• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango yaridhishwa na Utekelezaji wa Miradi ya maendeleo Chunya

Imewekwa: April 21st, 2022

WAJUMBE wa Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango wamefanya ziara ya kutembelea na kukagua ujenzi wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Halmashauri ya Wilaya ya Chunya katika kipindi cha robo ya tatu.

Miradi iliyotembelewa na kamati hiyo ni ujenzi wa Vituo vya Afya vya Kambikatoo, Mafyeko, na Ifumbo pamoja na ujenzi wa Zahanati ya Lyeselo na Igangwe.

Pia kamati ilitembelea na kukagua ujenzi wa majengo manne katika Hospitali ya Wilaya, ujenzi wa jengo la Bohari ya Dawa, ujenzi wa Jengo la Upasuaji pamoja na ujenzi wa Wodi ya Wanawake na Wanaume.

Akiongoza wajumbe wa Kamati hiyo Mheshimiwa Bosco Mwanginde ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ameupongeza uongozi wa Halmashauri kwa usimamizi mzuri wa miradi inayotekelezwa Wilayani Chunya.

“Mimi binafsi na kwa niaba ya wajumbe wenzangu niwapongeze kwa hatua mliyofikia, mara ya kwanza nilikuja hapa nikakuta pori lakini leo tunaona mpo hatua nzuri za ukamilishaji.

“Nampongeza Mkurugenzi wetu na wataalamu wake kwa ufuatiliaji wao kwenye ujenzi wa miradi ndani ya Halmashauri yetu nawaomba waongeze bidii ili miradi yote ikamilike kwa wakati na kuleta tija kwa wananchi wetu.” Alisema Mwanginde.

Kwa upande wake, Diwani wa Kata ya Lualaje ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango, Mheshimiwa Tusalimu Mwaijande ameipongeza Ofisi ya Mkurugenzi kwa jitihada wanazozifanya hadi sasa za kupeleka maendeleo kwa wananchi.

“Niipongeze Ofisi ya Mkurugenzi kwa namna ambavyo wanakimbiza hii miradi kwa ujumla, wataalam wetu wanafanya kazi nzuri sana kufuatilia miradi hii na kuhakikisha fedha iliyopelekwa kwenye mradi inafanya kazi iliyokusudiwa.” Alisema Mwaijande.

Aidha, kamati pamoja na kutoa pongezi na kuridhishwa na mwenendo wa miradi ya maendeleo wameagiza miradi yote ya maendeleo kukamilika kwa wakati ili ilete tija na maendeleo kwa wananchi huku ikisimamiwa katika ubora stahiki na kwa weledi mkubwa.

 Wajumbe wa Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango wakikagua Ujenzi wa Kituo cha Afya Ifumbo

 

Wajumbe wa Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango ya Halmashauri ya Wilaya ya Chunya Wakitembelea na Kukagua Ujenzi wa Jengo la Utawala

Muonekano wa Jengo la Utawala

Wajumbe wa Kamati ya Fedha Uongozi na Mipango wakikagua ujenzi wa Nyumba ya Wtumishi 3 in 1 katika kituo cha Afya cha Kambikatoto

Muonekano wa nyumba ya Watumishi ya 3 in 1 Katika kituo cha afya cha Kambkatoto

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.