• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DKT KILUSWA “HAKUNA SABABU YA KUTOROSHA MADINI”

Imewekwa: March 15th, 2023

Naibu waziri wa Madini Dkt Steven Kiluswa amewataka wachimbaji wanaotorosha madini kuacha mara moja kwani kutorosha madini ni kukosa uzalendo kwa nchi yako ili hali sekta ya madini imeboreshwa kwa kiwango kikubwa kwani masoko ya madini yameanzishwa nchini na vituo vya kununulia dhahau vinapatikana karibu kila kona

Mhe. Kiluswa amesema hayo leo tarehe 15/03/2023 alipokuwa anazungumza katika hafla ya ufunguzi wa maonesho ya teknolojia ya madini yanayofanyika katika mkoa wa kimadini Chunya, maonesho hayo yanafanyika katika viwanja vya Sinjilili ambapo taasisi mbalimbali binafsi na serikali zinashiriki pamoja na wachimbaji wadogo na wakubwa kutoka katika mkoa wa kimadini Chunya na hata nje ya mkoa huo

“Serikali imeweza kuanzisha masoko 52 ya madini, vituo 92 vya ununuzi wa madini na uwepo wa masoko haya umepunguza utoroshaji wa madini. Watoroshaji wa madini acheni kutorosha madini kwana hamna sababu ya kufanya hivyo maana masoko yapo na kuendelea kufanya hivyo ni kukosa uzalendo, na serikali iko macho kuhakikisha madini hayaendelei kutoroshwa” amesema Dkt Kiluswa

Aidha Dkt Kiluswa ameshauri mkoa wa kimadini Chunya Kuendelea kuwa na maonesho kama haya kwani yana mchango mkubwa sana katika kufungua fursa mbalimbali katika maeneo ya uchimbaji na Nyanja nyingine za kiuchumi kwani huwakutanisha wachimbaji, brokers, Dealers na wadau wengine wengi ambao huduma zao zinafanikisha mchakato wote wa uchimbaji

“Muwe na siku ya madini angalau kwa kila mwaka ambapo teknolojia mbalimbali zinaoneshwa hapo ili kuendelea kufungua fursa mbalimbali za uwekezaji kwani hata kupitia maonesho haya wako watu watakuja kuwekeza chunya kwani fursa hizo wameziona kupitia maonesho haya. Kongamano kama hili litatuwezesha kuwakutanisha wachimbaji wa madini kutoka maeneo mbalimbali, brokers, dealers na watoa huduma mbalimbali zinazohitajika katika mchakato wa uchimbaji”

Awali wakati Mgeni Rasmi anatembelea mabadna mbalimbali ya wadau waliojitokeza, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Mhe. Juma Zuberi Homera ameziomba taasisi za kifedha kupunguza Riba kwa wachimbaji angalau kufikia asilimia kumi na moja ili kuendelea kuwarahisishia katika shughuli zao tofauti na ilivyosasa ambapo wachimbaji hukopeshwa kwa riba ya asilimia ishirini

“Riba naomba mshushe angalau mpaka asilimia kumi na moja ili angalau waweze kujikwamua na hii imekuwa changamoto kubwa kwao, riba hii ikifika asilimia kumi na moja mimi nitafarijika sana” alisema Homera

Sekta ya madini kwa sasa inachangaia asilimia 9.7 katika pato la Taifa ambapo Ilani Ya Uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ikielekeza ifikapo 2025 sekta ya madini ifikishe asimilia kumi (10%) katika pato la Taifa huku ajira zinazozalishwa kutoka na sekta ya madini nchini mpaka sasa ni Milioni nane

Maonesho ya kwanza ya teknolojia ya Madini na fursa za uwekezaji mkoani Mbeya yamefunguliwa rasmi leo terehe 15 march na Naibu waziri wa madini Dkt Steven Kiluswa katika viwanja vya Chunya kati vilivyopo kata ya Itewe kijiji cha Sinjilili wilayani Chunya ambapo kauli mbiu ya maonesho hayo ikiwa ni “Uongezaji wa thamani na Madini kwa maendeleo ya Taifa”. Maonesho hayo yatadumu mpaka tarehe 17/3/2023.

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.