• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DED CHUNYA APONGEZA WANANCHI UTEKELEZAJI MIRADI YA TASAF

Imewekwa: July 16th, 2025

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Tamim Kambona amewataka wananchi wa Chunya hasa walengwa wa TASAF kuendelea kuibua miradi yenye tija na manufaa kwao na Jamii kwa ujumla huku akiwataka kuendelea kujituma katika kufanya kazi zao za kujipatia kipato ili kuwa na maisha bora.

Ametoa kauli hiyo mapema leo 16.07.2025 wakati alipotembelea miradi mbalimbali iliyoibuliwa na walengwa wa TASAF ili kutatua baadhi ya changamoto zinazoikumba jamii ya eneo fulani ambapo amesema kupitia miradi hiyo ufumbuzi wa changamoto mbalimbali umepatikana kupitia miradi hiyo.

“Kwanza kabisa hongereni kwa miradi hii mnayoendelea kutekeleza, tumepita baadhi ya maeneo wamefungua barabara, wengine miradi ya maji na hatimaye na ninyi hapa mna mradi wa visima vya maji, Napongeza sana, Muendelee kushirikiana na Serikali kuibua Miradi yenye tija na yenye manufaa kwenu na Jamii kwa ujumla” Amesema Kambona.

Aidha, Kambona amempongeza Mratibu wa TASAF Halmashauri ya wilaya ya Chunya pamoja na timu nzima kwa usimamizi, bidii na kujituma kwao katika kufuatilia utekelezaji wa miradi hiyo huku akisema utekelezaji mzuri wa miradi unatokana na usimamizi mzuri.

Mratibu wa TASAF Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu David Ngowo amesema walengwa wa TASAF katika Halmashauri ya wilaya ya Chunya wamekuwa wakiibua miradi wao wenyewe na wakiitekeleza jambo linalosaidia kuondoa baadhi ya changamoto katika maeneo yao huku akirejerea maeneo ambayo hayakuwa na barabara kupitia TASAF barabara zimepatikana, maeneo ambayo hayakuwa na maji sasa kupitia TASAF mmepata maji changamoto nyinginezo.

Mhandisi wa Halmashauri ya Chunya Eng. Sophia Mgaya na Afisa Mipango na uratibu walioongoza na Mkurugenzi kwenye ziara hiyo wametoa ushauri maeneo mbalimbali ili wananchi wa Chunya waendelee kutekeleza miradi yao kwa viwango stahiki ili iweze kudumu kwa muda mrefu na iendelee kuwasaidia wananchi kwa muda mrefu zaidi.

Miradi iliyotembelewa leo ni mradi wa ujenzi wa Barabara kijiji cha Mbugani, Mapogoro, Makongolosi, kijiji cha Upendo, Lola, Mtande na Mamba huku mradi wa maji Gepu, na mradi wa Lambo la maji Makongolosi unaounganisha na upandaji wa miti kuzunguka lambo la maji.

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Chunya Ndugu Tamim Kambona (Aliyevaa Tisheti Nyeupe Katikati na amenyoosha mkono) akitembelea mradi wa Barabara ilifunguliwa na Walengwa wa TASAF kijiji cha Mbugani, Kulia kwake ni Mratibu wa TASAF Chunya na Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa Kijiji cha Mbugani

Mkurugenzi mtendaji (Mwenye tisheti Nyeupe) akipokea taarifa ya utekelezaji wa Mradi wa lambo la maji Makongolosi, Mradi huo umeambatana na upandaji wa miti kuzunguka lambo hilo

Mkurugenzi mtendaji akipokea taarifa ya uchimaji wa kisima cha maji Gepu uliotekelezwa na walengwa wa TASAF ili kuondoa changamoto ya upatikanaji wa maji katika eneo hilo

Mratibu wa TASAF wilaya ya Chunya Ndugu David Ngowo (Aliye nyoosha mkono wenye makaratasi) akifafanua jambo kwa Mkurugenzi mtendaji wakati wa ukaguzi wa mradi wa Barabara katika kijiji cha Lola kilichopo kata ya Upendo

Matangazo

  • TANGAZO LA KAZI TOKA TUME HURU YA TAIFA YA UCHAGUZI July 03, 2025
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • DED CHUNYA APONGEZA WANANCHI UTEKELEZAJI MIRADI YA TASAF

    July 16, 2025
  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA.

    July 10, 2025
  • LENGO LA KUFUTA DARAJA LA TATU KWENYE MITIHANI LA TAIFA LINAFIKIWA CHUNYA

    July 08, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI

    July 03, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.