• Malalamiko |
    • wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Chunya District Council
Chunya District Council

jamhuri ya muungano wa Tanzania Ofisi ya Raisi na Tawala za mikoa na serikali za mitaa Halmashauri ya wilaya ya Chunya

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhamira na Dira
    • muundo wa Taasisi
    • Misingi Mikuu
  • Utawala
    • Mipaka ya Kiutawala
    • Idara
      • Utumishim na Utawala
      • Mipango,ufuatiliaji na Takwimu
      • Afya
      • Fedha na Biashara
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Maji
      • Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ardhi na Maliasili
      • Maendeleo ya Jamii
      • Ujenzi
      • Usafi na Mazingira
    • Vitengo
      • Sheria
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Manunuzi na Ugavi
      • Uchaguzi
      • Ufugaji Nyuki
      • Tehama
  • Fursa za Uwekezaji
    • Vivutio vya Utalii
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Madini
  • Huduma zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma ya Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Uvuvi
  • Madiwani
    • Orodha ya waheshimiwa Madiwani
    • Kamati za kudumu
      • Fedha, Utawala, Mipango
      • Afya, Elimu, Maji
      • Maadili
      • Ukimwi
      • Uchumi, Ujenzi na Mazingira
    • Ratiba
      • Ratiba ya vikao
      • Mwenyekiti kuonana na Wananchi
  • Miradi
    • Miradi Itakayotekelezwa
    • Miradi ambayo haijakamilika
    • Miradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Utaratibu wa kufuata
    • Ripoti
    • Sheria
    • fomu za maombi
  • kituo cha habari
    • taarifa kwa vyombo vya habari
    • Video
    • Hotuba mbali mbali
    • Maktaba ya picha
    • matukio mbali mbali
    • Habari

DC MAYEKA” WATOTO WASITUMIE VITU VYA KIELEKITRONIKI BILA USIMAMIZI WA WALEZI/WAZAZI”

Imewekwa: June 17th, 2023

Mkuu wa wilaya ya Chunya Mhe Mayeka S. Mayeka akimwakilisha Mkuu wa mkoa wa Mbeya amewataka Maafisa maendeleo ya jamii halmashauri zote za mkoa wa Mbeya pamoja na jamii kwa ujumla kuhakikisha wanawalinda watoto kwa kuwazuia kutumia vitu vya kielekitroniki bila usimamizi wa walezi au wazazi jambo ambalo litapelekea kuwalinda watoto hao na ukatili mbalimbali unaojitokeza katika jamii ya sasa.

Mhe. Mayeka amesema hayo leo tarehe 16/6/2023 alipomuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mbeya katika kilele cha Maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika ambayo imeadhimishwa kimkoa wilayani Chunya  katika viwanja vya shule ya Msingi Makongolosi iliyopo kata ya Bwawani Mamlaka ya Mji mdogo Makongolosi

“Nawaagiza Maafisa Maendeleo ya Jamii katika Halmashauri zote kuhakikisha wanatoa Elimu kwa wazazi na walezi ili watambue haki za mtoto ili kumpatia malezi yanayofaa. Na wazazi hakikisheni mnawazuia watoto kutumia vitu vya kielekitroniki kama vile simu, televisheni, intaneti na nyinginezo bila usimamizi wa wazazi au walezi amesema Mhe. Mayeka

Aidha Mhe. Mayeka amesema ukatili wa kijinsia bado ni tatizo katia mkoa wa Mbeya huku ubakaji ukiongoza kuwa na kesi nyingi hivyo amewataka wananchi wote kujitokeza kutoa taarifa mbalimbali za ukatili pamoja na kutoa ushahidi mahakamani pindi watuhumiwa wa unyanayasaji wa kijinsia wanapokuwa wamekamatwa ili kuhakikisha sheria inawatia hatia na kupewa adhabu stahiki

Ushahidi imekuwa changamoto kubwa sana mahakamani kwani sisi wananchi huwa hatujitokezi kutoa ushahidi pale tunapotakiwa kufanya hivyo, Niwaombe mjitokeze kutoa ushahidi pale mtapotakiwa kufanya hivyo kwani nje ya hapo maana yake mahakama inawaacha huru watuhumiwa wa ukatili wa kijinsia kwakukosa ushahidi

Awali akimkaribisha Mkuu wa wilaya ya Chunya, Katibu tawala wa wilaya ya hiyo Ndugu Anakleth Michombero amewataka wananchi waliojitokeza katika madhimisho hayo kuhakikisha wanawalea watoto wao ili watakapofika umri wa utu uzima waoneshe nidhamu na mwenendo mwema kama walivyolelewa

“Mlee mtoto katika njia impasayo, hataiacha hata akiwa mzee, hivyo kujua kama mtoto alilelewa vizuri au vibaya akiwa mtoto ni katika utu uzima wake ndipo itajulikana, Hivyo naomba tuwalee watoto katika maadili mema wawapo wadogo ili watakapokuwa wenye umri wa utu uzima waoneshe maadili mema waliyolelewa walipokuwa wadogo

Afisa Maendeleo ya Jamii wilaya ya Chunya Ndugu Vincent Msolla kwa Niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wilaya ya Chunya amesema kama halmashauri wataendelea kuhakikisha mtoto yuko salama na anapata mahitaji yote  muhimu katika maisha yake, Lakini pia amewataka wananchi wilaya ya chunya kuendelea kulipia kodi ili serikali ikusanye mapato ambayo baadaye yanarudi kujenga miradi mbalimbali kama ambavyo shule mpya ya msingi inayojengwa katika kata ya Makongolosi

“Tuna kazi ya kuhakikisha mtoto yuko salama na anapata mahitaji yote muhimu katiia maisha yake ya kawaida na hatimaye kutimiza ndoto za maisha yake. Lakini pia wananchi naomba tuendelee kutoa kodi kwa mujibu wa sheria ili tuendelee kuongoza katika ukusanyaji wa Mapato, kujitoa kwenye shughuli mbalimbali za maendeleo ili tuendelee kuungana na serikali yetu kutuletea maendeleo kama ambayo serikali imeona vema kutujengea shule mpya ya msingi katika kata ya Makongolosi”

Meneja wa Kanda Mkwawa Leaf Tobacco L.T.D ndugu Chrispine Mchafu amesema kampuni ya Mkwawa inaunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya sita Inayoongozwa na Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan katika kupambana na ukatili kwa watoto ambapo mwezi wa saba kampuni itaanzisha kampeni maalumu ya kupinga utumishwaji wa wototo kwenye mashamba ya Tumbaku maana kuna ukatili mkubwa katika shughuli hizo

Sisi Kampuni ya Mkwawa Leaf Tobacco tuko bega kwa began a serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kuanzia mwezi wa saba tunataraji kuanzisha Kampeni Maalumu ya kupinga utumikishwaji wa watoto kwenye mashamba ya Tumbaku tunayoyasimamia kwani katika uzalishaji wa Tumbaku kuna unyanyasaji mkubwa wa watoto hususani katika mchakato wa kukausha zao la Tumbaku amesema Mchafu

Naye Meneja miradi wa Child Support Mbeya Hildergade Megrab ametoa ombi maalumu kwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuboresha mazingira ya shule ya msingi Makongolosi ili iwape nafasi watoto wenye mahitaji maalumu kupata huduma kwa urahisi kuliko ilivyo sasa kwani watoto wenye uhitaji maalumu wapo zaidi ya 25 katika shule hiyo lakina miundombinu sio rafiki kwao

Naomba kuleta ombi binafsi kwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwamba irekebishe miundombinu ya Shule ya Msingi Makongolosi ili kuwapa nafasi watoto wenye mahitaji maalumu maana mpaka sasa kuna watoto zaidi ya 25 wenye mahitaji maalumu lakini miundombinu sio rafiki sana kwao

Sauda Mwendo na Angel Juma wanafunzi kutoka shule ya sekondari Makongolosi wamewawakilisha watoto wenzao wa Mkoa wa Mbyea kusoma Risala kwa Mgeni Rasmi ambapo wamesema Ndoa za utotoni, ubakaji,kubakwa, kufichwa kwa watoto wenye ulemavu na mengine mengi bado yanawakabili watoto wa Mbeya huku wakisema wanafamilia kukaa na kumalizana na ndugu wanaobainika kufanya vitendo hivyo kunapelekea watoto kuendelea kutokuwa salama katika maisha yao ya kila siku

Ndoa za utotoni, ubakaji na ulawiti, kufichwa kwa watoto wenye ulemavu pamoja na mambo mengine bado yanaendelea kututesa watoto na ndugu wanapokaa na kumalizana na ndugu waliobainika kufanya vitendo vya kikatili kwa watoto bado vinaendelea kufanya watoto kutokuwa salama, Hivyo tunaomba kila mtu atekeleze jukumu lake ili sisi watoto tuweze kuwa slama.

Matangazo

  • ORODHA YA WALIOITWA KWENYE MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA MPIGA KURA JIMBO LA LUPA December 21, 2024
  • Tangazo la Kuitwa kwenye usaili Kazi za MUDA ZA MAKARANI NA WASIMAMIZI WA SENSA 2022 July 17, 2022
  • Orodha ya walioitwa kwenye usaili Maombi ya kazi za sensa_Chunya_2022 July 17, 2022
  • ORODHA YA MAJINA YA WALIOITWA KWENYE USAILI 2022, HALMASHAURI YA WILAYA YA CHUNYA July 22, 2022
  • Zaidi

Habari Mpya

  • ZINGATIENI WELEDI NA UFANISI KAMA MLIVYOAMINIWA

    April 29, 2025
  • MAAFISA HABARI NA WAANDISHI WA HABARI KUNOLEWA ZAIDI JUU YA AFYA YA AKILI.

    April 16, 2025
  • DC CHUNYA NA SONGWE WAPELEKA OMBI MOJA KWA WAZIRI.

    April 04, 2025
  • TARAFA YA KIPEMBAWE CHUNYA YAJIDHATITI KUWATUMIKIA WANANCHI.

    March 21, 2025
  • Zaidi

Video

BILIONI 2.2 BAJETI YA TARURA WILAYA YA CHUNYA, SERIKALI TUNASHUKURU
video zaidi

Kiunganishi cha haraka

  • HATUA ZA KUANZISHA BIASHARA
  • MIONGOZO MBALIMBALI
  • FOMU ZA HUDUMA MBALIMBALI

Tovuti Nyingine Tunazohusiana

  • OR-TAMISEMI
  • BARAZA LA MITIHANI
  • majukumu ya Mamlaka ya Serikali Mtandao na Sheria ya Serikali Mtandao kwa ujumla
  • MKOA WA MBEYA
  • WIZARA YA ELIMU SAYANSI NA TEKNOLOJIA
  • WAKALA WA SERIKALI MTANDAO

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Ramani ya Mahali

wasiliana nasi

    Itigi Road

    sanduku la posta: P.O box 73 Chunya

    simu ya mezani: 025 2520121

    simu ya mkononi: 025 2520121

    Barua pepe: ded@chunyadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera binafsi
    • kanusho
    • MMM
    • Ramani elekezi
    • Huduma

Copyright ©2017 Chunya District Council . All rights reserved.