• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

Kamati ya kudumu ya Bunge, utawala yakagua miradi ya maendeleo Chunya

Imewekwa: March 15th, 2022

WAJUMBE wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Machi 14, 2022 wamefanya ziara ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo katika Halmashauri ya Wilaya ya Chunya.

Miradi iliyotembelewa na kamati hiyo ni pamoja na mradi wa ujenzi kituo cha afya cha Sangambi unaokadiriwa kutumia kiasi cha shilingi milioni 600, ambapo mapato ya ndani yalioyofanikisha mradi huo ni shilingi milioni 500 huku nguvu kazi za wananchi ikiwa ni shilingi milioni 100.

Kamati hiyo pia ilitembelea ujenzi wa soko la madini unaotarajiwa kugharimu zaidi ya shilingi milioni 497,430,119 ikiwa ni mapato ya ndani ya Halmashauri.

Akizungumza baada ya kukagua na kuridhishwa na utekelezaji wa miradi hiyo, Mwenyekiti wa kamati ya kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa Mhe. Abdallah Chaurembo ametoa pongezi kwa uongozi kwa kazi nzuri ya utekelezaji wa ujenzi wa miradi.

“Tumetembelea kituo hiki cha afya, kizuri ujenzi wake unaendelea vizuri, tunawapongeza sana, lakini kituo hiki pamoja na kasi nzuri inayokwenda kwenye ujenzi tumeona ‘material’ (malighafi) yapo ya kutosha tunaamini kitaisha kwa wakati.” Alisema Chaurembo.

Chaurembo alisema kuwa, matumaini yake kwenye bajeti itakayopitishwa wiki ijayo, fedha zitatengwa kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya kituo cha afya ikiwa ni mkakati wa kuhakikisha huduma za afya zinapatikanan kwa uhakika.

“Tunatarajia kwenye bajeti tunayokwenda kuijadili wiki ijayo tutaona fedha zimetengwa kwa ajili ya vifaa vya kituo hiki cha afya.” Alisema Chaurembo.

“Haitopendeza kituo hiki kimejengwa kwa gharama kubwa, wananchi wamejitolea na kamati ya Bunge na Mheshimiwa Mbunge amesisitiza tuje hapa, halafu tukaona kituo kinabaki majengo bila ya kutoa huduma.” Alionya Chaurembo.

Aidha, Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa wamemuagiza Meneja wa TARURA Mkoa kuhakikisha wanafanya matengenezo ya barabara ya Sangambi.

“Kutokana na umuhimu wa eneo hili Meneja wa TARURA tufanye kila inavyowezekana barabara hii iweze kufanyiwa matengenezo.

Tumeona uwekezaji mkubwa uliofanyika hapa halafu bila kuwa na barabara madhubuti ya kufika huku kituo hiki kinaweza kuwa kipo halafu hakifanyi kazi, sasa Meneja wa TARURA hili jambo mlichukulie umuhimu unaostahili.” Alisisitiza Chaurembo.

Kadhalika, Chaurembo ameupongeza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya kwa kuaandaa taarifa nzuri.

“Nimepitia taarifa ya Halmashauri ya Wilaya ya Chunya, nimeipitia kwa kina ambapo imeonesha mambo mengi humu ndani, naomba taarifa hii tuisome kwa kina na ikiwezekana Halmashauri nyingine zote pamoja na maelekezo tuliyoyasema yafanywe kama taarifa hii ilivyoandaliwa.”

Kwa upande wa Waziri wa Inchi Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na Serikali za Mitaa {TAMISEMI} Mhe. Innocent Bashungwa amewapongeza wananchi wa kata ya Sangambi kwa kuchangia nguvu kazi zao katika ujenzi wa miradi ya maendeleo.

“Pamoja na jitihada nzuri za Mweshimiwa Rais Samia Suluhu na Serikali ya Awamu ya Sita anayoiongoza, nimefurahi kuona wananchi hapa hamjabweteka bado mnachangia shughuli za maendeleo.” Alisema Bashungwa.

Pia, Bashungwa ameutaka uongozi wa Mkoa kuzisimamia Halmashauri zote ili kuhakikisha matumizi ya fedha yanakuwa vizuri na kunakuwa na uwazi kwenye utumiaji wa fedha hizo.

“Ninachokielekeza hapa kwa Mkurugenzi na Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa lisimamie hili kwenye halmashauri zote, fedha za Serikali zinazokuja kwenye maendeleo na zile fedha ambazo zinachangwa na wananchi kwa mapenzi yao kuchangia maendeleo kunakuwa na uwazi na uwajibikaji katika matumizi yake.” Alisema Mh. Bashungwa.

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ua Utawala na Serikali za Mitaa wakipokea maeleozo ya Ujenzi wa Maradi wa Soko la Midini Unaotekelezwa na Halmashauri ya wilaya ya Chunya kupitia mapato ya Ndani

wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa wakitembelea na Kukagua ujenzi wa kituo cha Afya cha Sangambi kilichopo kata ya Sangambi kinacho jengwa kwa Mapato wa Ndani

Muonekano wa Jengo la Wagonjwa wa Nje {OPD}

Ujenzi wa Jengo la Mama na Mtoto pamoja na Wodi ya Wazazi, Kituo cha Afya Sangambi

Muonekano wa Soko la Madini linalijengwa na Halmashauri ya wilaya ya Chunya kupitia mapato ya Ndani

Muonekano wa Ndani Soko la Madini

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.