunya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Shule ya Awali na Msingi inayojengwa Sangambi

Matangazo

  • KUPIGA KURA YA RAIS KITUO AMBACHO HAUKUJIANDIKISHA September 15, 2025
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • KAMATI ZA UJENZI ZATAMBULIWA CHUNYA: MWENYEKITI ATUMA OMBI POLISI

    January 15, 2026
  • MKAWE MABALOZI WA MFUMO WA SIS KWA WALIMU WENGINE.

    January 14, 2026
  • TUMIENI VYOMBO VYA HABARI NA NJIA NYINGINE KUTOA ELIMU YA BIMA YA AFYA KWA WANANCHI.

    January 07, 2026
  • KAMATI YA MIKOPO NGAZI YA KATA WATAKIWA KUSIMAMIA UREJESHWAJI WA MIKOPO..

    December 30, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.