• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DKT MWAKAJUMILO “WALIMU NI LAZIMA TUJITAFAKARI”.

Imewekwa: May 27th, 2023

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Mbeya Dkt Stephen Mwakajumilo amewataka wakuu wa shule za sekondari Mkoa wa Mbeya kujitafakari kama wanatimiza wajibu wao ipasavyo kwani walimu ni msingi imara na muhimu wa Maendeleo ya Taifa lolote Duniani

Dkt Mwakajumilo ametoa kauli hiyo leo tarehe 26/5/2023 kwenye kikao cha wakuu wa Shule Mkoa wa Mbeya (TAHOSA) kilichoketi katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya (Sapanjo) chenye lengo la kukumbushana, kuhimizana na kubadirisha uzoefu na ujuzi ili kuleta ufanisi wa wakuu wa shule katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku kwenye maeneo ya kazi

“Elimu mliyopata miaka ya nyuma haitoshi lazima muingie mifukoni ili kuitafuta Elimu itakayowafanya mpambane na maendeleo ya sayansi na teknolojia tuliyonayo sasa na muungane muwe kitu kimoja na muiambie serikali changamoto zetu ili kunusuru kizazi cha sasa maana bila walimu hakuna Taifa. Msikubali Elimu zenu zioze, bali zifanyieni kazi, hakikisheni mnatafuta maarifa mengine ili kuweza kutatua changamoto zinazoambatana na maendeleo ya sayansi na Teknolojia” Mwakajumilo

Akijibu hoja ya walimu kutaka siku za kumfukuza Mwanafunzi mtoro zipunguzwe Dkt Mwakajumilo amewataka walimu kuwa karibu na wanafunzi ili kutambua changamoto zao mapema kwani sio wote wanaoshindwa kufika shule kwasababu ya utoro tu bali ni changamoto mbalimbali

“Usikubali kumpoteza mwanafunzi wako, usikubali kumfanya mwanafunzi wako kuwa adui, bali mfanye awe rafiki yako ili aendelee kupenda masomo wakati wote na hii inaweza kusaidia hata kupunguza utoro wa wanafunzi shuleni” amesema Mwakajumilo

Awali akisoma Risala kwa Mgeni rasmi Mwenyekiti wa wakuu wa shule za sekondari Mkoa wa Mbeya Mwalim Francis J. Mwakihaba ameomba kupunguzwa kwa siku za kumfukuza mwanafunzi mtoro shuleni kutoka siku tisini (90) na kufikia thelasini (30) ili walimu waweze kukomesha suala la utoro kwa wanafunzi

“Sisi wakuu wa shule tunaomba idadi za siku za mwanafunzi mtoro kufukuzwa shule zipunguzwe kuto tisini (90) kama ilivyo sasa na kufikia siku thelesini (30) jambo ambalo litapelekea walimu wakuu na uongozi wa shule kuwaondoa wanafunzi watoro kwa wakati ili kuleta ufanisi na ufaulu katika masomo, kwani kuna wanafunzi wanakuwa watoro kwa siku themanini (80) na baadaye anaruhusiwa kufanya mitihani wakati hajafanya maandalizi” Mwl. Mwakihaba

Akitoa shukrani kwa mgeni rasmi Mwalimu Mulla O. Njeje pamoja na kumshukuru mgeni rasmi kufika wilaya ya Chunya pia amemuhakikishia kwamba ujumbe alioutoa umefika eneo sahihi na pia kwa niaba ya walimu wakuu  wote Mkoa wa Mbeya, Mwalimu Njeje amemuhakikishia Mgeni Rasmi kwamba ujumbe alioutoa utawafikia walimu wote

“Mimi naamini haya uliyotupatia tutayapeleka kwa walimu wenzetu na hata yale yanayohitaji utekelezaji tutayatekeleza ipasavyo hivyo maneno yako yamefika maeneo sahihi kabisa” amesema Mwl. Njeje

 Kikao hiki ni kiako cha kawadaida na Kimefanyika wilayani Chunya ikiwa ni utaratibu wa kawaida wa vikao hivyo kukaa kwa kubadirishana wilaya moja hadi nyingine zilizopo Mkoani Mbeya hivyo kwa sasa ilikuwa ni nafasi ya wilaya ya Chunya.

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.